< 1 Wafalme 10 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
A carica Savska èu glas o Solomunu i o imenu Gospodnjem, i doðe da ga iskuša zagonetkama.
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
I doðe u Jerusalim sa silnom pratnjom, s kamilama koje nošahu mirisa i zlata vrlo mnogo i dragoga kamenja; i došavši k Solomunu govori s njim o svemu što joj bješe u srcu.
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
I Solomun joj odgovori na sve rijeèi njezine; ne bješe od cara sakriveno ništa da joj ne bi odgovorio.
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
A kad carica Savska vidje svu mudrost Solomunovu i dom koji bješe sazidao,
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
I jela na stolu njegovu i stanove sluga njegovijeh i dvorbu dvorana njegovijeh i odijelo njihovo, i peharnike njegove i žrtve njegove paljenice koje prinošaše u domu Gospodnjem, ona doðe izvan sebe;
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Pa reèe caru: istina je što sam èula u svojoj zemlji o stvarima tvojim i o mudrosti tvojoj.
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
Ali ne htjeh vjerovati što se govoraše dokle ne doðem i vidim svojim oèima; a gle, ni pola mi nije kazano; tvoja mudrost i dobrota nadvišuje glas koji sam slušala.
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Blago ljudima tvojim, blago slugama tvojim, koji jednako stoje pred tobom i slušaju mudrost tvoju.
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Da je blagosloven Gospod Bog tvoj kojemu si omilio, te te posadi na prijesto Izrailjev; jer Gospod ljubi Izrailja uvijek, i postavi te carem da sudiš i dijeliš pravicu.
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Potom dade caru sto i dvadeset talanata zlata i vrlo mnogo mirisa i dragoga kamenja: nigda više ne doðe toliko takih mirisa koliko dade carica Savska caru Solomunu.
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
I laðe Hiramove, koje donošahu zlato iz Ofira, donesoše iz Ofira vrlo mnogo drveta almugima i dragoga kamenja.
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
I naèini car od toga drveta almugima zagradu u domu Gospodnjem i u domu carskom, i harfe i psaltire za pjevaèe; nigdje se više nije dovezlo takoga drveta almugima niti se vidjelo do današnjega dana.
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
A car Solomun dade carici Savskoj što god zaželje i zaiska osim onoga što joj dade sam po moguæstvu cara Solomuna. Potom ona otide i vrati se u zemlju svoju sa slugama svojim.
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
A zlata što dohoðaše Solomunu svake godine, bješe šest stotina i šezdeset i šest talanata,
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
Osim onoga što dohoðaše od trgovaca i onijeh koji prodavahu mirise i od svijeh careva Arapskih i upravitelja zemaljskih.
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
I car Solomun naèini dvjesta štitova od kovanoga zlata, šest stotina sikala zlata dajuæi na jedan štit;
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
I tri stotine malijeh štitova od kovanoga zlata, po tri mine zlata dajuæi na svaki štitiæ; i ostavi ih car u domu od šume Livanske.
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
I naèini car velik prijesto od slonove kosti, i obloži ga èistijem zlatom.
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Šest basamaka bješe u prijestola, i vrh okrugao bješe ozad na prijestolu, i ruèice bjehu s obje strane sjedišta, i dva lava stajahu pokraj tijeh ruèica.
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
I dvanaest lavova stajahu na šest basamaka otud i odovud. Ne bi taki naèinjen ni u kojem carstvu.
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
I svi sudovi iz kojih pijaše car Solomun bijahu zlatni, i svi sudovi u domu od šume Livanske bijahu od èistoga zlata; od srebra ne bješe ništa; srebro bješe ništa za vremena Solomunova.
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Jer car imaše laðe Tarsiske na moru s laðama Hiramovijem: jedanput u tri godine vraæahu se laðe Tarsiske donoseæi zlato i srebro, slonove kosti, majmune i paune.
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Tako car Solomun bijaše veæi od svijeh careva zemaljskih bogatstvom i mudrošæu.
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
I iz cijele zemlje tražahu da vide Solomuna, da èuju mudrost njegovu, koju mu dade Gospod u srce.
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
I donošahu mu svi dare, sudove srebrne i sudove zlatne, i haljine i oružje i mirise i konje i mazge, svake godine.
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Tako nakupi Solomun kola i konjika, i imaše tisuæu i èetiri stotine kola i dvanaest tisuæa konjika, koje razredi po gradovima, gdje mu bijahu kola, i kod sebe u Jerusalimu.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
I uèini car, te u Jerusalimu bijaše srebra kao kamenja, i kedrovijeh drva kao divljih smokava koje rastu po polju, tako mnogo.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
I dovoðahu Solomunu konje iz Misira i svakojaki trg, jer trgovci carevi uzimahu trg razlièan za cijenu.
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
I dolažahu kola iz Misira po šest stotina sikala srebra, a konj po sto i pedeset. I tako svi carevi Hetejski i carevi Sirski dobijahu konje preko njih.

< 1 Wafalme 10 >