< 1 Wafalme 11 >

1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
Et le Roi Salomon aima des femmes étrangères en grand nombre, et d'abord la fille de Pharaon, puis des Moabites, des Ammonites, des iduméennes, des Sidoniennes, des Héthiennes,
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
appartenant aux peuples desquels l'Éternel avait dit aux enfants d'Israël: Vous n'entrerez point chez eux, et ils n'entreront point chez vous; certainement ils tourneront votre cœur du côté de leurs dieux; c'est à eux que Salomon s'attacha par l'amour.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Et il avait en femmes sept cents princesses et trois cents concubines; et ses femmes firent dévier son cœur.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
Et à l'époque de la vieillesse de Salomon ses femmes tournèrent son cœur du côté d'autres dieux, et son cœur ne fut pas sans partage avec l'Éternel, son Dieu, comme le cœur de David, son père.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
Et Salomon se mit à la suite d'Astarté, divinité des Sidoniens, et de Milcom, l'Abominable des Ammonites.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
Et Salomon fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et il ne s'attacha point complètement à l'Éternel comme David, son père.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
Alors Salomon éleva un tertre à Camos, l'Abominable des Moabites, sur la montagne située devant Jérusalem, et à Moloch, l'Abominable des Ammonites.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
Et ainsi fit-il pour toutes ses femmes étrangères qui offraient de l'encens et des sacrifices à leurs dieux.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
Et l'Éternel se courrouça contre Salomon parce qu'il avait détourné son cœur de l'Éternel, Dieu d'Israël, qui lui était apparu deux fois,
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
et lui avait donné sur ce point un ordre exprès en lui défendant de s'attacher à d'autres dieux; mais Salomon n'observa point la défense de l'Éternel.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Et l'Éternel dit à Salomon: Puisque tu t'es ainsi comporté, et que tu n'as pas gardé mon alliance et mes statuts que je t'avais prescrits, je t'arracherai le royaume et le donnerai à ton serviteur;
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
cependant je ne le ferai pas de ton vivant, pour l'amour de David, ton père; c'est de la main de ton fils que je l'arracherai;
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
seulement ce n'est pas la totalité du royaume que je détacherai; je laisserai une Tribu à ton fils pour l'amour de David, mon serviteur, et pour l'amour de Jérusalem que j'ai choisie.
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
Et l'Éternel suscita un adversaire à Salomon, Hadad, l'Iduméen, de la race royale qui régnait en Edom.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Et il arriva, David étant en Idumée, lorsque Joab, général de l'armée, eut gagné les hauteurs pour donner la sépulture aux morts, que celui-ci massacra tous les mâles de l'Idumée
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
(car Joab y resta six mois avec tous les Israélites jusqu'à ce qu'il eût exterminé tous les mâles de l'Idumée);
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
alors Hadad, ayant avec lui des Iduméens d'entre les serviteurs de son père, prit la fuite pour gagner l'Egypte; or Hadad était encore un jeune garçon.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
Et après être partis de Madian, ils atteignirent Pharan, et de Pharan ils emmenèrent du monde avec eux et ils arrivèrent en Egypte chez Pharaon, roi d'Egypte, lequel lui donna une demeure, et lui assigna des subsistances et lui concéda des terres.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
Et Hadad trouva à un haut degré grâce aux yeux de Pharaon, qui lui donna en mariage la sœur de sa femme, la sœur de la reine Thachpenès.
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
Et la sœur de Thachpenès lui enfanta Genubath, son fils; et Thachpenès fit son sevrage au palais de Pharaon, et Genubath fut dans le palais de Pharaon au milieu des fils de Pharaon.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
Et Hadad ayant appris en Egypte que David reposait avec ses pères, et que Joab, général de l'armée, était mort, Hadad alors dit à Pharaon: Laisse-moi libre de retourner dans mon pays.
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
Et Pharaon lui dit: Mais, que te manque-t-il chez moi? Et te voilà cherchant à aller dans ton pays! Et il reprit: Non, mais laisse, laisse-moi partir!
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
En outre Dieu suscita à Salomon un adversaire dans Rezon, fils d'Eljada, déserteur d'Hadadézer, roi de Tsoba, son maître.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
Et il ramassa auprès de lui des hommes, et devint chef de bande, lorsque David en fit le carnage (des Syriens); et ils se portèrent à Damas, et ils s'y maintinrent, et dominèrent à Damas.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
Et il fut un adversaire pour Israël durant toute la vie de Salomon. Et quant au mal que fit Hadad, il harcela Israël et il régna sur la Syrie.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Et aussi Jéroboam, fils de Nebat, Ephraïmite de Tsérèda (or sa mère, veuve, s'appelait Tserua), sujet de Salomon, leva la main contre le Roi.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
Et voici la cause pour laquelle il leva la main contre le Roi: Salomon construisait la Redoute et fermait la brèche de la Cité de David, son père.
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
Et le personnage, Jéroboam, était un brave, un homme de ressource, et Salomon voyant dans le jeune homme de l'aptitude à l'œuvre, le préposa sur tous les gens de charge de la maison de Joseph…
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
Et il arriva dans ce temps-là que Jéroboam, étant sorti de Jérusalem, fut rencontré par Ahia, de Silo, le prophète, dans la route; or Ahia portait un manteau neuf, et ils étaient seuls dans la campagne.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
Alors Ahia prit le manteau neuf qu'il avait sur lui et le déchira en douze morceaux
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
et dit à Jéroboam: Prends pour toi dix morceaux; car ainsi parle l'Éternel, Dieu d'Israël: Voici, je vais arracher le royaume de la main de Salomon, et te remettre les dix Tribus;
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
mais une Tribu lui restera en considération de mon serviteur David et en considération de Jérusalem, la ville que j'ai choisie dans la totalité des Tribus d'Israël,
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
parce que l'on m'a abandonné et que l'on a adoré Astarté, divinité des Sidoniens, Camos, dieu de Moab, et Milcom, dieu des Ammonites, et que l'on n'a pas pratiqué mes voies pour accomplir ce qui est droit à mes yeux, ni mes statuts, ni mes lois, comme David, son père.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
Cependant je ne lui arracherai pas de la main la totalité du royaume, mais je lui laisserai sa place de Prince sa vie durant, en considération de David, mon serviteur, que j'ai choisi et qui a gardé mes commandements et mes statuts,
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
et j'arracherai le royaume de la main de son fils, et te donnerai les dix Tribus; quant à son fils,
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
je lui laisserai une Tribu, afin que mon serviteur David ait dans tous les temps une lampe devant moi à Jérusalem, la ville que je me suis choisie pour y placer mon Nom.
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
Et je te prendrai pour que tu règnes sur tout ce qu'ambitionne ton âme et deviennes roi d'Israël.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
Et si tu obéis à tout ce que je te commanderai, et pratiques mes voies et fais ce qui est droit à mes yeux, gardant mes statuts et mes commandements, comme l'a fait David, mon serviteur, alors je serai avec toi et t'édifierai une maison stable, comme je l'ai édifiée à David, et je te donnerai Israël
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
et j'humilierai la race de David à cet effet, seulement pas pour toujours. —
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
Et Salomon cherchait à se défaire de Jéroboam; alors Jéroboam partit, et s'enfuit en Egypte chez Sisac, roi d'Egypte, et il fut en Egypte jusqu'à la mort de Salomon.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
Et le reste de l'histoire de Salomon, et tous ses actes et sa sagesse sont consignés dans le livre de l'histoire de Salomon.
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Et le temps que Salomon régna à Jérusalem sur tout Israël, fut quarante années.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Salomon reposa à côté de ses pères et reçut la sépulture dans la ville de David, son père. Et Roboam, son fils, régna à sa place.

< 1 Wafalme 11 >