< 1 Wafalme 1 >

1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo.
Now king David had become elderly, and he had many days in his lifetime. And though he was covered with clothes, he was not warmed.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.”
Therefore, his servants said to him: “Let us seek, for our lord the king, a young virgin. And let her stand before the king, and warm him, and sleep in his bosom, and provide warmth for our lord the king.”
3 Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri wa sura na wakampata Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
And so they sought a beautiful young woman in all the parts of Israel. And they found Abishag, a Shunammite, and they led her to the king.
4 Msichana huyo alikuwa mzuri sana wa sura, akamtunza mfalme na kumhudumia, lakini mfalme hakufanya naye tendo la ndoa.
Now the girl was exceedingly beautiful. And she slept with the king, and she ministered to him. Yet truly, the king did not know her.
5 Basi Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi, akajigamba na kusema, “Mimi nitakuwa mfalme.” Hivyo akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, pamoja na watu hamsini wa kumtangulia wakikimbia.
Then Adonijah, the son of Haggith, exalted himself, saying, “I shall reign!” And he appointed for himself chariots and horsemen, with fifty men who would run before him.
6 (Baba yake hakuwa ameingilia na kumuuliza, “Kwa nini unafanya hivyo?” Alikuwa pia kijana mzuri sana wa sura, na alizaliwa baada ya Absalomu.)
Neither did his father chastise him at any time, saying, “Why have you done this?” Now he, too, was very beautiful, the second in birth, after Absalom.
7 Adoniya akashauriana pamoja na Yoabu mwana wa Seruya na kuhani Abiathari, nao wakamsaidia.
And he conferred with Joab, the son of Zeruiah, and with Abiathar, the priest, who gave assistance to the side of Adonijah.
8 Lakini kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, Nathani nabii, Shimei, Rei na walinzi maalum wa Daudi hawakujiunga na Adoniya.
Yet truly, Zadok, the priest, and Benaiah, the son of Jehoiada, and Nathan, the prophet, and Shimei and Rei, and the mature men of the army of David were not with Adonijah.
9 Ndipo Adoniya akatoa dhabihu ya kondoo, ngʼombe na ndama walionona kwenye Jiwe la Zohelethi karibu na En-Rogeli. Akawaalika ndugu zake wote, wana wa mfalme na wanaume wote wa Yuda waliokuwa maafisa wa mfalme,
Then Adonijah, having immolated rams and calves and every kind of fat cattle beside the Stone of the Serpent, which was in the vicinity of the fountain Rogel, summoned all his brothers, the sons of the king, and all the men of Judah, the servants of the king.
10 lakini hakumwalika nabii Nathani, Benaya, walinzi maalum wa mfalme, wala ndugu yake Solomoni.
But he did not summon Nathan, the prophet, and Benaiah, and all the mature men, and Solomon, his brother.
11 Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, “Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili?
And so Nathan said to Bathsheba, the mother of Solomon: “Have you not heard that Adonijah, the son of Haggith, has begun to reign, and that our lord David is ignorant of this?
12 Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni.
Now then, come, accept my counsel, and save your life and the life of your son Solomon.
13 Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, ‘Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: “Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?’
Go and enter to king David, and say to him: ‘Did you not, my lord the king, swear to me, your handmaid, saying: “Your son Solomon shall reign after me, and he himself shall sit on my throne?” Then why does Adonijah reign?’
14 Utakapokuwa ukizungumza na mfalme, nitaingia na kuthibitisha hayo uliyoyasema.”
And while you are still speaking with the king there, I will enter after you, and I will complete your words.”
15 Hivyo Bathsheba akaenda kumwona mfalme chumbani mwake mahali ambapo Abishagi, Mshunami, alikuwa akimhudumia, naye mfalme alikuwa mzee sana.
And so Bathsheba entered to the king in the bedroom. Now the king was very old, and Abishag, the Shunammite, was ministering to him.
16 Bathsheba akasujudu na kupiga magoti mbele ya mfalme. Mfalme akauliza, “Ni nini hiki unachotaka?”
Bathsheba bowed herself, and she reverenced the king. And the king said to her, “What do you wish?”
17 Akamwambia, “Bwana wangu, wewe mwenyewe uliniapia mimi mtumishi wako kwa Bwana Mungu wako kwamba: ‘Solomoni Mwanao atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha ufalme.’
And responding, she said: “My lord, you swore to your handmaid, by the Lord your God: ‘your son Solomon will reign after me, and he himself shall sit upon my throne.’
18 Lakini sasa Adoniya amekuwa mfalme, nawe, bwana wangu mfalme huna habari kuhusu jambo hilo.
And now behold, Adonijah reigns, while you, my lord the king, are ignorant of it.
19 Ametoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo, naye amewaalika wana wa mfalme wote, kuhani Abiathari, na Yoabu jemadari wa jeshi, lakini hakumwalika Solomoni mtumishi wako.
He has slain oxen, and every kind of fattened cattle, and many rams. And he has summoned all the sons of the king, as well as Abiathar, the priest, and Joab, the leader of the military. But Solomon, your servant, he did not summon.
20 Bwana wangu mfalme, macho ya Israeli yote yanakutazama wewe wajue kutoka kwako kuwa ni nani atakayeketi katika kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.
Truly now, my lord the king, the eyes of all of Israel look with favor upon you, that you may indicate to them who ought to sit upon your throne, my lord the king, after you.
21 Kama sivyo, mara tu bwana wangu mfalme atakapopumzishwa pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Solomoni tutatendewa kama wahalifu.”
Otherwise, this will be: when my lord the king sleeps with his fathers, I and my son Solomon will be as sinners.”
22 Alipokuwa angali anazungumza na mfalme, nabii Nathani akafika.
And while she was still speaking with the king, Nathan, the prophet, arrived.
23 Wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa.” Kisha akaenda mbele ya mfalme na kumsujudia hadi uso wake ukagusa ardhi.
And they announced to the king, saying, “Nathan, the prophet, is here.” And when he had entered in the sight of the king, and he had reverenced prone on the ground,
24 Nathani akasema, “Je, bwana wangu mfalme, umetangaza kuwa Adoniya atakuwa mfalme baada yako na kwamba ataketi kwenye kiti chako cha ufalme?
Nathan said: “My lord the king, did you say, ‘Let Adonijah reign after me, and let him sit upon my throne?’
25 Leo ameshuka na kutoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo. Amewaalika wana wote wa mfalme, jemadari wa jeshi na kuhani Abiathari. Sasa hivi, wanakula na kunywa pamoja naye wakisema, ‘Aishi maisha marefu, Mfalme Adoniya!’
For today, he descended, and he immolated oxen, and fattened cattle, and many rams. And he summoned all the sons of the king, and the leaders of the army, along with Abiathar, the priest. And they are eating and drinking before him, and saying, ‘As king Adonijah lives.’
26 Lakini mimi mtumishi wako, kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada na mtumishi wako Solomoni hakutualika.
But he did not summon me, your servant, and Zadok, the priest, and Benaiah, the son of Jehoiada, and Solomon, your lowly servant.
27 Je, hili ni jambo ambalo bwana wangu mfalme amelifanya pasipo kuwajulisha watumishi wake ili wapate kujua ni nani atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake?”
Could this word have gone out from my lord the king, and could you not have revealed it to me, your servant, as to who would be seated upon the throne of my lord the king after him?”
28 Ndipo Mfalme Daudi akasema, “Mwite Bathsheba, aingie ndani.” Hivyo akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele yake.
And king David responded, saying, “Summon to me Bathsheba.” And when she had entered before the king, and she had stood before him,
29 Ndipo mfalme akaapa: “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka kila taabu,
the king swore and said: “As the Lord lives, who has rescued my soul from all distress,
30 hakika nitatekeleza leo kile nilichokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli: Mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha ufalme baada yangu.”
just as I swore to you by the Lord God of Israel, saying: ‘Your son Solomon shall reign after me, and he himself shall sit upon my throne in my place,’ so shall I do this day.”
31 Kisha Bathsheba akasujudu akipiga magoti mbele ya mfalme uso wake ukigusa ardhi akasema, “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi milele!”
And Bathsheba, having lowered her face to the ground, reverenced the king, saying, “May my lord David live forever.”
32 Mfalme Daudi akasema, “Mwite kuhani Sadoki ndani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Walipofika mbele ya mfalme,
And king David said, “Summon to me Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, and Benaiah, the son of Jehoiada.” And when they had entered before the king,
33 akawaambia: “Wachukueni watumishi wa bwana wenu pamoja nanyi na mkamkalishe mwanangu Solomoni juu ya nyumbu wangu mwenyewe mkamteremshe hadi Gihoni.
he said to them: “Take with you the servants of your lord, and place my son Solomon upon my mule. And lead him to Gihon.
34 Huko kuhani Sadoki na nabii Nathani wamtie mafuta awe mfalme juu ya Israeli. Pigeni tarumbeta na mpaze sauti, ‘Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!’
And let Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, anoint him in that place as the king over Israel. And you shall sound the trumpet, and you shall say, ‘As king Solomon lives.’
35 Kisha mtapanda pamoja naye, atakuja na kuketi kwenye kiti changu cha ufalme na kutawala badala yangu. Nimemweka awe mtawala juu ya Israeli na Yuda.”
And you shall ascend after him, and he shall arrive and shall sit upon my throne. And he himself shall reign in my place. And I will command that he be the ruler over Israel and over Judah.”
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, “Amen! Bwana, Mungu wa bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
And Benaiah, the son of Jehoiada, responded to the king, saying: “Amen. So says the Lord, the God of my lord the king.
37 Kama vile Bwana alivyokuwa na bwana wangu mfalme, vivyo hivyo na awe na Solomoni kukifanya kiti chake cha utawala kuwa kikuu kuliko kile cha bwana wangu Mfalme Daudi!”
In the same way that the Lord has been with my lord the king, so may he be with Solomon. And may he make his throne more sublime than the throne of my lord, king David.”
38 Hivyo kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi wakampandisha Solomoni juu ya nyumbu wa Mfalme Daudi, nao wakamsindikiza hadi Gihoni.
Then Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, descended, with Benaiah, the son of Jehoiada, and the Cherethites and Pelethites. And they placed Solomon on the mule of king David, and they led him to Gihon.
39 Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta kutoka kwenye hema takatifu na kumtia Solomoni mafuta. Kisha wakapiga tarumbeta na watu wote wakapaza sauti wakisema, “Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!”
And Zadok, the priest, took the horn of oil from the tabernacle, and he anointed Solomon. And they sounded the trumpet. And all the people said, “As king Solomon lives.”
40 Na watu wote wakakwea wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hata ardhi ikatikisika kwa ile sauti.
And the entire multitude ascended after him. And the people were playing on pipes, and rejoicing with great joy. And the earth resounded before the noise of them.
41 Adoniya pamoja na wageni wote waliokuwa pamoja naye wakasikia sauti hiyo walipokuwa wakimalizia karamu yao. Waliposikia sauti ya tarumbeta, Yoabu akauliza, “Nini maana ya makelele yote haya katika mji?”
Then Adonijah, and all who had been summoned by him, heard it. And now the feast had ended. Then, too, Joab, hearing the voice of the trumpet, said, “What is the meaning of this clamor from the tumultuous city?”
42 Hata alipokuwa anasema, Yonathani mwana wa kuhani Abiathari akafika. Adoniya akasema, “Ingia ndani. Mtu mstahiki kama wewe ni lazima alete habari njema.”
While he was still speaking, Jonathan, the son of Abiathar the priest, arrived. And Adonijah said to him, “Enter, for you are a valiant man, and you report good news.”
43 Yonathani akajibu, “La hasha! Mfalme Daudi bwana wetu amemfanya Solomoni kuwa mfalme.
And Jonathan answered Adonijah: “By no means. For our lord king David has appointed Solomon as king.
44 Mfalme amemtuma pamoja naye kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi, nao wamempandisha juu ya nyumbu wa mfalme,
And he has sent with him Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, and Benaiah, the son of Jehoiada, and the Cherethites and Pelethites. And they have placed him on the mule of the king.
45 nao kuhani Sadoki na nabii Nathani wamemtia mafuta kuwa mfalme huko Gihoni. Kuanzia hapo wameendelea kushangilia na sauti zimeenea pote mjini. Hizo ndizo kelele unazosikia.
And Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, have anointed him king, at Gihon. And they are ascending from there, rejoicing, and so the city resounds. This is the noise that you have heard.
46 Zaidi ya hayo, Solomoni ameketi juu ya kiti chake cha ufalme.
But also, Solomon sits upon the throne of the kingdom.
47 Pia, maafisa wa mfalme wamekuja ili kumtakia heri bwana wetu Mfalme Daudi wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Solomoni kuwa mashuhuri kuliko lako na kiti chake cha ufalme kiwe na ukuu kuliko chako!’ Naye mfalme akasujudu akiabudu kitandani mwake
And the servants of the king, entering, have blessed our lord king David, saying: ‘May God amplify the name of Solomon above your name, and may he magnify his throne above your throne.’ And the king reverenced from his bed.
48 na kusema, ‘Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye ameruhusu macho yangu kuona mrithi juu ya kiti changu cha ufalme leo hii.’”
And he said: ‘Blessed is the Lord, the God of Israel, who today has bestowed someone to sit upon my throne, while my eyes may see it.’”
49 Katika hili, wageni wote wa Adoniya wakainuka kwa mshtuko wa hofu na kutawanyika.
Therefore, all those who had been summoned by Adonijah were terrified. And they all rose up, and each one went his own way.
50 Lakini Adoniya kwa kumwogopa Solomoni, akaenda na kushika pembe za madhabahu.
Then Adonijah, fearing Solomon, rose up and went away. And he took hold of the horn of the altar.
51 Kisha Solomoni akaambiwa, “Adoniya anamwogopa Mfalme Solomoni na ameshikilia pembe za madhabahu. Anasema, ‘Mfalme Solomoni na aniapie leo kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’”
And they reported to Solomon, saying: “Behold, Adonijah, fearing king Solomon, has taken hold of the horn of the altar, saying: ‘May king Solomon swear to me this day that he will not put to death his servant with the sword.’”
52 Solomoni akajibu, “Kama akijionyesha kuwa mtu mstahiki, hakuna unywele wake utakaoanguka juu ya ardhi, lakini kama uovu ukionekana ndani yake, atakufa.”
And Solomon said: “If he is a good man, not so much as one hair of his head shall fall to the ground. But if evil is found in him, he shall die.”
53 Ndipo Mfalme Solomoni akawatuma watu, nao wakamshusha kutoka madhabahuni. Naye Adoniya akaja akamwinamia Mfalme Solomoni, naye Solomoni akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
Therefore, king Solomon sent and brought him from the altar. And entering, he reverenced king Solomon. And Solomon said to him, “Go to your own house.”

< 1 Wafalme 1 >