< 1 Wafalme 10 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
И Савската царица, като чу, че Соломон се прочува като служител на Господното име, дойде да го опита с мъчни за нея въпроси.
2 Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Дойде в Ерусалим с една твърде голяма свита, с камили натоварени с аромати, и с твърде много злато и скъпоценни камъни; и като дойде при Соломона, говори с него за всичко що имаше на сърцето си.
3 Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
И Соломон отговори на всичките й въпроси; нямаше нищо скрито за царя, което на можа да й обясни.
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
А като видя Савската царица всичката мъдрост на Соломона, и къщата който бе построил,
5 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
ястията на трапезата му, седенето на слугите му, и прислужването на служителите му, и облеклото им, и виночерпците му, и нагорнището, с което отиваше в Господния дом, не остана дух в нея.
6 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
И рече на царя: Верен беше слухът, който чух в земята си, за твоето състояние и за мъдростта ти.
7 Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
Аз не вярвах думите, докато не дойдох и не видях с очите си; но, ето, нито половината не ми е била казана; мъдростта ти о благоденствието ти надминават слуха, който бях чула.
8 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Честити мажете ти, честити тия твои слуги, които стоят всякога пред тебе та слушат мъдростта ти.
9 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Да бъде благословен Господ твоят Бог, Който има благоволение към тебе да те постави на Израилевия престол. Понеже Господ е възлюбил Израиля за винаги, затова те е поставил цар, за да раздаваш правосъдие и да вършиш правда.
10 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
И тя даде на царя сто и двадесет таланта злато, и твърде много аромати и скъпоценни камъни; не дойде вече такова изобилие от аромати, каквото ония, които Савската царица даде на Соломона.
11 (Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Още и Хирамовите кораби, които донасяха злато от Офир, донасяха от Офир и голямо изобилие алмугови дървета и скъпоценни камъни.
12 Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
А от алмуговите дървета царят направи преградки в Господния дом и в царската къща, тоже и арфи и псалтири за певците; такива алмугови дървета не са дохождали нито са били виждали до днес.
13 Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
И цар Соломон даде на Савската царица всичко що тя желаеше, каквото поиска, освен онова, което цар Соломон й даде доброволно. И тъй тя се върна със слугите си та си отиде в своята си земя.
14 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
А теглото на златото, което дохождаше на Соломона всяка година, беше шестстотин и шестдесет и шест златни таланта,
15 mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
освен онова, което се внасяше от купувачите, от товарите на търговците, от всичките арабски царе и от управителите на страната.
16 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
И цар Соломон направи двеста щита от ковано злато; шестстотин сикли злато се иждиви за всеки щит:
17 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
и триста щитчета от ковано злато; три фунта злато се иждиви за всяко щитче; и царят ги положи в къщата Ливански лес.
18 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Царят направи и един великолепен престол от слонова кост, който позлати с най-чисто злато.
19 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Престолът имаше шест стъпала, и върхът на престола беше кръгъл отзаде; и имаше облегалки от двете страни на седалището, и два лъва стояха край облегалките.
20 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
А там, върху шестте стъпала, от двете страни, стояха дванадесет лъва; подобно нещо не се е направило в никое царство.
21 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
И всичките цар Соломонови съдове за пиене бяха златни, и всичките съдове в къщата Ливански лес от чисто злато; ни един не бе от сребро; среброто се считаше за нищо в Соломоновото време.
22 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Защото царят имаше на морето кораби, като тарсийските, заедно с корабите на Хирама; еднъж в три години тия тарсийски кораби дохождаха и донасяха злато и сребро, слонова кост, маймуни и пауни.
23 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Така цар Соломон надмина всичките царе на света по богатство и мъдрост.
24 Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
И целият свят търсеше Соломоновото присъствие, за да чуят мъдростта, която Бог бе турил в сърцето му.
25 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
И всяка година донасяха всеки от тях подаръка си, сребърни вещи, златни вещи, облекла, оръжия и аромати, коне и мъски.
26 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Тоже Соломон събра колесници и конници; имаше хиляда и четиристотин колесници, и дванадесет хиляди конници, които настани в градовете за колесниците и при царя в Ерусалим.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
И царят направи среброто да изобилва в Ерусалим, като камъни, а кедрите направи, като полските черници.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
И конете, които имаше Соломон, се докарваха из Египет; и царските търговци ги купуваха по стада с определена цена.
29 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
А всяка колесница излизаше из Египет и възхождаше в Ерусалим за шестстотин сребърни сикли и всеки кон за сто и петдесет; така също за всичките хетейски царе, и за сирийските царе, те се доставяха чрез тия търговци.

< 1 Wafalme 10 >