< 1 Wafalme 11 >

1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
Now King Solomon loved many foreign women including the daughter of Pharaoh—women of the Moabites, Ammonites, Edomites, Sidonians, and Hittites.
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
They were from the nations about which Yahweh said to the people of Israel, “You will not go among them to marry, neither will they come among you, for they will certainly turn your heart to their gods.” In spite of this command, Solomon was affectionate toward these women in love.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Solomon had seven hundred royal wives and three hundred concubines. His wives turned his heart away.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
For when Solomon grew old, his wives turned away his heart after other gods; his heart was not fully surrendered to Yahweh his God, as was the heart of David his father.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
For Solomon followed Ashtoreth, the goddess of the Sidonians, and he followed Molech, the disgusting idol of the Ammonites.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
Solomon did what was evil in the sight of Yahweh; he did not fully follow Yahweh as David his father had done.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
Then Solomon built a high place for Chemosh, the disgusting idol of Moab, on a hill east of Jerusalem, and also for Molech, the disgusting idol of the people of Ammon.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
He also built high places for all his foreign wives, who burned incense and sacrificed to their gods at them.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
Yahweh was angry with Solomon, because his heart had turned away from him, the God of Israel, even though he had appeared to him twice
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
and commanded him about this very thing, that he should not go after other gods. But Solomon did not obey what Yahweh commanded.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Therefore Yahweh said to Solomon, “Because you have done this and have not kept the covenant and my statutes that I have commanded you, I will surely tear the kingdom from you and give it to your servant.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
However, for David your father's sake, I will not do it in your lifetime, but I will tear it out of the hand of your son.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
Yet I will not tear away all the kingdom; I will give one tribe to your son for David my servant's sake, and for the sake of Jerusalem, which I have chosen.”
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
Then Yahweh raised up an adversary to Solomon, Hadad the Edomite. He was from the royal family of Edom.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
When David was in Edom, Joab the captain of the army had gone up to bury the dead, every man who had been killed in Edom.
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
Joab and all Israel remained there six months until he had killed every male in Edom.
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
But Hadad was taken with other Edomites by his father's servants into Egypt, since Hadad was still a little child.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
They left Midian and came to Paran, from where they took men with them to Egypt, to Pharaoh king of Egypt, who gave him a house and land and food.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
Hadad found great favor in the sight of Pharaoh, so that Pharaoh gave him a wife, his own wife's sister, the sister of Tahpenes the queen.
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
The sister of Tahpenes gave birth to Hadad's son. They named him Genubath. Tahpenes raised him in Pharaoh's palace. So Genubath lived in Pharaoh's palace among the children of Pharaoh.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
While he was in Egypt, Hadad heard that David had lain down with his ancestors and that Joab the captain of the host was dead, Hadad said to Pharaoh, “Let me depart, so I may go to my own country.”
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
Then Pharaoh said to him, “But what have you lacked with me, that you now seek to go to your own country?” Hadad answered, “Nothing. Please let me go.”
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
God also raised up another adversary to Solomon, Rezon son of Eliada, who had fled from his master Hadadezer king of Zobah.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
Rezon gathered men to himself and became captain over a small force, when David defeated the men of Zobah. Rezon's men went to Damascus and lived there, and Rezon controlled Damascus.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
He was an enemy of Israel all the days of Solomon, along with the trouble that Hadad caused. Rezon abhorred Israel and reigned over Aram.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Then Jeroboam son of Nebat, an Ephraimite of Zeredah, an official of Solomon, whose mother's name was Zeruah, a widow, also lifted up his hand against the king.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
He lifted up his hand against the king because Solomon had built up the place located at Millo and repaired the opening in the city wall of David his father.
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
Jeroboam was a mighty man of valor. Solomon saw that the young man was industrious, so he gave him command over all the labor of the house of Joseph.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
At that time, when Jeroboam went out of Jerusalem, the prophet Ahijah the Shilonite found him on the road. Now Ahijah had dressed in a new garment and the two men were alone in the field.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
Then Ahijah grabbed hold of the new garment that was on him and tore it into twelve pieces.
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
He said to Jeroboam, “Take ten pieces, for Yahweh, the God of Israel, says, 'Look, I will tear the kingdom out of the hand of Solomon and I will give ten tribes to you
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
(but Solomon will have one tribe, for my servant David's sake and for Jerusalem's sake—the city that I have chosen out of all the tribes of Israel),
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
because they have forsaken me and have worshiped Ashtoreth the goddess of the Sidonians, Chemosh the god of Moab, and Molech the god of the people of Ammon. They have not walked in my ways, to do what is right in my eyes, and to keep my statutes and my decrees, as did David his father.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
However, I will not take the whole kingdom out of Solomon's hand. Instead, I have made him ruler all the days of his life, for David my servant's sake whom I chose, the one who kept my commandments and my statutes.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
But I will take the kingdom out of his son's hand and I will give it to you, ten tribes.
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
I will give one tribe to Solomon's son, so that David my servant may always have a lamp before me in Jerusalem, the city in which I have chosen to put my name.
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
I will take you, and you will rule to fulfill all that you desire, and you will be king over Israel.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
If you listen to all that I command you, and if you walk in my ways and do what is right in my eyes, to keep my statutes and my commandments, as David my servant did, then I will be with you and will build you a sure house, as I built for David, and will give Israel to you.
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
I will punish the descendants of David, but not forever.'”
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
So Solomon tried to kill Jeroboam. But Jeroboam got up and fled into Egypt, to Shishak king of Egypt, and he remained in Egypt until the death of Solomon.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
As for the other matters concerning Solomon, all that he did and his wisdom, are they not written in the book of the events of Solomon?
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Solomon reigned in Jerusalem over all Israel for forty years.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
He slept with his ancestors and he was buried in the city of David his father. Rehoboam his son became king in his place.

< 1 Wafalme 11 >