< 1 Yohana 1 >
1 Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
That which was from the beginning, which we have heard, which we have seen with our eyes, which we for ourselves gazed upon, and our hands did handle, concerning the Word of Life, —
2 Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios )
And, the Life, was made manifest, and we have seen, and are bearing witness, and announcing unto you, the Age-abiding Life, which, indeed, was with the Father, and was made manifest unto us; (aiōnios )
3 Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo.
That which we have seen and heard, are we announcing, even unto you, in order that, ye too, may have fellowship with us, and, our own fellowship also, may be with the Father, and with his Son Jesus Christ.
4 Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
And, these things, are we writing, in order that, our joy, may be made full.
5 Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
And this is the message which we have heard from him, and are reporting unto you, —that, God, is, light, and in him is, no darkness at all.
6 Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
If we say—We have, fellowship, with him! and, in darkness, are walking, we are dealing falsely, and not doing the truth;
7 Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
Whereas, if, in the light, we are walking, as, he, is in the light, we have, fellowship one with another, and, the blood of Jesus his Son, is cleansing us from all sin.
8 Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
If we say—Sin, have we none! we are deceiving, ourselves, and, the truth, is not in us.
9 Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote.
If we are confessing our sins, faithful, is he and, righteous—that he should forgive us our sins, and cleanse us from all unrighteousness.
10 Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.
If we say—We have not sinned! false, are we making, him, and, his word, is not in us.