< 1 Yohana 3 >
1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Behold then what manner of love the Father hath bestowed upon us, that we should be called the children of God: though for this reason the world knoweth us not, because it knew not Him.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, we are now the children of God, but it doth not yet appear what we shall be: we know however, that, when He shall appear, we shall be like Him; for we shall see Him as He is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
And every one, that hath this hope in Him, purifieth himself, even as He is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Every one that committeth sin, transgresseth the law; for sin is the violation of the law.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
And ye know that He was manifested, to take away our sins: and in Him there is no sin.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Whosoever abideth in Him sinneth not: whosoever sinneth hath not seen Him, nor known Him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Little children, let no one deceive you: he that practiseth righteousness is righteous, even as He is righteous:
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
he, that makes a practise of sin, is of the devil; for the devil sinneth from the beginning. And for this the Son of God was manifested, that He might destroy the works of the devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Whosoever is born of God doth not practise sin, because his seed remaineth in him: and he cannot sin, because he is born of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
In this the children of God are manifest, and the children of the devil: whosoever doth not practise righteousness, and he who loveth not his brother, is not of God:
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
for this is the injunction which ye heard from the beginning, that we should love one another: not as Cain who was of the evil one, and slew his brother;
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
and why did he slay him? because his own works were evil, and his brother's righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Wonder not then, my brethren, if the world hate you:
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
since we know that we have passed from death to life, because we love the brethren: he, that loveth not his brother, remaineth in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Whosoever hateth his brother is a murderer: and ye know that no murderer hath eternal life abiding in him. (aiōnios )
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
In this we know his love, that He laid down his life for us: and we should be ready to lay down our lives for the brethren.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
But if any one, who hath the good things of the world, seeth his brother in want, and shutteth up his bowels from him, how dwelleth the love of God in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My little children, let us not love in word, or in tongue only, but in deed and in truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
And hereby we know that we are of the truth, and shall assure our hearts before Him.
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
For, if our heart condemn us, God is still greater than our heart, and knoweth all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our heart condemn us not, then have we confidence towards God:
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
and whatsoever we ask, we receive from Him, because we keep his commandments, and do the things that are pleasing in his sight.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
And this is his commandment, that we should believe in the name of his Son Jesus Christ, and love one another, as He hath given us a charge to do.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
And he, that keepeth his commandments, abideth in Him, and He in him: and hereby we know that He abideth in us, even by the Spirit which He hath given us.