< 1 Yohana 4 >

1 Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni.
Do not believe every spirit, beloved, but test the spirits to see whether they are of God; for many false prophets are gone out into the world.
2 Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu.
By this you know the Spirit of God; every spirit that confesses that Jesus Christ is come in the flesh is from God;
3 Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.
and every spirit which confesses him not, is not from God. And this is that spirit of Antichrist of which you have heard that it is coming, and that now it is already in the world.
4 Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
My little children, you are of God and have conquered them; because he that is within you is greater than he that is in the world.
5 Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza.
They are of the world, and for this reason they speak as of the world, and the world listens to them.
6 Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.
But you are of God. He who is beginning to know God listens to us; he who is not of God does not listen to us. By this we may distinguish the spirit of truth from the spirit of error.
7 Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
Beloved, let us love one another; for love is of God; and every one that loves us a child of God.
8 Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo.
He who does not love, does not know God; for God is love.
9 Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake.
In this was the love of God clearly shown toward us, by his sending his only Son into the world, so that we might live through him.
10 Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.
In this is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son to be a propitiation for our sins.
11 Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana.
If God so loved us, beloved, we also ought to love one another.
12 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
No man has ever gazed on God; but if we love one another, God ever abides in us, and his love is perfected in us.
13 Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake.
By this we come to know that we are abiding in him, and he in us, because he has given us of his Spirit;
14 Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu.
and we have beheld and do testify that the Father has sent the Son to be the Saviour of the world.
15 Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
If any man confesses that "Jesus is the Son of God." God is abiding in that man, and he in God.
16 Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu. Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake.
And we do know and have believed the love which God has for us. God is love; and he who is abiding in love is abiding in God, and God is abiding in him.
17 Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.
In this is love made perfect with us, so that we may have cheerful confidence in the Day of Judgment, because we are living in this world as He lives.
18 Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.
Fear does not exist in love; but love, when it is perfect, drives out fear. For fear has always torment, and he who has fear is not yet perfected in love.
19 Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza.
We love because He loved us first.
20 Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona?
If any one says, "I love God," and yet hates his brother, he is a liar; for he who does not love his brother whom he has seen, cannot possibly love God, whom he has not seen.
21 Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.
And we have this command from God. HE WHO LOVES GOD IS TO LOVE HIS BROTHER ALSO.

< 1 Yohana 4 >