< 1 Yohana 3 >
1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Vidite kakvu nam je ljubav dao otac, da se djeca Božija nazovemo i budemo; zato svijet ne poznaje nas, jer njega ne pozna.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Ljubazni! sad smo djeca Božija, i još se ne pokaza šta æemo biti; nego znamo da kad se pokaže, biæemo kao i on, jer æemo ga vidjeti kao što jest.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
I svaki koji ovaj nad ima na njega, èisti se, kao i on što je èist.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Svaki koji èini grijeh i bezakonje èini: i grijeh je bezakonje.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
I znate da se on javi da grijehe naše uzme; i grijeha u njemu nema.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Koji god u njemu stoji ne griješi; koji god griješi ne vidje ga niti ga pozna.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Djeèice! niko da vas ne vara: koji pravdu tvori pravednik je, kao što je on pravedan;
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
Koji tvori grijeh od ðavola je, jer ðavo griješi od poèetka. Zato se javi sin Božij da raskopa djela ðavolja.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Koji je god roðen od Boga ne èini grijeha, jer njegovo sjeme stoji u njemu, i ne može griješiti, jer je roðen od Boga.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
Po tom se poznaju djeca Božija i djeca ðavolja: koji god ne tvori pravde, nije od Boga, i koji ne ljubi brata svojega.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
Jer je ovo zapovijest, koju èuste ispoèetka, da ljubimo jedan drugoga.
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
Ne kao što Kain bješe od neèastivoga i zakla brata svojega. I za koji ga uzrok zakla? Jer djela njegova bijahu zla, a brata mu pravedna.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Ne èudite se, braæo moja, ako svijet mrzi na vas.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
Mi znamo da prijeðosmo iz smrti u život, jer ljubimo braæu; jer ko ne ljubi brata ostaje u smrti.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Svaki koji mrzi na brata svojega krvnik je ljudski; i znate da nijedan krvnik ljudski nema u sebi vjeènoga života. (aiōnios )
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
Po tom poznasmo ljubav što on za nas dušu svoju položi: mi smo dužni polagati duše za braæu.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
Koji dakle ima bogatstvo ovoga svijeta, i vidi brata svojega u nevolji i zatvori srce svoje od njega, kako ljubav Božija stoji u njemu?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
Djeèice moja! da se ne ljubimo rijeèju ni jezikom, nego djelom i istinom.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
I po tom doznajemo da smo od istine, i pred njim tješimo srca svoja.
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
Jer ako nam zazire srce naše, Bog je veæi od srca našega i zna sve.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Ljubazni! ako nam srce naše ne zazre, slobodu imamo pred Bogom;
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
I što god zaištemo, primiæemo od njega, jer zapovijesti njegove držimo i èinimo što je njemu ugodno.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
I ovo je zapovijest njegova da vjerujemo u ime sina njegova Isusa Hrista, i da ljubimo jedan drugoga kao što nam je dao zapovijest.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
I koji drži zapovijesti njegove u njemu stoji, i on u njemu. I po tom poznajemo da stoji u nama, po Duhu koga nam je dao.