< 1 Wafalme 1 >

1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo.
And kyng Dauid wax eld, and hadde ful many daies of age; and whanne he was hilid with clothis, he was not maad hoot.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.”
Therfor hise seruauntis seiden to hym, Seke we to oure lord the kyng a yong wexynge virgyn; and stonde sche bifor the kyng, and nursche sche hym, and slepe in his bosum, and make hoot oure lord the kyng.
3 Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri wa sura na wakampata Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
Therfor thei souyten a yong wexyng virgyn, fair in alle the coostis of Israel; and thei founden Abisag of Sunam, and thei brouyten hir to the kyng.
4 Msichana huyo alikuwa mzuri sana wa sura, akamtunza mfalme na kumhudumia, lakini mfalme hakufanya naye tendo la ndoa.
Forsothe the damysel was ful fair, and sche slepte with the kyng, and mynystride to hym; forsothe the king knew not hir fleischli.
5 Basi Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi, akajigamba na kusema, “Mimi nitakuwa mfalme.” Hivyo akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, pamoja na watu hamsini wa kumtangulia wakikimbia.
Sotheli Adonye, sone of Agith, was reisid, and seide, Y schal regne. And he made to hym a chare, and knyytis, and fifti men, that runnen bifor hym.
6 (Baba yake hakuwa ameingilia na kumuuliza, “Kwa nini unafanya hivyo?” Alikuwa pia kijana mzuri sana wa sura, na alizaliwa baada ya Absalomu.)
Nether his fadir repreuyde hym ony tyme, and seide, Whi `didist thou this? Forsothe also he was ful fair, the secounde child aftir Absolon; and his word was with Joab,
7 Adoniya akashauriana pamoja na Yoabu mwana wa Seruya na kuhani Abiathari, nao wakamsaidia.
sone of Saruye, and with `Abiathar, preest, that helpiden the partis of Adonye.
8 Lakini kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, Nathani nabii, Shimei, Rei na walinzi maalum wa Daudi hawakujiunga na Adoniya.
Sotheli Sadoch, the preest, and Banaie, sone of Joiada, and Nathan, the prophete, and Semey, and Cerethi, and Ferethi, and al the strengthe of the oost of Dauid, weren not with Adonye.
9 Ndipo Adoniya akatoa dhabihu ya kondoo, ngʼombe na ndama walionona kwenye Jiwe la Zohelethi karibu na En-Rogeli. Akawaalika ndugu zake wote, wana wa mfalme na wanaume wote wa Yuda waliokuwa maafisa wa mfalme,
Therfor whanne rammes weren offrid, and caluys, and alle fatte thingis, bisidis the stoon Zoelech, that was nyy the welle of Rogel, Adonye clepide alle hise britheren, sones of the kyng, and alle the men of Juda, seruauntis of the kyng.
10 lakini hakumwalika nabii Nathani, Benaya, walinzi maalum wa mfalme, wala ndugu yake Solomoni.
Sotheli `he clepide not Nathan, the profete, and Banaie, and alle stronge men, and Salomon, his brothir.
11 Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, “Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili?
Therfor Nathan seide to Bersabee, modir of Salomon, Whether thou herdist, that Adonye, sone of Agith, regnede, and oure lord Dauid knoweth not this?
12 Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni.
Now therfor come thou, take thou counsel of me, and saue thi lijf, and of Salomon thi sone.
13 Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, ‘Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: “Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?’
Go thou, and entre to kyng Dauid, and seie thou to hym, Whether not thou, my lord the kyng, hast swore to me, thin handmaide, and seidist, that Salomon thi sone schal regne aftir me, and he schal sitte in my trone?
14 Utakapokuwa ukizungumza na mfalme, nitaingia na kuthibitisha hayo uliyoyasema.”
Whi therfor regneth Adonye? And yit while thou schalt speke there with the kyng, Y schal come aftir thee, and `Y schal fille thi wordis.
15 Hivyo Bathsheba akaenda kumwona mfalme chumbani mwake mahali ambapo Abishagi, Mshunami, alikuwa akimhudumia, naye mfalme alikuwa mzee sana.
Therfor Bersabee entride to the kyng in the closet; forsothe the kyng was ful eeld, and Abisag of Sunam `mynystride to hym.
16 Bathsheba akasujudu na kupiga magoti mbele ya mfalme. Mfalme akauliza, “Ni nini hiki unachotaka?”
Bersabee bowide hir silf, and worschipide the kyng; to whom the kyng seide, What wolt thou to thee?
17 Akamwambia, “Bwana wangu, wewe mwenyewe uliniapia mimi mtumishi wako kwa Bwana Mungu wako kwamba: ‘Solomoni Mwanao atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha ufalme.’
And sche answeride, and seide, My lord the kyng, thou hast swore to thin handmaide bi thi Lord God, Salomon thy sone schal regne aftir me, and he schal sitte in my trone;
18 Lakini sasa Adoniya amekuwa mfalme, nawe, bwana wangu mfalme huna habari kuhusu jambo hilo.
and lo! Adonye hath regnede now, `while thou, my lord the kyng, knowist not;
19 Ametoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo, naye amewaalika wana wa mfalme wote, kuhani Abiathari, na Yoabu jemadari wa jeshi, lakini hakumwalika Solomoni mtumishi wako.
he hath slayn oxis, and alle fatte thingis, and ful many rammes; and he clepide alle the sones of the king, also `Abiathar preest, and Joab, the prince of chyualri; but he clepide not Salomon, thi seruaunt.
20 Bwana wangu mfalme, macho ya Israeli yote yanakutazama wewe wajue kutoka kwako kuwa ni nani atakayeketi katika kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.
Netheles, my lord the kyng, the iyen of al Israel biholden in to thee, that thou schewe to hem, who owith to sitte in thi trone, my lord the kyng, aftir thee;
21 Kama sivyo, mara tu bwana wangu mfalme atakapopumzishwa pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Solomoni tutatendewa kama wahalifu.”
and it schal be, whanne my lord the kyng hath slepte with hise fadris, Y and my sone Salomon schulen be synneris.
22 Alipokuwa angali anazungumza na mfalme, nabii Nathani akafika.
`While sche spak yit with the king, Nathan, the prophete, cam.
23 Wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa.” Kisha akaenda mbele ya mfalme na kumsujudia hadi uso wake ukagusa ardhi.
And thei telden to the kyng, and seiden, Nathan, the prophete, is present. And whanne he hadde entrid in the siyt of the kyng, and hadde worschipide hym lowli to erthe,
24 Nathani akasema, “Je, bwana wangu mfalme, umetangaza kuwa Adoniya atakuwa mfalme baada yako na kwamba ataketi kwenye kiti chako cha ufalme?
Nathan seide, My lord the kyng, seidist thou, Adonye regne aftir me, and sitte he on my trone?
25 Leo ameshuka na kutoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo. Amewaalika wana wote wa mfalme, jemadari wa jeshi na kuhani Abiathari. Sasa hivi, wanakula na kunywa pamoja naye wakisema, ‘Aishi maisha marefu, Mfalme Adoniya!’
For he cam doun to dai, and offride oxis, and fatte thingis, and ful many wetheris; and he clepide alle the sones of the kyng, also Abiathar, preest; and whanne thei eten, and drunken bifor hym, and seiden, Kyng Adonye lyue;
26 Lakini mimi mtumishi wako, kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada na mtumishi wako Solomoni hakutualika.
he clepide not me, thi seruaunt, and Sadoch, preest, and Banaie, sone of Joiada, and Salomon, thi sone.
27 Je, hili ni jambo ambalo bwana wangu mfalme amelifanya pasipo kuwajulisha watumishi wake ili wapate kujua ni nani atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake?”
Whether this word yede out fro my lord the kyng, and thou schewidist not to me, thi seruaunt, who schulde sitte on the trone of my lord the king after hym?
28 Ndipo Mfalme Daudi akasema, “Mwite Bathsheba, aingie ndani.” Hivyo akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele yake.
And kyng Dauid answeride, and seide, Clepe ye Bersabee to me. And whanne sche hadde entrid bifor the kyng, and hadde stonde bifor hym, the kyng swoor,
29 Ndipo mfalme akaapa: “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka kila taabu,
and seide, The Lord lyueth, that delyueryde my lijf fro al angwisch;
30 hakika nitatekeleza leo kile nilichokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli: Mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha ufalme baada yangu.”
for as Y swore to thee bi the Lord God of Israel, and seide, Salomon, thi sone, schal regne after me, and he schal sitte on my trone for me, so Y schal do to dai.
31 Kisha Bathsheba akasujudu akipiga magoti mbele ya mfalme uso wake ukigusa ardhi akasema, “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi milele!”
And Bersabee, with the cheer cast doun in to erthe, worschipide the kyng, and seide, My lord the kyng Dauid lyue with outen ende.
32 Mfalme Daudi akasema, “Mwite kuhani Sadoki ndani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Walipofika mbele ya mfalme,
And kyng Dauid seide, Clepe ye Sadoch, the preest, to me, and Nathan, the prophete, and Banaie, sone of Joiada. And whanne thei hadden entrid bifor the kyng,
33 akawaambia: “Wachukueni watumishi wa bwana wenu pamoja nanyi na mkamkalishe mwanangu Solomoni juu ya nyumbu wangu mwenyewe mkamteremshe hadi Gihoni.
the kyng seide to hem, Take with you the seruauntis of youre lord, and putte ye my sone Salomon on my mule, and lede ye hym in to Gyon.
34 Huko kuhani Sadoki na nabii Nathani wamtie mafuta awe mfalme juu ya Israeli. Pigeni tarumbeta na mpaze sauti, ‘Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!’
And Sadoch, the preest, and Nathan, the profete, anoynte hym in to kyng on Israel and Juda; and ye schulen synge with a clarioun, and ye schulen seie, Lyue kyng Salomon!
35 Kisha mtapanda pamoja naye, atakuja na kuketi kwenye kiti changu cha ufalme na kutawala badala yangu. Nimemweka awe mtawala juu ya Israeli na Yuda.”
Ye schulen stie aftir hym, and ye schulen come to Jerusalem; and he schal sitte on my trone, and he schal regne for me; and Y schal comaunde to hym, that he be duyk on Israel and on Juda.
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, “Amen! Bwana, Mungu wa bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
And Banaie, sone of Joiada, answeride to the kyng, and seide, Amen, `that is, so be it, ether verili, ether feithfuli; so speke the Lord God of my lord the kyng.
37 Kama vile Bwana alivyokuwa na bwana wangu mfalme, vivyo hivyo na awe na Solomoni kukifanya kiti chake cha utawala kuwa kikuu kuliko kile cha bwana wangu Mfalme Daudi!”
As the Lord was with my lord the kyng, so be he with Salomon, and make he the trone of Salomon heiyere than the trone of my lord the kyng Dauid.
38 Hivyo kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi wakampandisha Solomoni juu ya nyumbu wa Mfalme Daudi, nao wakamsindikiza hadi Gihoni.
Therfor Sadoch, the preest, yede doun, and Nathan, the prophete, and Banaie, sone of Joiada, and Cerethi, and Ferethi; and thei puttiden Salomon on the mule of Dauid, the kyng, and thei brouyten hym in to Gion.
39 Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta kutoka kwenye hema takatifu na kumtia Solomoni mafuta. Kisha wakapiga tarumbeta na watu wote wakapaza sauti wakisema, “Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!”
And Sadoch, the preest, took an horn of oile of the tabernacle, and anoyntide Salomon; and thei sungen with a clarioun; and al the puple seide, Lyue kyng Salomon!
40 Na watu wote wakakwea wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hata ardhi ikatikisika kwa ile sauti.
And al the multitude stiede after hym, and the puple of men syngynge with pipis, and `of men beynge glad with greet ioye, `stiede aftir hym; and the erthe sownede of the cry of hem.
41 Adoniya pamoja na wageni wote waliokuwa pamoja naye wakasikia sauti hiyo walipokuwa wakimalizia karamu yao. Waliposikia sauti ya tarumbeta, Yoabu akauliza, “Nini maana ya makelele yote haya katika mji?”
Forsothe Adonye herde, and alle that weren clepid of hym to feeste; and thanne the feeste was endid. But also Joab seide, whanne the vois of trumpe was herd, What wole it to it silf the cry of the citee makynge noise?
42 Hata alipokuwa anasema, Yonathani mwana wa kuhani Abiathari akafika. Adoniya akasema, “Ingia ndani. Mtu mstahiki kama wewe ni lazima alete habari njema.”
Yit the while he spak, Jonathan, sone of Abiathar, the preest, cam; to whom Adonye seide, Entre thou, for thou art a strong man, and tellynge goode thingis.
43 Yonathani akajibu, “La hasha! Mfalme Daudi bwana wetu amemfanya Solomoni kuwa mfalme.
And Jonathan answeride to Adonye, Nay; for oure lord the kyng Dauid hath ordeyned Salomon kyng;
44 Mfalme amemtuma pamoja naye kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi, nao wamempandisha juu ya nyumbu wa mfalme,
and Dauid sente with Salomon Sadoch, the preest, and Nathan, the prophete, and Banaie, sone of Joiada, and Cerethi, and Ferethi; and thei puttiden Salomon on the mule of the kyng.
45 nao kuhani Sadoki na nabii Nathani wamemtia mafuta kuwa mfalme huko Gihoni. Kuanzia hapo wameendelea kushangilia na sauti zimeenea pote mjini. Hizo ndizo kelele unazosikia.
And Sadoch, the preest, and Nathan, the prophete, anoyntiden hym kyng in Gion; and thei camen doun fro thennus beynge glad, and the citee sownede; this is the vois which ye herden.
46 Zaidi ya hayo, Solomoni ameketi juu ya kiti chake cha ufalme.
But also Salomon sittith on the trone of rewme;
47 Pia, maafisa wa mfalme wamekuja ili kumtakia heri bwana wetu Mfalme Daudi wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Solomoni kuwa mashuhuri kuliko lako na kiti chake cha ufalme kiwe na ukuu kuliko chako!’ Naye mfalme akasujudu akiabudu kitandani mwake
and the seruauntis of the kyng entriden, and blessiden oure lord the kyng Dauid, and seiden, God make large the name of Salomon aboue thi name, and magnyfye his trone aboue thi trone. And kyng Dauid worschipide in his bed;
48 na kusema, ‘Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye ameruhusu macho yangu kuona mrithi juu ya kiti changu cha ufalme leo hii.’”
and ferthermore he spak these thingis, Blessid be the Lord God of Israel, that yaf to dai a sittere in my trone, while myn iyen seen.
49 Katika hili, wageni wote wa Adoniya wakainuka kwa mshtuko wa hofu na kutawanyika.
Therfor alle, that weren clepid of Adonye to feeste, weren aferd, and risiden, and ech man yede in to his weie.
50 Lakini Adoniya kwa kumwogopa Solomoni, akaenda na kushika pembe za madhabahu.
Sotheli Adonye dredde Salomon, and roos, and yede in to the tabernacle of the Lord, and helde the horn of the auter.
51 Kisha Solomoni akaambiwa, “Adoniya anamwogopa Mfalme Solomoni na ameshikilia pembe za madhabahu. Anasema, ‘Mfalme Solomoni na aniapie leo kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’”
And thei telden to Salomon, and seiden, Lo! Adonye dredith the kyng Salomon, and holdith the horn of the auter, and seith, Kyng Salomon swere to me to dai, that he schal not sle his seruaunt bi swerd.
52 Solomoni akajibu, “Kama akijionyesha kuwa mtu mstahiki, hakuna unywele wake utakaoanguka juu ya ardhi, lakini kama uovu ukionekana ndani yake, atakufa.”
And Salomon seide, If he is a good man, sotheli not oon heer of hym schal falle in to erthe; but if yuel be foundun in hym, he schal die.
53 Ndipo Mfalme Solomoni akawatuma watu, nao wakamshusha kutoka madhabahuni. Naye Adoniya akaja akamwinamia Mfalme Solomoni, naye Solomoni akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
Therfor kyng Salomon sente, and ledde `hym out fro the auter; and he entride, and worschipide kyng Salomon; and Salomon seide to hym, Go in to thin hows.

< 1 Wafalme 1 >