< 1 Wafalme 11 >

1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
Or le Roi Salomon aima plusieurs femmes étrangères, outre la fille de Pharaon; [savoir] des Moabites, des Hammonites, des Iduméènnes, des Sidoniènnes et des Héthiènes;
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
Qui étaient d'entre les nations dont l'Eternel avait dit aux enfants d'Israël: Vous n'irez point vers elles, et elles ne viendront point vers vous; [car] certainement elles feraient détourner votre cœur pour suivre leurs dieux. Salomon s'attacha à elles, et les aima.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Il eut donc sept cents femmes Princesses, et trois cents concubines; et ses femmes firent égarer son cœur.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
Car il arriva sur le temps de la vieillesse de Salomon, que ses femmes firent détourner son cœur après d'autres dieux; et son cœur ne fut point droit devant l'Eternel son Dieu, comme avait été le cœur de David son père.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
Et Salomon marcha après Hastaroth, la divinité des Sidoniens, et après Milcom, l'abomination des Hammonites.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
Ainsi Salomon fit ce qui déplaît à l'Eternel, et il ne persévéra point à suivre l'Eternel, comme [avait fait] David son père.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
Et Salomon bâtit un haut lieu à Kémos, l'abomination des Moabites, sur la montagne qui est vis-à-vis de Jérusalem; et à Molec, l'abomination des enfants de Hammon.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
Il en fit de même pour toutes ses femmes étrangères, qui faisaient des encensements et qui sacrifiaient à leurs dieux.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
C'est pourquoi l'Eternel fut irrité contre Salomon, parce qu'il avait détourné son cœur de l'Eternel le Dieu d'Israël, qui lui était apparu deux fois;
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
Et qui même lui avait fait ce commandement exprès, qu'il ne marchât point après d'autres dieux; mais il ne garda point ce que l'Eternel lui avait commandé.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Et l'Eternel dit à Salomon: Parce que ceci a été en toi, que tu n'as pas gardé mon alliance et mes ordonnances que je t'avais prescrites, certainement je déchirerai le Royaume, afin qu'il ne soit plus à toi, et je le donnerai à ton serviteur.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
Toutefois pour l'amour de David ton père je ne le ferai point en ton temps; ce sera d'entre les mains de ton fils que je déchirerai le Royaume.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
Néanmoins je ne déchirerai pas tout le Royaume, j'en donnerai une Tribu à ton fils, pour l'amour de David mon serviteur, et pour l'amour de Jérusalem, que j'ai choisie.
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
L'Eternel donc suscita un ennemi à Salomon, [savoir] Hadad Iduméen, qui était de la race Royale d'Edom.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Car il était arrivé qu'au temps que David était en Edom, lorsque Joab Chef de l'armée monta pour ensevelir ceux qui avaient été tués, comme il tuait tous les mâles d'Edom;
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
(Car Joab demeura là six mois avec tout Israël, jusqu'à ce qu'il eût exterminé tous les mâles d'Edom, )
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
Hadad s'était enfui, avec quelques Iduméens qui étaient d'entre les serviteurs de son père, pour se retirer en Egypte; et Hadad était [alors] fort jeune.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
Et quand ils furent partis de Madian, ils vinrent à Paran, et prirent avec eux des gens de Paran, et se retirèrent en Egypte vers Pharaon Roi d'Egypte, qui lui donna une maison, et lui assigna de quoi vivre, et lui donna aussi une terre.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
Et Hadad fut fort dans les bonnes grâces de Pharaon, de sorte qu'il le maria à la sœur de sa femme, la sœur de la Reine Tachpenès.
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
Et la sœur de Tachpenès lui enfanta son fils Guénubath, que Tachpenès sevra dans la maison de Pharaon. Ainsi Guénubath était de la maison de Pharaon, entre les fils de Pharaon.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
Or quand Hadad eut appris en Egypte que David s'était endormi avec ses pères, et que Joab Chef de l'armée était mort, il dit à Pharaon: Donne-moi [mon] congé, et je m'en irai en mon pays.
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
Et Pharaon lui répondit: Mais de quoi as-tu besoin étant avec moi, pour demander ainsi de t'en aller en ton pays? et il dit: [Je n'ai besoin] de rien; mais cependant donne-moi mon congé.
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
Dieu suscita aussi un [autre] ennemi à Salomon, [savoir] Rézon fils d'Eljadah, qui s'en était fui d'avec son Seigneur Hadar-hézer, Roi de Tsoba,
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
Qui assembla des gens contre lui, et fut Chef de quelques bandes, quand David les défit; et ils s'en allèrent à Damas, et y demeurèrent, et y régnèrent.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
[Rézon] donc fut ennemi d'Israël tout le temps de Salomon, outre le mal que fit Hadad; et il donna du chagrin à Israël, et régna sur la Syrie.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Jéroboam aussi fils de Nébat, Ephratien, de Tséréda, dont la mère avait nom Tséruha, femme veuve, serviteur de Salomon, s'éleva contre le Roi.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
Et ce fut ici l'occasion pour laquelle il s'éleva contre le Roi; c'est que quand Salomon bâtissait Millo, [et] comblait le creux de la Cité de David son père;
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
Là se trouva Jéroboam, qui était un homme fort et vaillant; et Salomon voyant que ce jeune homme travaillait, le commit sur toute la charge de la maison de Joseph.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
Or il arriva en ce même temps, que Jéroboam étant sorti de Jérusalem, Ahija Silonite, Prophète, vêtu d'une robe neuve, le trouva dans le chemin, et ils étaient eux deux tout seuls aux champs.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
Et Ahija prit la robe neuve qu'il avait sur lui, et la déchira en douze pièces;
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
Et il dit à Jéroboam: Prends-en pour toi dix pièces; car ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël: Voici, je m'en vais déchirer le Royaume d'entre les mains de Salomon, et je t'en donnerai dix Tribus.
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
Mais il en aura une Tribu, pour l'amour de David mon serviteur, et pour l'amour de Jérusalem, qui est la ville que j'ai choisie d'entre toutes les Tribus d'Israël.
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
Parce qu'ils m'ont abandonné, et se sont prosternés devant Hastaroth le dieu des Sidoniens, devant Kémos le dieu de Moab, et devant Milcom le dieu des enfants de Hammon, et qu'ils n'ont point marché dans mes voies, pour faire ce qui est droit devant moi, et [pour garder] mes statuts, et mes ordonnances, comme [avait fait] David, père de Salomon.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
Toutefois je n'ôterai rien de ce Royaume d'entre ses mains; car tout le temps qu'il vivra je le maintiendrai Prince, pour l'amour de David mon serviteur que j'ai choisi, [et] qui a gardé mes commandements et mes statuts.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
Mais j'ôterai le Royaume d'entre les mains de son fils, et je t'en donnerai dix Tribus.
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
Et j'en donnerai une Tribu à son fils, afin que David mon serviteur ait une Lampe à toujours devant moi dans Jérusalem, qui est la ville que j'ai choisie pour y mettre mon Nom.
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
Je te prendrai donc, et tu régneras sur tout ce que ton âme souhaitera, et tu seras Roi sur Israël.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
Et il arrivera que si tu m'obéis en tout ce que je te commanderai, et que tu marches dans mes voies, et que tu fasses tout ce qui est droit devant moi, en gardant mes statuts et mes commandements, comme a fait David mon serviteur, je serai avec toi, et je te bâtirai une maison qui sera stable, comme j'en ai bâti [une] à David, et je te donnerai Israël.
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
Ainsi j'affligerai la postérité de David à cause de cela, mais non pas à toujours.
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
Salomon donc chercha de faire mourir Jéroboam; mais Jéroboam se leva, et s'enfuit en Egypte vers Sisak Roi d'Egypte; et il demeura en Egypte jusqu'à la mort de Salomon.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
r le reste des faits de Salomon, tout ce qu'il a fait, et sa sagesse, cela n'est-il pas écrit au Livre des faits de Salomon?
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Or le temps que Salomon régna à Jérusalem sur tout Israël fut quarante ans.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ainsi Salomon s'endormit avec ses pères, et il fut enseveli dans la Cité de David son père; et Roboam son fils régna en sa place.

< 1 Wafalme 11 >