< 1 Wafalme 10 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
Et la reine de Sheba entendit parler de la renommée de Salomon, en relation avec le nom de l’Éternel, et elle vint pour l’éprouver par des énigmes.
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Et elle vint à Jérusalem avec un fort grand train, avec des chameaux qui portaient des aromates, et de l’or en très grande quantité, et des pierres précieuses; et elle vint vers Salomon et lui parla de tout ce qu’elle avait sur son cœur.
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
Et Salomon lui expliqua toutes les choses dont elle parlait: il n’y eut pas une chose cachée pour le roi, [pas une chose] qu’il ne lui explique.
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Et la reine de Sheba vit toute la sagesse de Salomon, et la maison qu’il avait bâtie,
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
et les mets de sa table, et la tenue de ses serviteurs, et l’ordre de service de ses officiers, et leurs vêtements, et ses échansons, et la rampe par laquelle il montait dans la maison de l’Éternel, et il n’y eut plus d’esprit en elle;
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
et elle dit au roi: Ce que j’ai entendu dire dans mon pays sur tout ton état et sur ta sagesse, était la vérité;
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
mais je n’ai pas cru ces choses, jusqu’à ce que je sois venue et que mes yeux aient vu; et voici, on ne m’avait pas rapporté la moitié; tu surpasses en sagesse et en prospérité la rumeur que j’en ai entendue.
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Heureux tes gens, heureux ceux-ci, tes serviteurs, qui se tiennent continuellement devant toi, et qui entendent ta sagesse!
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Béni soit l’Éternel, ton Dieu, qui a pris plaisir en toi pour te placer sur le trône d’Israël! Parce que l’Éternel aimait Israël à toujours, il t’a établi roi pour faire droit et justice.
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Et elle donna au roi 120 talents d’or, et des aromates en très grande quantité, et des pierres précieuses. Il n’est plus venu une abondance d’aromates pareille à ce que la reine de Sheba en donna au roi Salomon.
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
(La flotte aussi de Hiram qui amenait de l’or d’Ophir, apporta d’Ophir du bois d’almuggim en très grande quantité, et des pierres précieuses.
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
Et, avec le bois d’almuggim, le roi fit des balustrades pour la maison de l’Éternel et pour la maison du roi, et des harpes et des luths pour les chanteurs. Il n’est pas venu de semblable bois d’almuggim, et on n’en a pas vu jusqu’à ce jour.)
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Et le roi Salomon donna à la reine de Sheba tout son désir, [tout ce] qu’elle demanda, outre ce qu’il lui donna selon le pouvoir du roi Salomon. Et elle s’en retourna, et s’en alla dans son pays, elle et ses serviteurs.
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Et le poids de l’or qui arrivait à Salomon dans une année était de 666 talents d’or,
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
outre [ce qui lui venait] des commerçants ambulants et du trafic des marchands, et de tous les rois de l’Arabie, et des gouverneurs du pays.
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Et le roi Salomon fit 200 grands boucliers d’or battu, mettant à chaque bouclier 600 [sicles] d’or,
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
et 300 petits boucliers d’or battu, mettant à chaque bouclier trois mines d’or; et le roi les mit dans la maison de la forêt du Liban.
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Et le roi fit un grand trône d’ivoire, et le recouvrit d’or affiné:
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
le trône avait six degrés, et le haut du trône par-derrière était arrondi; et il y avait des bras d’un côté et de l’autre à l’endroit du siège, et deux lions qui se tenaient à côté des bras,
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
et douze lions qui se tenaient là sur les six degrés, d’un côté et de l’autre: il ne s’en était point fait de pareil dans aucun royaume.
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
Et tous les vases à boire du roi Salomon étaient d’or, et tous les vases de la maison de la forêt du Liban, d’or pur: aucun n’était d’argent, il n’était compté pour rien aux jours de Salomon.
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Car la flotte de Tarsis qu’avait le roi, tenait la mer avec la flotte de Hiram; une fois tous les trois ans la flotte de Tarsis venait, apportant de l’or et de l’argent, de l’ivoire, et des singes et des paons.
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Et le roi Salomon fut plus grand que tous les rois de la terre, en richesse et en sagesse.
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Et toute la terre recherchait la face de Salomon, pour entendre sa sagesse, que Dieu avait mise dans son cœur.
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
Et ils apportaient chacun son présent: des vases d’argent et des vases d’or, et des vêtements, et des armes, et des aromates, des chevaux et des mulets: chaque année le tribut de l’année.
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Et Salomon rassembla des chars et des cavaliers; et il eut 1 400 chars, et 12 000 cavaliers; et il les plaça dans les villes à chars et auprès du roi à Jérusalem.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Et le roi fit que l’argent, dans Jérusalem, était comme les pierres, et il fit que les cèdres étaient, en quantité, comme les sycomores qui sont dans le pays plat.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
Et quant aux chevaux de Salomon, il les tirait d’Égypte: une caravane de marchands du roi prenait un convoi [de chevaux] pour un certain prix;
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
et un char montait et sortait d’Égypte pour 600 [sicles] d’argent, et un cheval pour 150; et on en faisait venir ainsi, par leur main, pour tous les rois des Héthiens et pour les rois de Syrie.

< 1 Wafalme 10 >