< 1 Wafalme 10 >
1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
And the queen of Sheba is hearing of the fame of Solomon concerning the name of Jehovah, and cometh to try him with enigmas,
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
and she cometh to Jerusalem, with a very great company, camels bearing spices, and very much gold, and precious stone, and she cometh unto Solomon, and speaketh unto him all that hath been with her heart.
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
And Solomon declareth to her all her matters — there hath not been a thing hid from the king that he hath not declared to her.
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
And the queen of Sheba seeth all the wisdom of Solomon, and the house that he built,
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
and the food of his table, and the sitting of his servants, and the standing of his ministers, and their clothing, and his butlers, and his burnt-offering that he causeth to ascend in the house of Jehovah, and there hath not been in her any more spirit.
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
And she saith unto the king, 'True hath been the word that I heard in my land, concerning thy matters and thy wisdom;
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
and I gave no credence to the words till that I have come, and my eyes see, and lo, it was not declared to me — the half; thou hast added wisdom and goodness unto the report that I heard.
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
O the happiness of thy men, O the happiness of thy servants — these — who are standing before thee continually, who are hearing thy wisdom!
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Jehovah thy God is blessed who delighted in thee, to put thee on the throne of Israel; in Jehovah's loving Israel to the age He doth set thee for king, to do judgment and righteousness.
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
And she giveth to the king a hundred and twenty talents of gold, and spices very many, and precious stone; there came not like that spice any more for abundance that the queen of Sheba gave to king Solomon.
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
And also, the navy of Hiram that bore gold from Ophir, brought in from Ophir almug-trees very many, and precious stone;
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
and the king maketh the almug-trees a support for the house of Jehovah, and for the house of the king, and harps and psalteries for singers; there have not come such almug-trees, nor have there been seen [such] unto this day.
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And king Solomon gave to the queen of Sheba all her desire that she asked, apart from that which he gave to her as a memorial of king Solomon, and she turneth and goeth to her land, she and her servants.
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
And the weight of the gold that hath come to Solomon in one year is six hundred sixty and six talents of gold,
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
apart from [that of] the tourists, and of the traffic of the merchants, and of all the kings of Arabia, and of the governors of the land.
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
And king Solomon maketh two hundred targets of alloyed gold — six hundred of gold go up on the one target;
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
and three hundred shields of alloyed gold — three pounds of gold go up on the one shield; and the king putteth them [in] the house of the forest of Lebanon.
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
And the king maketh a great throne of ivory, and overlayeth it with refined gold;
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
six steps hath the throne, and a round top [is] to the throne behind it, and hands [are] on this [side] and on that, unto the place of the sitting, and two lions are standing near the hands,
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
and twelve lions are standing there on the six steps, on this [side] and on that; it hath not been made so for any kingdom.
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
And all the drinking vessels of king Solomon [are] of gold, and all the vessels of the house of the forest of Lebanon [are] of refined gold — there are none of silver; it was not reckoned in the days of Solomon for anything,
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
for a navy of Tarshish hath the king at sea with a navy of Hiram; once in three years cometh the navy of Tarshish, bearing gold, and silver, ivory, and apes, and peacocks.
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
And king Solomon is greater than any of the kings of the earth for riches and for wisdom,
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
and all the earth is seeking the presence of Solomon, to hear his wisdom that God hath put into his heart,
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
and they are bringing each his present, vessels of silver, and vessels of gold, and garments, and armour, and spices, horses, and mules, the matter of a year in a year.
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
And Solomon gathereth chariots, and horsemen, and he hath a thousand and four hundred chariots, and twelve thousand horsemen, and he placeth them in the cities of the chariot, and with the king in Jerusalem.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the king maketh the silver in Jerusalem as stones, and the cedars he hath made as the sycamores that [are] in the low country, for abundance.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
And the outgoing of the horses that king Solomon hath [is] from Egypt, and from Keveh; merchants of the king take from Keveh at a price;
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
and a chariot cometh up and cometh out of Egypt for six hundred silverlings, and a horse for fifty and a hundred, and so for all the kings of the Hittites, and for the kings of Aram; by their hand they bring out.