< 1 Wafalme 11 >
1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
А цар Соломон залюби, освен Фараоновата дъщеря, много чужденки, моавки, амонки, едомки, сидонки, хетейки,
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
от народите за които Господ каза на израилтяните: Не влизайте при тях, нито те да влизат при вас, за да не преклонят сърцата ви към боговете си. Към тях Соломон се страстно прилепи.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Имаше седемстотин жени княгини и триста наложници; и жените му отвърнаха сърцето му.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
Защото, когато остаря Соломон, жените му преклониха сърцето му към други богове; и сърцето му не беше съвършено пред Господа неговия Бог, както сърцето на баща му Давида.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
Защото Соломон отиде след Астарта, богинята на сидонците, и след Мелхома, мерзостта на амонците.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
Така Соломон стори зло пред Господа, и не следваше съвършено Господа, както беше сторил баща му Давид.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
В това време Соломон издигна високо място на Хамоса, мерзостта на Моава, и на Молоха, мерзостта на амонците, в хълма, който е срещу Ерусалим.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
Така направи и за всичките си чужденки жени, които кадяха и жертвуваха на боговете си.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
Така направи и за всичките си чужденки жени, които кадяха и жертвуваха на боговете си.
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
А Господ се разгневи на Соломона, понеже сърцето му се отвърна от Господа Израилевия Бог, Който му се яви два пъти.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Затова, Господ каза на Соломона: Понеже това е сторено от тебе, и ти не опази завета Ми о повеленията, които ти заповядах, непременно ще откъсна царството от тебе, и ще го дам на слугите ти.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
Но заради баща ти Давида, в твоите дни няма да направя това; от ръката на сина ти що го откъсна.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
Обаче, няма да откъсна цялото царство; едно племе ще дам на сина ти, заради слугата Ми Давида и заради Ерусалим, който избрах.
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
След това, Господ подигна противник на Соломона, едомеца Адад, който бе от царското потекло в Едом.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Защото, когато Давид бе в Едом, и военачалникът Иоав възлезе да погребе избитите, като беше убил всекиго от мъжки пол в Едом,
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
(понеже Иоав седя там с целия Израил шест месеца, докато изтреби всекиго от мъжки пол в Едом),
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
Адад побягна, и с него няколко едомци от слугите на баща му, за да отидат в Египет; а Адат беше още малко дете.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
Като станаха от Мадиам, дойдоха във Фаран; и вземайки със себе си мъже от Фаран, дойдоха в Египет при египетския цар Фараон, който му даде къща, определи му храна и му даде земя.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
И Адад придоби голямо благоволение пред Фараона, така щото той му даде за жена балдъза си, сестра на царицата Тахпенеса,
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
И Тахпенесината сестра му роди сина му Генуват, когото Тахпенеса отби във Фараоновата къща; и Генуват бе в дома на Фараона между неговите синове.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
И когато Адад чу в Египет, че Давид заспал с бащите си, и че военачалникът Иоав умрял, Адад каза на Фараона: Отпусни ме да си отида в моята страна.
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
А Фараон му каза: Ами от що си лишен при мене та искаш да отидеш в страната си? И отговори: От нищо; но както и да е, отпусни ме.
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
Бог му подигна и друг противник, Резона Елиадевия син, който бе побягнал от господаря си Ададзера, софския цар.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
И който, като събра около себе си мъже, стана главатар на чета, когато Давид порази совците; и те отидоха в Дамаск та се зеселиха там, и царуваха в Дамаск.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
Той бе противник на Израиля през всичките Соломонови дни; и освен пакостите които направи Адад, Резон досаждаше на Израиля като царуваше над Сирия.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Също и Еревоам Наватовия син, ефремец от Сарида, Соломонов слуга, чиято майка, една вдовица, се наричаше Серуа, и той дигна ръка против царя.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
А ето причината, по която той дигна ръка против царя: Соломон беше съградил Мило, и когато поправяше разваленото в стената на града на баща си Давида,
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
тоя Еровоам, човек силен и храбър, бе там; и Соломон, като видя, че момъкът беше способен за работа, постави го надзирател над всичката работа наложена върху Иосифовия дом.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
А в това време, като беше излязъл Еровоам из Ерусалим, намери го на пътя пророк Ахия силонецът, облечен в нова дреха; и двамата бяха сами на полето.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
И Ахия хвана новата дреха, която носеше, и разкъса я на дванадесет части.
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
И рече на Еровоама: Вземи си десет части; защото така казва Господ Израилевият Бог: Ето, ще откъсна царството от Соломоновата ръка, и ще дам на тебе десет племена;
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
(ще остане, обаче, нему едни племе, заради слугата Ми Давида, и заради Ерусалим, града който избрах между всичките Израилеви племена);
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
защото оставиха Мене та послужиха на Астарта, богинята на сидонците, на Хамоса, бога на моавците, и на Мелхома, бога на амонците, и не ходиха в пътищата Ми, да вършат онова, което е право пред Мене, и да пазят повеленията Ми, и съдбите Ми, както правеше баща му Давид.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
Не ща, обаче, да отнема цялото царство от ръката му, но ще го поставя владетел през всичките дни на живота ме, заради слугата Ми Давида, когото избрах, защото той пазеше заповедите Ми и повеленията Ми.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
Обаче, ще отнема царството от ръката на сина му, и ще го дам на тебе, сиреч, десет племена;
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
А на сина му ще дам едно племе, тъй щото слугата Ми Давид да има всякога светилник пред мене в Ерусалим, в града, който избрах за себе Си, за да настаня там името Си.
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
А тебе ще взема, и ти ще царуваш над всичко, което желае душата ти, и ще бъдеш цар над Израиля.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
И ако слушаш всичко, което ти заповядвам, и ходиш в пътищата Ми, и вършиш всичко, което е право пред Мене, като пазиш повеленията Ми и заповедите Ми, както правеше слугата Ми Давид, тогава ще бъда с тебе, и ще ти съградя непоклатим дом, както съградих на Давида, и ще ти дам Израиля.
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
И чрез това ще оскърбя Давидовия род, но не за винаги.
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
Затова, Соломон поиска да убие Еровоама. А Еровоам, като стана, побягна в Египет при египетския цар Сисак, и остана в Египет до Соломоновата смърт.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
А останалите дела на Соломона, всичко, което той извърши, и мъдростта му, не са ли записани в книгата на Соломоновите дела?
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
А времето на Соломоновото царуване в Ерусалим, над целия Израил, беше четиридесет години.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Така Соломон заспа с бащите си, и беше погребан в града на баща си Давида; а вместо него се възцари син му Ровоам.