< 1 Yohana 4 >
1 Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni.
Najmilsi! nie każdemu duchowi wierzcie; ale doświadczajcie duchów, jeźli z Boga są. Bo wiele fałszywych proroków wyszło na świat.
2 Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu.
Przez to poznawajcie Ducha Bożego: Wszelki duch, który wyznaje, iż Jezus Chrystus w ciele przyszedł, z Boga jest.
3 Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.
Ale wszelki duch, który nie wyznaje, że Jezus Chrystus w ciele przyszedł, nie jest z Boga; ale ten jest on duch antychrystowy, o którymeście słyszeli, iż idzie i teraz już jest na świecie.
4 Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
Wy z Boga jesteście, dziateczki! i zwyciężyliście ich; iż większy jest ten, który w was jest, niż ten, który jest na świecie.
5 Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza.
Onić są z świata; przetoż o świecie mówią, a świat ich słucha.
6 Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.
My z Boga jesteśmy. Kto zna Boga, słucha nas; kto nie jest z Boga, nie słucha nas. Przez to poznajemy ducha prawdy i ducha błędu.
7 Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
Najmilsi! miłujmyż jedni drugich, gdyż miłość jest z Boga; i każdy, co miłuje, z Boga jest narodzony i zna Boga.
8 Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo.
Kto nie miłuje, nie zna Boga; gdyż Bóg jest miłość.
9 Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake.
Przez to objawiona jest miłość Boża ku nam, iż Syna swego jednorodzonego posłał Bóg na świat, abyśmy żyli przez niego.
10 Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.
W tem jest miłość, nie iżbyśmy my umiłowali Boga, ale iż on umiłował nas i posłał Syna swego, aby był ubłaganiem za grzechy nasze.
11 Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana.
Najmilsi! ponieważ nas tak Bóg umiłował, i myśmy powinni jedni drugich miłować.
12 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
Boga żaden nigdy nie widział; ale jeźli miłujemy jedni drugich, Bóg w nas mieszka, a miłość jego doskonała jest w nas.
13 Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake.
Przez to poznajemy, iż w nim mieszkamy, a on w nas, iż z Ducha swego nam dał.
14 Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu.
A myśmy widzieli i świadczymy, iż Ojciec posłał Syna, aby był Zbawicielem świata.
15 Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
Ktobykolwiek wyznał, iż Jezus jest Synem Bożym, Bóg w nim mieszka, a on w Bogu.
16 Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu. Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake.
I myśmy poznali i uwierzyli o miłości, którą Bóg ma ku nam. Bóg jest miłość; a kto mieszka w miłości, w Bogu mieszka, a Bóg w nim.
17 Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.
W tem doskonała jest miłość Boża z nami, abyśmy ufanie mieli w dzień sądny, iż jaki on jest, tacy i my jesteśmy na tym świecie.
18 Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.
Nie maszci bojaźni w miłości, ale miłość doskonała precz wyrzuca bojaźń: bo bojaźń ma udręczenie, a kto się boi, nie jest doskonały w miłości.
19 Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza.
My go miłujemy, iż on nas pierwej umiłował.
20 Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona?
Jeźliby kto rzekł: Miłuję Boga, a brata by swego nienawidził, kłamcą jest; albowiem kto nie miłuje brata swego, którego widział, Boga, którego nie widział, jakoż może miłować?
21 Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.
A toć rozkazanie mamy od niego, aby ten, co miłuje Boga, miłował i brata swego.