< 1 Wafalme 1 >

1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo.
Or le roi David était vieux et avancé en âge; on le couvrait de vêtements, mais il n'avait pas chaud.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.”
Ses serviteurs lui dirent alors: « Qu'on cherche une jeune vierge pour mon seigneur le roi. Qu'elle se tienne devant le roi et qu'elle le chérisse; qu'elle soit couchée dans ton sein, afin que mon seigneur le roi ait chaud. »
3 Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri wa sura na wakampata Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
Ils cherchèrent donc une belle jeune fille dans tout le territoire d'Israël, trouvèrent Abischag, la Sunamite, et l'amenèrent au roi.
4 Msichana huyo alikuwa mzuri sana wa sura, akamtunza mfalme na kumhudumia, lakini mfalme hakufanya naye tendo la ndoa.
La jeune femme était très belle, elle chérissait le roi et le servait, mais le roi ne la connaissait pas intimement.
5 Basi Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi, akajigamba na kusema, “Mimi nitakuwa mfalme.” Hivyo akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, pamoja na watu hamsini wa kumtangulia wakikimbia.
Alors Adonija, fils de Haggith, s'éleva et dit: « Je veux être roi. » Alors il lui prépara des chars et des cavaliers, et cinquante hommes pour courir devant lui.
6 (Baba yake hakuwa ameingilia na kumuuliza, “Kwa nini unafanya hivyo?” Alikuwa pia kijana mzuri sana wa sura, na alizaliwa baada ya Absalomu.)
Son père ne l'avait jamais mécontenté en disant: « Pourquoi as-tu agi ainsi? » Il était aussi très beau, et il était né après Absalom.
7 Adoniya akashauriana pamoja na Yoabu mwana wa Seruya na kuhani Abiathari, nao wakamsaidia.
Il s'entretint avec Joab, fils de Tseruja, et avec le prêtre Abiathar; ils suivirent Adonija et le secoururent.
8 Lakini kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, Nathani nabii, Shimei, Rei na walinzi maalum wa Daudi hawakujiunga na Adoniya.
Mais le sacrificateur Tsadok, Benaja, fils de Jehojada, Nathan, le prophète, Shimei, Rei, et les hommes forts qui appartenaient à David, n'étaient pas avec Adonija.
9 Ndipo Adoniya akatoa dhabihu ya kondoo, ngʼombe na ndama walionona kwenye Jiwe la Zohelethi karibu na En-Rogeli. Akawaalika ndugu zake wote, wana wa mfalme na wanaume wote wa Yuda waliokuwa maafisa wa mfalme,
Adonija tua des brebis, des bœufs et des veaux près de la pierre de Zoheleth, qui est près d'En Rogel; il appela tous ses frères, les fils du roi, et tous les hommes de Juda, les serviteurs du roi;
10 lakini hakumwalika nabii Nathani, Benaya, walinzi maalum wa mfalme, wala ndugu yake Solomoni.
mais il n'appela pas Nathan, le prophète, ni Benaja, ni les hommes forts, ni Salomon, son frère.
11 Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, “Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili?
Nathan s'adressa à Bethsabée, mère de Salomon, et dit: « N'as-tu pas entendu dire qu'Adonija, fils de Haggith, règne, et que David, notre seigneur, ne le sait pas?
12 Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni.
Viens donc maintenant, que je te donne un conseil, afin que tu sauves ta vie et celle de ton fils Salomon.
13 Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, ‘Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: “Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?’
Va trouver le roi David et dis-lui: « N'as-tu pas juré à ton serviteur, mon seigneur le roi, en disant: « Salomon, ton fils, régnera après moi, et il s'assiéra sur mon trône? ». Pourquoi donc Adonias règne-t-il? »
14 Utakapokuwa ukizungumza na mfalme, nitaingia na kuthibitisha hayo uliyoyasema.”
Voici que, pendant que tu discutes encore là avec le roi, je vais aussi entrer après toi et confirmer tes paroles. »
15 Hivyo Bathsheba akaenda kumwona mfalme chumbani mwake mahali ambapo Abishagi, Mshunami, alikuwa akimhudumia, naye mfalme alikuwa mzee sana.
Bethsabée entra chez le roi dans sa chambre. Le roi était très âgé, et Abishag, la Sunamite, était au service du roi.
16 Bathsheba akasujudu na kupiga magoti mbele ya mfalme. Mfalme akauliza, “Ni nini hiki unachotaka?”
Bethsabée s'inclina et montra du respect au roi. Le roi dit: « Que désirez-vous? »
17 Akamwambia, “Bwana wangu, wewe mwenyewe uliniapia mimi mtumishi wako kwa Bwana Mungu wako kwamba: ‘Solomoni Mwanao atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha ufalme.’
Elle lui dit: « Mon seigneur, tu as juré par Yahvé ton Dieu à ton serviteur: « Salomon, ton fils, régnera après moi, et il s'assiéra sur mon trône ».
18 Lakini sasa Adoniya amekuwa mfalme, nawe, bwana wangu mfalme huna habari kuhusu jambo hilo.
Or, voici qu'Adonija règne, et toi, mon seigneur le roi, tu ne le sais pas.
19 Ametoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo, naye amewaalika wana wa mfalme wote, kuhani Abiathari, na Yoabu jemadari wa jeshi, lakini hakumwalika Solomoni mtumishi wako.
Il a tué du bétail, des animaux gras et des moutons en abondance, et il a appelé tous les fils du roi, le prêtre Abiathar et Joab, le chef de l'armée; mais il n'a pas appelé Salomon, ton serviteur.
20 Bwana wangu mfalme, macho ya Israeli yote yanakutazama wewe wajue kutoka kwako kuwa ni nani atakayeketi katika kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.
Toi, mon seigneur le roi, les yeux de tout Israël sont sur toi, pour que tu leur dises qui sera assis sur le trône de mon seigneur le roi après lui.
21 Kama sivyo, mara tu bwana wangu mfalme atakapopumzishwa pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Solomoni tutatendewa kama wahalifu.”
Sinon, il arrivera, lorsque mon seigneur le roi se couchera avec ses pères, que moi et mon fils Salomon serons considérés comme des criminels. »
22 Alipokuwa angali anazungumza na mfalme, nabii Nathani akafika.
Et voici, pendant qu'elle parlait encore avec le roi, Nathan, le prophète, entra.
23 Wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa.” Kisha akaenda mbele ya mfalme na kumsujudia hadi uso wake ukagusa ardhi.
On en informa le roi, en disant: « Voici Nathan, le prophète! » Lorsqu'il fut entré devant le roi, il se prosterna devant le roi, le visage contre terre.
24 Nathani akasema, “Je, bwana wangu mfalme, umetangaza kuwa Adoniya atakuwa mfalme baada yako na kwamba ataketi kwenye kiti chako cha ufalme?
Nathan dit: « Mon seigneur, le roi, as-tu dit: Adonija régnera après moi, et il s'assiéra sur mon trône?
25 Leo ameshuka na kutoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo. Amewaalika wana wote wa mfalme, jemadari wa jeshi na kuhani Abiathari. Sasa hivi, wanakula na kunywa pamoja naye wakisema, ‘Aishi maisha marefu, Mfalme Adoniya!’
Car il est descendu aujourd'hui, il a tué en abondance du bétail, des animaux gras et des brebis, et il a appelé tous les fils du roi, les chefs de l'armée et le prêtre Abiathar. Voici qu'ils mangent et boivent devant lui, et qu'ils disent: « Vive le roi Adonija! »
26 Lakini mimi mtumishi wako, kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada na mtumishi wako Solomoni hakutualika.
Mais il ne m'a pas appelé, moi, ton serviteur, le sacrificateur Tsadok, Benaja, fils de Jehojada, et ton serviteur Salomon.
27 Je, hili ni jambo ambalo bwana wangu mfalme amelifanya pasipo kuwajulisha watumishi wake ili wapate kujua ni nani atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake?”
Est-ce que cette chose a été faite par mon seigneur le roi, et tu n'as pas montré à tes serviteurs qui devait s'asseoir sur le trône de mon seigneur le roi après lui? ».
28 Ndipo Mfalme Daudi akasema, “Mwite Bathsheba, aingie ndani.” Hivyo akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele yake.
Le roi David prit alors la parole: « Fais venir Bathsheba auprès de moi. » Elle vint en présence du roi et se présenta devant le roi.
29 Ndipo mfalme akaapa: “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka kila taabu,
Le roi fit un vœu et dit: « L'Éternel est vivant, qui a racheté mon âme de toute adversité,
30 hakika nitatekeleza leo kile nilichokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli: Mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha ufalme baada yangu.”
et comme je te l'ai juré par l'Éternel, le Dieu d'Israël, en disant: « Ton fils Salomon régnera après moi, et il s'assiéra sur mon trône à ma place, je le ferai aujourd'hui. »
31 Kisha Bathsheba akasujudu akipiga magoti mbele ya mfalme uso wake ukigusa ardhi akasema, “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi milele!”
Alors Bethsabée se prosterna le visage contre terre et montra du respect au roi, et dit: « Que mon seigneur le roi David vive à jamais! ».
32 Mfalme Daudi akasema, “Mwite kuhani Sadoki ndani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Walipofika mbele ya mfalme,
Le roi David dit: « Appelez-moi le prêtre Tsadok, le prophète Nathan, et Benaja, fils de Jehoiada. » Ils se présentèrent devant le roi.
33 akawaambia: “Wachukueni watumishi wa bwana wenu pamoja nanyi na mkamkalishe mwanangu Solomoni juu ya nyumbu wangu mwenyewe mkamteremshe hadi Gihoni.
Le roi leur dit: « Prenez avec vous les serviteurs de votre seigneur, faites monter Salomon, mon fils, sur ma propre mule, et faites-le descendre au Guihon.
34 Huko kuhani Sadoki na nabii Nathani wamtie mafuta awe mfalme juu ya Israeli. Pigeni tarumbeta na mpaze sauti, ‘Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!’
Que le prêtre Tsadok et le prophète Nathan l'y oignent comme roi d'Israël. On sonnera de la trompette et on dira: « Vive le roi Salomon ».
35 Kisha mtapanda pamoja naye, atakuja na kuketi kwenye kiti changu cha ufalme na kutawala badala yangu. Nimemweka awe mtawala juu ya Israeli na Yuda.”
Puis montez après lui, et il viendra s'asseoir sur mon trône, car il sera roi à ma place. Je l'ai établi comme prince sur Israël et sur Juda. »
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, “Amen! Bwana, Mungu wa bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
Benaja, fils de Jehoïada, répondit au roi et dit: « Amen. Que Yahvé, le Dieu de mon seigneur le roi, le dise.
37 Kama vile Bwana alivyokuwa na bwana wangu mfalme, vivyo hivyo na awe na Solomoni kukifanya kiti chake cha utawala kuwa kikuu kuliko kile cha bwana wangu Mfalme Daudi!”
Comme Yahvé a été avec le roi mon seigneur, qu'il le soit aussi avec Salomon, et qu'il rende son trône plus grand que le trône du roi David mon seigneur. »
38 Hivyo kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi wakampandisha Solomoni juu ya nyumbu wa Mfalme Daudi, nao wakamsindikiza hadi Gihoni.
Le prêtre Tsadok, Nathan le prophète, Benaja, fils de Jehojada, les Kéréthiens et les Péléthiens descendirent, firent monter Salomon sur la mule du roi David, et l'amenèrent à Guihon.
39 Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta kutoka kwenye hema takatifu na kumtia Solomoni mafuta. Kisha wakapiga tarumbeta na watu wote wakapaza sauti wakisema, “Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!”
Le prêtre Tsadok prit la corne d'huile dans la Tente et oignit Salomon. On sonna de la trompette, et tout le peuple dit: « Vive le roi Salomon! »
40 Na watu wote wakakwea wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hata ardhi ikatikisika kwa ile sauti.
Tout le peuple monta après lui, et le peuple joua de la flûte et se réjouit d'une grande joie, si bien que la terre trembla à leur bruit.
41 Adoniya pamoja na wageni wote waliokuwa pamoja naye wakasikia sauti hiyo walipokuwa wakimalizia karamu yao. Waliposikia sauti ya tarumbeta, Yoabu akauliza, “Nini maana ya makelele yote haya katika mji?”
Adonija et tous les convives qui étaient avec lui l'entendirent comme ils avaient fini de manger. Lorsque Joab entendit le son de la trompette, il dit: « Pourquoi ce bruit de la ville en émoi? »
42 Hata alipokuwa anasema, Yonathani mwana wa kuhani Abiathari akafika. Adoniya akasema, “Ingia ndani. Mtu mstahiki kama wewe ni lazima alete habari njema.”
Comme il parlait encore, voici qu'arrive Jonathan, fils du sacrificateur Abiathar, et Adonija dit: « Entre, car tu es un homme digne, et tu apportes de bonnes nouvelles. »
43 Yonathani akajibu, “La hasha! Mfalme Daudi bwana wetu amemfanya Solomoni kuwa mfalme.
Jonathan répondit à Adonija: Certainement, notre seigneur le roi David a fait roi Salomon.
44 Mfalme amemtuma pamoja naye kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi, nao wamempandisha juu ya nyumbu wa mfalme,
Le roi a envoyé avec lui le prêtre Tsadok, Nathan le prophète, Benaja, fils de Jehojada, les Kéréthiens et les Péléthiens, et ils l'ont fait monter sur la mule du roi.
45 nao kuhani Sadoki na nabii Nathani wamemtia mafuta kuwa mfalme huko Gihoni. Kuanzia hapo wameendelea kushangilia na sauti zimeenea pote mjini. Hizo ndizo kelele unazosikia.
Le prêtre Tsadok et Nathan le prophète l'ont oint comme roi à Gihon. Ils sont remontés de là en se réjouissant, si bien que la ville a retenti de nouveau. C'est ce bruit que vous avez entendu.
46 Zaidi ya hayo, Solomoni ameketi juu ya kiti chake cha ufalme.
Et Salomon s'est assis sur le trône du royaume.
47 Pia, maafisa wa mfalme wamekuja ili kumtakia heri bwana wetu Mfalme Daudi wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Solomoni kuwa mashuhuri kuliko lako na kiti chake cha ufalme kiwe na ukuu kuliko chako!’ Naye mfalme akasujudu akiabudu kitandani mwake
Les serviteurs du roi sont venus bénir le roi David, notre seigneur, en disant: « Que ton Dieu rende le nom de Salomon meilleur que ton nom, et son trône plus grand que ton trône ».
48 na kusema, ‘Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye ameruhusu macho yangu kuona mrithi juu ya kiti changu cha ufalme leo hii.’”
Et le roi dit: « Béni soit Yahvé, le Dieu d'Israël, qui a donné aujourd'hui à quelqu'un de s'asseoir sur mon trône, sans que mes yeux le voient. »
49 Katika hili, wageni wote wa Adoniya wakainuka kwa mshtuko wa hofu na kutawanyika.
Tous les hôtes d'Adonija eurent peur; ils se levèrent, et chacun s'en alla de son côté.
50 Lakini Adoniya kwa kumwogopa Solomoni, akaenda na kushika pembe za madhabahu.
Adonija eut peur à cause de Salomon; il se leva, partit, et s'accrocha aux cornes de l'autel.
51 Kisha Solomoni akaambiwa, “Adoniya anamwogopa Mfalme Solomoni na ameshikilia pembe za madhabahu. Anasema, ‘Mfalme Solomoni na aniapie leo kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’”
On dit à Salomon: « Voici qu'Adonija craint le roi Salomon; car voici qu'il s'accroche aux cornes de l'autel, en disant: « Que le roi Salomon me jure d'abord qu'il ne fera pas mourir son serviteur par l'épée. »
52 Solomoni akajibu, “Kama akijionyesha kuwa mtu mstahiki, hakuna unywele wake utakaoanguka juu ya ardhi, lakini kama uovu ukionekana ndani yake, atakufa.”
Salomon a dit: « S'il se montre un homme digne, pas un de ses cheveux ne tombera sur la terre; mais si la méchanceté se trouve en lui, il mourra. »
53 Ndipo Mfalme Solomoni akawatuma watu, nao wakamshusha kutoka madhabahuni. Naye Adoniya akaja akamwinamia Mfalme Solomoni, naye Solomoni akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
Le roi Salomon l'envoya, et on le fit descendre de l'autel. Il vint se prosterner devant le roi Salomon, et Salomon lui dit: « Va dans ta maison. »

< 1 Wafalme 1 >