< 1 Wafalme 10 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
و چون ملکه سبا آوازه سلیمان رادرباره اسم خداوند شنید، آمد تا او رابه مسائل امتحان کند.۱
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
پس با موکب بسیار عظیم و با شترانی که به عطریات و طلای بسیار وسنگهای گرانبها بار شده بود به اورشلیم واردشده، به حضور سلیمان آمد و با وی از هر‌چه دردلش بود، گفتگو کرد.۲
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
و سلیمان تمامی مسائلش را برایش بیان نمود و چیزی از پادشاه مخفی نماند که برایش بیان نکرد.۳
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
و چون ملکه سبا تمامی حکمت سلیمان را دید و خانه‌ای را که بنا کرده بود،۴
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
و طعام سفره او و مجلس بندگانش را و نظام و لباس خادمانش را و ساقیانش وزینه‌ای را که به آن به خانه خداوند برمی آمد، روح در او دیگر نماند.۵
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
و به پادشاه گفت: «آوازه‌ای که درباره کارها وحکمت تو در ولایت خود شنیدم، راست بود.۶
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
اما تا نیامدم و به چشمان خود ندیدم، اخبار راباور نکردم، و اینک نصفش به من اعلام نشده بود؛ حکمت و سعادتمندی تو از خبری که شنیده بودم، زیاده است.۷
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
خوشابه‌حال مردان تو وخوشابه‌حال این بندگانت که به حضور تو همیشه می‌ایستند و حکمت تو را می‌شنوند.۸
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
متبارک بادیهوه، خدای تو، که بر تو رغبت داشته، تو را برکرسی اسرائیل نشانید.۹
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
از این سبب که خداوند، اسرائیل را تا به ابد دوست می‌دارد، تو رابر پادشاهی نصب نموده است تا داوری و عدالت را بجا آوری.»۱۰
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
و به پادشاه صد و بیست وزنه طلا وعطریات از حد زیاده و سنگهای گرانبها داد، ومثل این عطریات که ملکه سبا به سلیمان پادشاه داد، هرگز به آن فراوانی دیگر نیامد.۱۱
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
وکشتیهای حیرام نیز که طلا از اوفیر آوردند، چوب صندل از حد زیاده، و سنگهای گرانبها ازاوفیر آوردند.۱۲
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
و پادشاه از این چوب صندل، ستونها به جهت خانه خداوند و خانه پادشاه و عودها وبربطها برای مغنیان ساخت، و مثل این چوب صندل تا امروز نیامده و دیده نشده است.۱۳
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
و سلیمان پادشاه به ملکه سبا، تمامی اراده او را که خواسته بود داد، سوای آنچه سلیمان ازکرم ملوکانه خویش به وی بخشید. پس او بابندگانش به ولایت خود توجه نموده، رفت.۱۴
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
و وزن طلایی که در یک سال نزد سلیمان رسید ششصد و شصت و شش وزنه طلا بود.۱۵
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
سوای آنچه از تاجران و تجارت بازرگانان وجمیع پادشاهان عرب و حاکمان مملکت می‌رسید.۱۶
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
و سلیمان پادشاه دویست سپرطلای چکشی ساخت که برای هر سپر ششصدمثقال طلا به‌کار برده شد، و سیصد سپر کوچک طلای چکشی ساخت که برای هر سپر سه منای طلا به‌کار برده شد، و پادشاه آنها را در خانه جنگل لبنان گذاشت.۱۷
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
و پادشاه تخت بزرگی ازعاج ساخت و آن را به زر خالص پوشانید.۱۸
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
وتخت را شش پله بود و سر تخت از عقبش مدوربود، و به این طرف و آن طرف کرسی‌اش دسته هابود و دو شیر به پهلوی دستها ایستاده بودند.۱۹
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
وآنجا دوازده شیر از این طرف و آن طرف بر آن شش پله ایستاده بودند که در هیچ مملکت مثل این ساخته نشده بود.۲۰
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
و تمامی ظروف نوشیدنی سلیمان پادشاه از طلا و تمامی ظروف خانه جنگل لبنان از زر خالص بود و هیچ‌یکی ازآنها از نقره نبود زیرا که آن در ایام سلیمان هیچ به حساب نمی آمد.۲۱
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
زیرا پادشاه کشتیهای ترشیشی با کشتیهای حیرام به روی دریا داشت. وکشتیهای ترشیشی هر سال یک مرتبه می‌آمدند وطلا و نقره و عاج و میمونها و طاووسهامی آوردند.۲۲
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
پس سلیمان پادشاه در دولت و حکمت ازجمیع پادشاهان جهان بزرگتر شد.۲۳
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
و تمامی اهل جهان، حضور سلیمان را می‌طلبیدند تاحکمتی را که خداوند در دلش نهاده بود، بشنوند.۲۴
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
و هر یکی از ایشان هدیه خود را از آلات نقره و آلات طلا و رخوت و اسلحه و عطریات واسبان و قاطرها، سال به سال می‌آوردند.۲۵
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
و سلیمان ارابه‌ها و سواران جمع کرده، هزار و چهارصد ارابه و دوازده هزار سوار داشت و آنها را در شهرهای ارابه‌ها و نزد پادشاه دراورشلیم گذاشت.۲۶
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
و پادشاه نقره را در اورشلیم مثل سنگها و چوب سرو آزاد را مثل چوب افراغ که در صحراست، فراوان ساخت.۲۷
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
و اسبهای سلیمان از مصر آورده می‌شد، و تاجران پادشاه دسته های آنها را می‌خریدند هر دسته را به قیمت معین.۲۸
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
و یک ارابه را به قیمت ششصد مثقال نقره از مصر بیرون آوردند، و می‌رسانیدند و یک اسب را به قیمت صد و پنجاه، و همچنین برای جمیع پادشاهان حتیان و پادشاهان ارام به توسطآنها بیرون می‌آوردند.۲۹

< 1 Wafalme 10 >