< 1 Wafalme 10 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
Lorsque la reine de Saba apprit la renommée de Salomon concernant le nom de Yahvé, elle vint pour l'éprouver par des questions difficiles.
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Elle vint à Jérusalem avec une très grande caravane, avec des chameaux qui portaient des épices, beaucoup d'or et des pierres précieuses; et quand elle fut arrivée auprès de Salomon, elle lui parla de tout ce qu'elle avait dans le cœur.
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
Salomon répondit à toutes ses questions. Il n'y avait rien de caché au roi qu'il ne lui ait dit.
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Lorsque la reine de Saba eut vu toute la sagesse de Salomon, la maison qu'il avait bâtie,
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
les mets de sa table, les sièges de ses serviteurs, la présence de ses fonctionnaires, leurs vêtements, ses échansons, et l'escalier par lequel il montait à la maison de Yahvé, il n'y eut plus d'esprit en elle.
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Elle dit au roi: « C'est un récit véridique que j'ai entendu dans mon pays sur tes actes et ta sagesse.
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
Mais je n'ai pas cru à ces paroles jusqu'à ce que je sois venue et que mes yeux l'aient vu. Voici qu'on ne m'a pas dit la moitié de ce qu'on m'a dit! Ta sagesse et ta prospérité dépassent la renommée que j'ai entendue.
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Heureux sont tes hommes, heureux sont tes serviteurs qui se tiennent continuellement devant toi, qui écoutent ta sagesse.
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Béni soit Yahvé, ton Dieu, qui a pris plaisir à te placer sur le trône d'Israël. Parce que l'Éternel a aimé Israël pour toujours, il t'a établi roi, pour que tu fasses droit et justice. »
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Elle donna au roi cent vingt talents d'or, une très grande quantité d'aromates et de pierres précieuses. Jamais encore il n'y eut une telle abondance d'aromates que ceux que la reine de Saba donna au roi Salomon.
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
La flotte de Hiram qui apportait de l'or d'Ophir ramenait aussi d'Ophir de grandes quantités d'almugs et de pierres précieuses.
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
Le roi fit des almugs des colonnes pour la maison de l'Éternel et pour la maison du roi, des harpes et des instruments à cordes pour les chanteurs; aucun almug n'est venu et n'a été vu jusqu'à ce jour.
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Le roi Salomon donna à la reine de Saba tout ce qu'elle désirait, tout ce qu'elle demandait, en plus de ce que Salomon lui avait donné de sa générosité royale. Elle se retourna et s'en alla dans son pays, elle et ses serviteurs.
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Le poids de l'or qui arriva à Salomon en un an fut de six cent soixante-six talents d'or,
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
sans compter ce qu'apportèrent les marchands, le trafic des marchands, de tous les rois des peuples mélangés et des gouverneurs du pays.
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Le roi Salomon fit deux cents boucliers d'or battu; six cents sicles d'or entraient dans un bouclier.
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
Il fit trois cents boucliers d'or battu; on mettait trois mina d'or par bouclier; et le roi les plaça dans la maison de la forêt du Liban.
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Le roi fit un grand trône d'ivoire, et il le couvrit d'or fin.
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Il y avait six marches pour accéder au trône, et le sommet du trône était rond derrière; il y avait des accoudoirs de chaque côté de la place du siège, et deux lions se tenaient à côté des accoudoirs.
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
Douze lions se tenaient là, d'un côté et de l'autre, sur les six marches. Rien de semblable n'a été fait dans aucun royaume.
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
Tous les vases à boire du roi Salomon étaient en or, et tous les vases de la maison de la forêt du Liban étaient en or pur. Aucun n'était en argent, car il était considéré comme de peu de valeur à l'époque de Salomon.
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Car le roi avait une flotte de navires de Tarsis en mer avec la flotte d'Hiram. Une fois tous les trois ans, la flotte de Tarsis venait apporter de l'or, de l'argent, de l'ivoire, des singes et des paons.
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Le roi Salomon surpassa ainsi tous les rois de la terre en richesse et en sagesse.
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Toute la terre recherchait la présence de Salomon pour entendre la sagesse que Dieu avait mise dans son cœur.
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
Année après année, chacun apportait son tribut, des objets d'argent, des objets d'or, des vêtements, des armures, des épices, des chevaux et des mules.
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Salomon rassembla des chars et des cavaliers. Il avait mille quatre cents chars et douze mille cavaliers. Il les garda dans les villes de chars et auprès du roi à Jérusalem.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Le roi rendit l'argent aussi commun que les pierres à Jérusalem, et les cèdres aussi communs que les sycomores qui sont dans la plaine.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
Les chevaux que possédait Salomon furent amenés d'Égypte. Les marchands du roi les reçurent en troupeaux, chacun conduisant à un prix.
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
On importait d'Égypte un char pour six cents sicles d'argent et un cheval pour cent cinquante sicles, et on les exportait ainsi à tous les rois des Hittites et aux rois de Syrie.

< 1 Wafalme 10 >