< 1 Wafalme 1 >

1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo.
Now king David was old, stricken in years; and they covered him with clothes, but he could not become warm.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.”
Wherefore his servants said unto him, Let them seek out for my lord the king a young virgin, and let her stand before the king, and let her be an attendant on him; and let her lie in thy bosom, that my lord the king may become warm.
3 Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri wa sura na wakampata Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
So they sought for a fair maiden throughout all the territory of Israel; and they found Abishag the Shunammite, and brought her to the king.
4 Msichana huyo alikuwa mzuri sana wa sura, akamtunza mfalme na kumhudumia, lakini mfalme hakufanya naye tendo la ndoa.
And the maiden was exceedingly fair; and she became an attendant on the king, and ministered to him; but the king knew her not.
5 Basi Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi, akajigamba na kusema, “Mimi nitakuwa mfalme.” Hivyo akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, pamoja na watu hamsini wa kumtangulia wakikimbia.
And Adoniyah the son of Chaggith exalted himself, saying, I shall be king: and he procured himself a chariot and horsemen, and fifty men who ran before him.
6 (Baba yake hakuwa ameingilia na kumuuliza, “Kwa nini unafanya hivyo?” Alikuwa pia kijana mzuri sana wa sura, na alizaliwa baada ya Absalomu.)
And his father had never grieved him in all his life by saying, Why hast thou done so? and he also was of a very goodly form; and his mother had born him after Abshalom.
7 Adoniya akashauriana pamoja na Yoabu mwana wa Seruya na kuhani Abiathari, nao wakamsaidia.
And he had conferences with Joab the son of Zeruyah, and with Ebyathar the priest: and they, following Adoniyah, helped him.
8 Lakini kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, Nathani nabii, Shimei, Rei na walinzi maalum wa Daudi hawakujiunga na Adoniya.
But Zadok the priest, and Benayahu the son of Yehoyada', and Nathan the prophet, and Shim'i, and Re'i, and the mighty men that belonged to David, were not with Adoniyah.
9 Ndipo Adoniya akatoa dhabihu ya kondoo, ngʼombe na ndama walionona kwenye Jiwe la Zohelethi karibu na En-Rogeli. Akawaalika ndugu zake wote, wana wa mfalme na wanaume wote wa Yuda waliokuwa maafisa wa mfalme,
And Adoniyah slaughtered sheep and oxen and fatted cattle by the stone Zocheleth, which is by 'En-rogel; and he invited all his brothers the king's sons, and all the men of Judah the king's servants;
10 lakini hakumwalika nabii Nathani, Benaya, walinzi maalum wa mfalme, wala ndugu yake Solomoni.
But Nathan the prophet, and Benayahu, and the mighty men, and Solomon his brother, he invited not.
11 Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, “Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili?
And Nathan spoke unto Bath-sheba' the mother of Solomon, saying, Hast thou not heard that Adoniyah the son of Chaggith is become king, and [that] David our lord knoweth it not?
12 Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni.
And now come, let me, I pray thee, give thee counsel, that thou mayest save thy own life, and the life of thy son Solomon.
13 Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, ‘Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: “Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?’
Go and get thee in unto king David, and say unto him, Didst not thou, my lord, O king, swear unto thy hand-maid, saying, Assuredly, Solomon thy son shall reign after me, and only he shall sit upon my throne? why then is Adoniyah become king?
14 Utakapokuwa ukizungumza na mfalme, nitaingia na kuthibitisha hayo uliyoyasema.”
And, lo, while thou shalt be yet speaking there with the king, I myself will come in after thee, and confirm thy words.
15 Hivyo Bathsheba akaenda kumwona mfalme chumbani mwake mahali ambapo Abishagi, Mshunami, alikuwa akimhudumia, naye mfalme alikuwa mzee sana.
And Bath-sheba' went in unto the king into the chamber, and the king was very old; and Abishag the Shunammite was ministering unto the king.
16 Bathsheba akasujudu na kupiga magoti mbele ya mfalme. Mfalme akauliza, “Ni nini hiki unachotaka?”
And Bath-sheba' bowed, and prostrated herself unto the king: and the king said, What wouldst thou?
17 Akamwambia, “Bwana wangu, wewe mwenyewe uliniapia mimi mtumishi wako kwa Bwana Mungu wako kwamba: ‘Solomoni Mwanao atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha ufalme.’
And she said unto him, My lord, thou thyself didst swear by the Lord thy God unto thy hand-maid, Assuredly, Solomon thy son shall reign after me, and only he shall sit upon my throne.
18 Lakini sasa Adoniya amekuwa mfalme, nawe, bwana wangu mfalme huna habari kuhusu jambo hilo.
And now, behold, Adoniyah is become king; and now, my lord, O king, thou knowest it not:
19 Ametoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo, naye amewaalika wana wa mfalme wote, kuhani Abiathari, na Yoabu jemadari wa jeshi, lakini hakumwalika Solomoni mtumishi wako.
And he hath slaughtered oxen and fatted cattle and sheep in abundance, and hath invited all the sons of the king, and Ebyathar the priest, and Joab the captain of the army; but Solomon thy servant hath he not invited.
20 Bwana wangu mfalme, macho ya Israeli yote yanakutazama wewe wajue kutoka kwako kuwa ni nani atakayeketi katika kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.
And as for thee, my lord, O king, the eyes of all Israel are upon thee, to tell them, who shall sit on the throne of my lord the king after him.
21 Kama sivyo, mara tu bwana wangu mfalme atakapopumzishwa pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Solomoni tutatendewa kama wahalifu.”
Otherwise it would come to pass, when my lord the king sleepeth with his fathers, that I and my son Solomon may be counted offenders.
22 Alipokuwa angali anazungumza na mfalme, nabii Nathani akafika.
And, lo, while she was yet speaking with the king, Nathan the prophet also came in.
23 Wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa.” Kisha akaenda mbele ya mfalme na kumsujudia hadi uso wake ukagusa ardhi.
And they told the king, saying, Behold, here is Nathan the prophet: and when he was come in before the king, he prostrated himself before the king with his face to the ground.
24 Nathani akasema, “Je, bwana wangu mfalme, umetangaza kuwa Adoniya atakuwa mfalme baada yako na kwamba ataketi kwenye kiti chako cha ufalme?
And Nathan said, My lord, O king, hast thou then said, Adoniyah shall reign after me, and he shall sit upon my throne?
25 Leo ameshuka na kutoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo. Amewaalika wana wote wa mfalme, jemadari wa jeshi na kuhani Abiathari. Sasa hivi, wanakula na kunywa pamoja naye wakisema, ‘Aishi maisha marefu, Mfalme Adoniya!’
For he is gone down this day, and hath slaughtered oxen and fatted cattle and sheep in abundance, and hath invited all the king's sons, and the captains of the army, and Ebyathar the priest: and, behold, they are eating and drinking before him, and they say, Long live king Adoniyah.
26 Lakini mimi mtumishi wako, kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada na mtumishi wako Solomoni hakutualika.
But as for me, me thy servant, and Zadok the priest, and Benayahu the son of Yehoyada', and thy servant Solomon, hath he not invited.
27 Je, hili ni jambo ambalo bwana wangu mfalme amelifanya pasipo kuwajulisha watumishi wake ili wapate kujua ni nani atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake?”
Can it be that this hath been done by order of my lord the king, and thou hast not informed thy servant, who should sit on the throne of my lord the king after him?
28 Ndipo Mfalme Daudi akasema, “Mwite Bathsheba, aingie ndani.” Hivyo akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele yake.
Then answered king David, and said, Call me Bath-sheba'; and she came into the king's presence, and stood before the king.
29 Ndipo mfalme akaapa: “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka kila taabu,
And the king swore and said, As the Lord liveth, that hath redeemed my soul out of all distress,
30 hakika nitatekeleza leo kile nilichokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli: Mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha ufalme baada yangu.”
Even as I have sworn unto thee by the Lord the God of Israel, saying, Assuredly Solomon thy son shall reign after me, and only he shall sit upon my throne in my stead: even so will I certainly do this day.
31 Kisha Bathsheba akasujudu akipiga magoti mbele ya mfalme uso wake ukigusa ardhi akasema, “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi milele!”
Then did Bath-sheba' bow herself with her face to the earth, and prostrate herself unto the king; and she said, May my lord, the king David, live for ever!
32 Mfalme Daudi akasema, “Mwite kuhani Sadoki ndani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Walipofika mbele ya mfalme,
And king David said, Call unto me Zadok the priest, and Nathan the prophet, and Benayahu the son of Yehoyada'. And they came before the king.
33 akawaambia: “Wachukueni watumishi wa bwana wenu pamoja nanyi na mkamkalishe mwanangu Solomoni juu ya nyumbu wangu mwenyewe mkamteremshe hadi Gihoni.
And the king said unto them, Take with you the servants of your lord, and cause Solomon my son to ride upon my own mule, and conduct him down to Gichon:
34 Huko kuhani Sadoki na nabii Nathani wamtie mafuta awe mfalme juu ya Israeli. Pigeni tarumbeta na mpaze sauti, ‘Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!’
And let Zadok the priest with Nathan the prophet anoint him there as king over Israel; and blow ye with the cornet, and say, Long live king Solomon.
35 Kisha mtapanda pamoja naye, atakuja na kuketi kwenye kiti changu cha ufalme na kutawala badala yangu. Nimemweka awe mtawala juu ya Israeli na Yuda.”
Then shall ye go up after him, and he shall come and sit upon my throne; and he shall be king in my stead: and him have I ordained to be ruler over Israel and over Judah.
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, “Amen! Bwana, Mungu wa bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
And Benayahu the son of Yehoyada' answered the king, and said, Amen: May thus say the Eternal the God of my lord the king.
37 Kama vile Bwana alivyokuwa na bwana wangu mfalme, vivyo hivyo na awe na Solomoni kukifanya kiti chake cha utawala kuwa kikuu kuliko kile cha bwana wangu Mfalme Daudi!”
As the Eternal hath been with my lord the king, even so may he be with Solomon, and may he make his throne greater than the throne of my lord the king David.
38 Hivyo kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi wakampandisha Solomoni juu ya nyumbu wa Mfalme Daudi, nao wakamsindikiza hadi Gihoni.
Thereupon Zadok the priest, and Nathan the prophet, and Benayahu the son of Yehoyada', and the Kerethites, and the Pelethites, went down, and caused Solomon to ride upon king David's mule, and conducted him to Gichon.
39 Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta kutoka kwenye hema takatifu na kumtia Solomoni mafuta. Kisha wakapiga tarumbeta na watu wote wakapaza sauti wakisema, “Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!”
And Zadok the priest took the horn of oil out of the tabernacle, and anointed Solomon. And they blew with the cornet; and all the people said, Long live king Solomon.
40 Na watu wote wakakwea wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hata ardhi ikatikisika kwa ile sauti.
And all the people went up after him, and the people blew on flutes, and rejoiced with great joy, so that the earth was rent at their noise.
41 Adoniya pamoja na wageni wote waliokuwa pamoja naye wakasikia sauti hiyo walipokuwa wakimalizia karamu yao. Waliposikia sauti ya tarumbeta, Yoabu akauliza, “Nini maana ya makelele yote haya katika mji?”
And Adoniyah and all the guests that were with him heard it as they had just finished eating: and when Joab heard the sound of the cornet, he said, Wherefore is this noise of the city in an uproar?
42 Hata alipokuwa anasema, Yonathani mwana wa kuhani Abiathari akafika. Adoniya akasema, “Ingia ndani. Mtu mstahiki kama wewe ni lazima alete habari njema.”
And while he was yet speaking, behold, Jonathan the son of Ebyathar the priest came in: and Adoniyah said [unto him], Come in; for thou art a worthy man, and must bring good tidings.
43 Yonathani akajibu, “La hasha! Mfalme Daudi bwana wetu amemfanya Solomoni kuwa mfalme.
And Jonathan answered and said to Adoniyah, Alas, no; our lord king David hath made Solomon king;
44 Mfalme amemtuma pamoja naye kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi, nao wamempandisha juu ya nyumbu wa mfalme,
And the king hath sent with him Zadok the priest, and Nathan the prophet, and Benayahu the son of Yehoyada', and the Kerethites, and the Pelethites, and they have caused him to ride upon the king's mule;
45 nao kuhani Sadoki na nabii Nathani wamemtia mafuta kuwa mfalme huko Gihoni. Kuanzia hapo wameendelea kushangilia na sauti zimeenea pote mjini. Hizo ndizo kelele unazosikia.
And Zadok the priest and Nathan the prophet have anointed him as king on the Gichon; and they are come up from there rejoicing, and the city hath been set in commotion. This is the noise that ye have heard.
46 Zaidi ya hayo, Solomoni ameketi juu ya kiti chake cha ufalme.
And Solomon hath also sat on the kingly throne.
47 Pia, maafisa wa mfalme wamekuja ili kumtakia heri bwana wetu Mfalme Daudi wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Solomoni kuwa mashuhuri kuliko lako na kiti chake cha ufalme kiwe na ukuu kuliko chako!’ Naye mfalme akasujudu akiabudu kitandani mwake
And also the king's servants are come to bless our lord king David, saying, May God make the name of Solomon more famous than thy name, and make his throne greater than thy throne: and the king hath bowed himself upon the bed.
48 na kusema, ‘Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye ameruhusu macho yangu kuona mrithi juu ya kiti changu cha ufalme leo hii.’”
And also thus hath the king said, Blessed be the Lord the God of Israel, who hath given [me] this day one who sitteth on my throne, while my eyes see it.
49 Katika hili, wageni wote wa Adoniya wakainuka kwa mshtuko wa hofu na kutawanyika.
And all the guests that were with Adoniyah were terrified, and rose up, and went, every man, on his own way.
50 Lakini Adoniya kwa kumwogopa Solomoni, akaenda na kushika pembe za madhabahu.
And Adoniyah was afraid because of Solomon; and he arose, and went, and caught hold on the horns of the altar.
51 Kisha Solomoni akaambiwa, “Adoniya anamwogopa Mfalme Solomoni na ameshikilia pembe za madhabahu. Anasema, ‘Mfalme Solomoni na aniapie leo kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’”
And it was told unto Solomon, saying, Behold, Adoniyah feareth king Solomon; and, behold, he hath caught hold on the horns of the altar, saying, Let king Solomon swear unto me today that he will not slay his servant with the sword.
52 Solomoni akajibu, “Kama akijionyesha kuwa mtu mstahiki, hakuna unywele wake utakaoanguka juu ya ardhi, lakini kama uovu ukionekana ndani yake, atakufa.”
And Solomon said, If he will become a worthy man, there shall not a hair of his fall to the earth; but if any wrong shall be found on him, then shall he die.
53 Ndipo Mfalme Solomoni akawatuma watu, nao wakamshusha kutoka madhabahuni. Naye Adoniya akaja akamwinamia Mfalme Solomoni, naye Solomoni akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
So king Solomon sent, and they brought him down from the altar; and he came and bowed himself to king Solomon; and Solomon said unto him, Go to thy house.

< 1 Wafalme 1 >