< 1 Yohana 3 >

1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Voyez quel grand amour le Père nous a donné, pour que nous soyons appelés enfants de Dieu! C'est pourquoi le monde ne nous connaît pas, parce qu'il ne l'a pas connu.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Bien-aimés, maintenant nous sommes enfants de Dieu. Ce que nous serons n'a pas encore été révélé; mais nous savons que, lorsqu'il sera révélé, nous lui serons semblables, car nous le verrons tel qu'il est.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
Quiconque met cette espérance en lui se purifie, comme lui-même est pur.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Quiconque pèche commet aussi l'anarchie. Le péché est l'anarchie.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
Vous savez qu'il a été révélé pour ôter nos péchés, et qu'il n'y a pas de péché en lui.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Celui qui demeure en lui ne pèche pas. Celui qui pèche ne l'a pas vu et ne le connaît pas.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Petits enfants, que personne ne vous égare. Celui qui pratique la justice est juste, comme lui-même est juste.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
Celui qui pèche est du diable, car le diable a péché dès le commencement. C'est pour cela que le Fils de Dieu a été révélé, afin qu'il détruise les œuvres du diable.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Celui qui est né de Dieu ne commet pas de péché, car sa semence demeure en lui, et il ne peut pas pécher, puisqu'il est né de Dieu.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
C'est en cela que se révèlent les enfants de Dieu et les enfants du diable. Celui qui ne pratique pas la justice n'est pas de Dieu, ni celui qui n'aime pas son frère.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
Car c'est là le message que vous avez entendu dès le commencement, que nous devons nous aimer les uns les autres -
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
contrairement à Caïn, qui était du malin et qui tua son frère. Pourquoi l'a-t-il tué? Parce que ses actions étaient mauvaises, et que celles de son frère étaient justes.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Ne vous étonnez pas, mes frères, si le monde vous hait.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
Nous savons que nous sommes passés de la mort à la vie, parce que nous aimons les frères. Celui qui n'aime pas son frère demeure dans la mort.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
Celui qui hait son frère est un meurtrier, et vous savez qu'aucun meurtrier n'a la vie éternelle qui demeure en lui. (aiōnios g166)
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
A ceci nous connaissons l'amour, car il a donné sa vie pour nous. Et nous devons donner notre vie pour les frères.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
Mais quiconque possède les biens du monde et voit son frère dans le besoin, puis ferme contre lui son cœur de compassion, comment l'amour de Dieu demeure-t-il en lui?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
Mes petits enfants, n'aimons pas en paroles seulement, ni avec la langue seulement, mais en actes et en vérité.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
Et par là nous savons que nous sommes de la vérité et que nous persuadons nos cœurs devant lui,
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
car si notre cœur nous condamne, Dieu est plus grand que notre cœur, et il connaît toutes choses.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Bien-aimés, si notre cœur ne nous condamne pas, nous avons de l'assurance devant Dieu;
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
et tout ce que nous demandons, nous le recevons de lui, parce que nous gardons ses commandements et que nous faisons ce qui est agréable à ses yeux.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
Voici son commandement: que nous croyions au nom de son Fils, Jésus-Christ, et que nous nous aimions les uns les autres, comme il l'a ordonné.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
Celui qui garde ses commandements demeure en lui, et lui en lui. Nous savons par là qu'il demeure en nous, par l'Esprit qu'il nous a donné.

< 1 Yohana 3 >