< 1 Yohana 4 >

1 Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni.
Beloved, believe not every spirit, but try the spirits whether they are of God: because many false prophets have gone out into the world.
2 Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu.
By this ye know the Spirit of God: Every spirit that confesseth that Jesus Christ hath come in the flesh, is from God:
3 Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.
And every spirit that confesseth not that Jesus Christ is come in the flesh, is not from God. And this is that [spirit] of antichrist, of which ye have heard that it should come; and even now already it is in the world.
4 Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
Ye are of God, little children, and have overcome them: because greater is he that is in you, than he that is in the world.
5 Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza.
They are of the world: therefore they speak from the world, and the world heareth them.
6 Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.
We are of God. He that knoweth God, heareth us; he that is not of God, heareth not us. By this we know the spirit of truth, and the spirit of error.
7 Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
Beloved, let us love one another: for love is from God; and every one that loveth is born of God, and knoweth God.
8 Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo.
He that loveth not, knoweth not God; for God is love.
9 Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake.
In this was manifested the love of God towards us, because that God sent his only begotten Son into the world, that we might live through him.
10 Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.
In this is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son [to be] the propitiation for our sins.
11 Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana.
Beloved, if God so loved us, we ought also to love one another.
12 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
No man hath seen God at any time. If we love one another, God dwelleth in us, and his love is perfected in us.
13 Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake.
By this we know that we dwell in him, and he in us, because he hath given us of his Spirit.
14 Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu.
And we have seen and do testify, that the Father sent the Son [to be] the Savior of the world.
15 Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
Whoever shall confess that Jesus is the Son of God, God dwelleth in him, and he in God.
16 Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu. Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake.
And we have known and believed the love that God hath to us. God is love: and he that dwelleth in love, dwelleth in God, and God in him.
17 Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.
In this is our love made perfect, that we may have boldness in the day of judgment: because as he is, so are we in this world.
18 Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.
There is no fear in love; but perfect love casteth out fear: because fear hath torment. He that feareth, is not made perfect in love.
19 Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza.
We love him, because he first loved us.
20 Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona?
If a man sayeth, I love God, and hateth his brother, he is a liar. For he that loveth not his brother, whom he hath seen, how can he love God, whom he hath not seen?
21 Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.
And this commandment have we from him, That he who loveth God, love his brother also.

< 1 Yohana 4 >