< 1 Wafalme 11 >

1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
[撒羅滿敬拜邪神]撒羅滿除了法郎的公主外,又愛上了許多外國女子:即摩阿布女子,阿孟女子,厄東女子,漆冬女子,赫特女子。
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
關於這些民族,上主曾吩咐以色列子民說:「你們不可到他們中間去,他們也不可到你們中間來,否則他們必會引誘你們的心,傾向他們的神。」但是,撒羅滿卻戀愛這些女子。
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
他有七百個各地公主為妻妾,另外還有三百妃子;這些妻妾終於敗壞了他的心。
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
當撒羅滿年老的時候,這些妻妾迷惑了他的心,勾引他去崇拜別的神;他的心已不像他父親達味的心,全屬於上主他的天主。
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
這樣,他隨從了漆冬人的女神阿市托勒特和阿孟人的可憎之物米耳公。
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
撒羅滿作了上主眼中視為惡的事,不像他父親達味那樣全心服從上主。
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
那時,撒羅滿在耶路撒冷東面的山上,為摩阿布人的可憎之物革摩士,為阿孟子民的可憎之物摩肋客,修築了丘壇。
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
他為所有的外國妻妾,都修築了丘壇,各給自己的神焚香獻祭。上主發怒警告
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
上主遂向撒羅滿發怒,因為他的心偏離了兩次顯現給他的上主以色列的天主。
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
當時,上主對此事曾吩咐過他,不可去隨從別的神,但他卻沒有遵守上主的命令。
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
於是,上主對撒羅滿說:「你既然這樣行事,不遵守我的盟約,和我吩咐你的誡命,我必要奪去你的王國,賜給你的一個臣僕。
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
雖然如此,但為了你父親達味的緣故,在你有生之日,我不作這事;我將要由你兒子手中奪去。
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
但是仍不完全奪去,為了我僕人達味和我所揀選的耶路撒冷,我仍給你的兒子留下一支派。」撒羅滿的外患
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
那時,上主興起一個反抗撒羅滿的人,就是厄東王的後裔,厄東人哈達得。
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
當達味打敗厄東後,軍長約阿布前去埋葬陣亡的人時,殺了厄東所有的男子;
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
約阿布和全以色列在厄東逗留了六個月,直到將厄東所有的男子完全殺掉。
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
哈達得卻同他父親的幾個臣僕厄東人逃往埃及,那時哈達得還很年輕。
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
他們從米德楊起身,到了帕蘭,從帕蘭又帶了些人到埃及,投奔埃及王法郎;法郎給了他一座房屋,供給他食用,又給了他一塊土地。
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
哈達得在法郎眼前很是得寵,因此將自己的妻子塔培乃斯王后的妹妹,嫁給他為妻。
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
塔培乃斯的妹妹給哈達得生了一個兒子叫革奴巴特。塔培乃斯在法郎宮中撫養他,因此革奴巴特便住在法郎宮中,同法郎的公子們一起。
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
哈達得在埃及聽說達味已與他的列祖同眠,軍長約阿布也已去世,便對法郎說:「請讓我走,回到我故鄉去! 」
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
法郎對他說:「你在我這裏缺少什麼,竟想回到你的故鄉去﹖」他回答說:「什麼也不缺,只求你讓我回去! 」
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
天主又興起一個反抗撒羅滿的人,就是厄肋雅達的兒子勒宗。他由自己的主人祚巴王哈達德則爾前出走。
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
在達味擊殺阿蘭人時,聚集了一些人,作了土匪頭目,去了大馬士革,盤踞在那裏,做了大馬士革王。
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
撒羅滿有生之日,勒宗始終與以色列為敵。哈達得就回了國。哈達得的危害,即在於他作了厄東的君王,不斷騷擾以色列。撒羅滿的內憂
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
厄弗辣大地責勒達人,乃巴特的兒子雅洛貝罕,─他的母親名叫責魯阿,是個寡婦─原是撒羅滿的臣僕,他也起來反抗君王。
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
他反抗君王的原委是這樣:當時撒羅滿正在建築米羅,修葺他父親達味城的裂口;
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
雅洛貝罕這個人原很有才能,撒羅滿見這少年人很能做事,便派他監督若瑟族的一切勞役。
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
有一次,雅洛貝罕走出耶路撒冷,史羅的先知阿希雅在路上遇見了他;先知身上穿著一件新外衣,在田間只有他們二人。
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
阿希雅便拿起他所穿的新外衣,撕成了十二塊,
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
然後對雅洛貝罕說:「你拿十塊,因為上主以色列的天主這樣說:看,我必將撒羅滿手中的王國撕裂,將十個支派交給你。
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
為了我僕人達味,和我從以色列支派中選的耶路撒冷城的緣故,仍給他留下一支派,
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
因為他背棄了我,崇拜了漆冬人的女神阿市托勒特、摩阿布人的神革摩士和阿孟人的神米耳公。他沒有像他父親達味那樣履行我的道路,行我視為正義的事,恪守我的律例和誡命。
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
但我不願從他手中奪去整個王國,我要使他有生之日作首領,是為了我所選的僕人達味的緣故,因為他遵守了我的誡命和律例。
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
我卻意從他兒子的手中奪回王國,給你十個支派,
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
只留下一個支派給他的兒子,使我的僕人達味,在我所揀選立我名的耶路撒冷城中,在我面前常有一盞明燈。
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
我選取你,使你隨意統治一切,作以色列的君王。
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
如果你聽從我吩咐你的一切,履行我的道路,行我視為正義的事,恪守我的律例和誡命,如同我的僕人達味一樣,我必與你同在,為你建立一鞏固的家室,像我為達味所建立的一樣。我將以色列交給你,
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
藉以貶抑達味的後裔,但不致於久遠。」
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
因此,撒羅滿想殺害雅洛貝罕,雅洛貝罕遂起身逃往埃及,投奔埃及王史沙克;他住埃及,直到撒羅滿逝世。撒羅滿逝世
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
撒羅滿其餘的事蹟,他的一切作為和智慧,都記載在撒羅滿實錄上。
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
撒羅滿在耶路撒冷作王,統治全以色列,凡四十年。
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
撒羅滿與他的列祖同眠,葬在他父親達味城內;他的兒子勒哈貝罕繼位為王。

< 1 Wafalme 11 >