< 1 Wafalme 11 >
1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
Le roi Salomon aimait beaucoup de femmes étrangères, ainsi que la fille de Pharaon: des femmes des Moabites, des Ammonites, des Édomites, des Sidoniens et des Hittites,
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
des nations au sujet desquelles Yahvé a dit aux enfants d'Israël: « Vous n'irez pas au milieu d'elles, et elles n'entreront pas au milieu de vous, car elles détourneront certainement votre cœur de leurs dieux ». Salomon s'unit à elles par amour.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Il eut sept cents femmes, des princesses, et trois cents concubines. Ses femmes détournèrent son cœur.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
Lorsque Salomon fut âgé, ses femmes détournèrent son cœur vers d'autres dieux, et son cœur ne fut pas parfait avec l'Éternel, son Dieu, comme l'avait été le cœur de David, son père.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
Car Salomon alla après Ashtoreth, la déesse des Sidoniens, et après Milcom, l'abomination des Ammonites.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
Salomon fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et il ne suivit pas entièrement l'Éternel, comme avait fait David, son père.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
Et Salomon bâtit un haut lieu à Kemosh, l'abomination de Moab, sur la montagne qui est devant Jérusalem, et à Moloch, l'abomination des Ammonites.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
Il fit de même pour toutes ses femmes étrangères, qui brûlaient de l'encens et offraient des sacrifices à leurs dieux.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
L'Éternel fut irrité contre Salomon, parce que son cœur s'était détourné de l'Éternel, le Dieu d'Israël, qui lui était apparu deux fois,
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
et lui avait donné l'ordre de ne pas aller après d'autres dieux; mais il ne garda pas ce que l'Éternel avait ordonné.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Yahvé dit à Salomon: « Puisque tu as agi de la sorte et que tu n'as pas gardé mon alliance et mes lois que je t'ai prescrites, je t'arracherai le royaume et je le donnerai à ton serviteur.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
Cependant, je ne le ferai pas de ton vivant, à cause de David, ton père, mais je l'arracherai de la main de ton fils.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
Cependant, je n'arracherai pas tout le royaume; mais je donnerai une tribu à ton fils, à cause de David, mon serviteur, et à cause de Jérusalem, que j'ai choisie. »
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
Yahvé suscita un adversaire à Salomon: Hadad, l'Édomite. Il était l'un des descendants du roi en Édom.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Comme David était en Édom, et que Joab, chef de l'armée, était monté pour enterrer les morts et avait frappé tous les mâles d'Édom
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
(car Joab et tout Israël restèrent là six mois, jusqu'à ce qu'il eût tué tous les mâles d'Édom),
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
Hadad s'enfuit, lui et quelques Édomites des serviteurs de son père avec lui, pour aller en Égypte, alors qu'Hadad était encore un petit enfant.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
Ils se levèrent de Madian et arrivèrent à Paran; ils prirent avec eux des hommes de Paran, et ils allèrent en Égypte, chez Pharaon, roi d'Égypte, qui lui donna une maison, le nourrit et lui donna des terres.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
Hadad trouva une grande faveur aux yeux de Pharaon, de sorte qu'il lui donna pour femme la sœur de sa propre femme, la sœur de la reine Tahpenes.
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
La sœur de Tahpenes lui enfanta son fils Genubath, que Tahpenes sevra dans la maison de Pharaon; et Genubath fut dans la maison de Pharaon parmi les fils de Pharaon.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
Lorsque Hadad apprit en Égypte que David s'était couché avec ses pères et que Joab, chef de l'armée, était mort, il dit à Pharaon: « Laisse-moi partir, et je m'en irai dans mon pays. »
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
Alors Pharaon lui dit: « Mais qu'est-ce qui t'a manqué avec moi, pour que tu cherches à aller dans ton pays? » Il répondit: « Rien, mais laissez-moi partir. »
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
Dieu lui suscita un adversaire, Rezon, fils d'Eliada, qui s'était enfui de chez son seigneur, Hadadézer, roi de Tsoba.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
Il rassembla des hommes pour lui et devint chef d'une troupe, lorsque David tua ceux de Tsoba. Ils allèrent à Damas, y habitèrent, et régnèrent à Damas.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
Il fut un adversaire d'Israël pendant toute la durée de Salomon, en plus des méfaits d'Hadad. Il avait Israël en horreur, et il régnait sur la Syrie.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Jéroboam, fils de Nebath, Éphraïmite de Zéreda, serviteur de Salomon, dont la mère s'appelait Zéroua et qui était veuve, leva aussi la main contre le roi.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
Voici la raison pour laquelle il leva la main contre le roi: Salomon bâtit Millo, et répara la brèche de la ville de David, son père.
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
Jéroboam était un homme fort et vaillant; Salomon vit que le jeune homme était laborieux, et il le chargea de tous les travaux de la maison de Joseph.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
En ce temps-là, lorsque Jéroboam sortit de Jérusalem, le prophète Achija, le Shilonite, le trouva en chemin. Achija s'était revêtu d'un vêtement neuf, et ils étaient tous deux seuls dans les champs.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
Achija prit le vêtement neuf qui était sur lui, et le déchira en douze morceaux.
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
Il dit à Jéroboam: « Prends dix morceaux; Car Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: Voici que j'arrache le royaume de la main de Salomon et que je te donne dix tribus
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
(mais il n'aura qu'une seule tribu, à cause de mon serviteur David et de Jérusalem, la ville que j'ai choisie parmi toutes les tribus d'Israël),
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
parce qu'ils m'ont abandonné et qu'ils se sont prosternés devant Ashtoreth, la déesse des Sidoniens, Kemosh, le dieu de Moab, et Milcom, le dieu des enfants d'Ammon. Ils n'ont pas marché dans mes voies, pour faire ce qui est droit à mes yeux, et pour observer mes lois et mes ordonnances, comme l'a fait David, son père.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
"'Cependant, je n'enlèverai pas tout le royaume de sa main, mais je l'établirai prince tous les jours de sa vie, à cause de David, mon serviteur, que j'ai choisi et qui a gardé mes commandements et mes lois.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
Mais j'enlèverai le royaume de la main de son fils et je vous le donnerai, à vous, dix tribus.
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
Je donnerai une tribu à son fils, afin que David, mon serviteur, ait toujours une lampe devant moi à Jérusalem, la ville que je me suis choisie pour y mettre mon nom.
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
Je te prendrai, et tu régneras selon tout ce que ton âme désire, et tu seras roi d'Israël.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
Si tu écoutes tout ce que je te commande, si tu marches dans mes voies, si tu fais ce qui est droit à mes yeux, si tu observes mes lois et mes commandements, comme l'a fait David, mon serviteur, je serai avec toi, je te bâtirai une maison solide, comme je l'ai bâtie à David, et je te donnerai Israël.
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
J'affligerai la descendance de David pour cela, mais pas pour toujours.'"
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
Salomon chercha à tuer Jéroboam, mais celui-ci se leva et s'enfuit en Égypte, chez Shishak, roi d'Égypte, et il resta en Égypte jusqu'à la mort de Salomon.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
Le reste des actes de Salomon, tout ce qu'il a fait, et sa sagesse, ne sont-ils pas écrits dans le livre des actes de Salomon?
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Le temps que Salomon régna à Jérusalem sur tout Israël fut de quarante ans.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Salomon se coucha avec ses pères et fut enterré dans la ville de David, son père; et Roboam, son fils, régna à sa place.