< 1 Yohana 3 >
1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
See what kind of love the Father has given to us, that we should be called children of God, and this is what we are. For this reason, the world does not know us, because it did not know him.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, we are now children of God, and it has not yet been revealed what we will be. We know that when Christ appears, we will be like him, for we will see him just as he is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
Everyone who has this hope fixed on him purifies himself just as he is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Everyone who sins is committing acts of lawlessness, for sin is lawlessness.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
You know that Christ was revealed in order to take away sins, and in him there is no sin.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
No one who remains in him will keep on sinning. No one who continues to sin has seen him or known him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Dear children, do not let anyone lead you astray. The one who does righteousness is righteous, just as Christ is righteous.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
The one who commits sin is from the devil, for the devil has sinned from the beginning. For this reason the Son of God was revealed, so that he would destroy the devil's works.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Whoever has been born from God does not continue to sin because God's seed remains in him. He cannot continue to sin because he has been born of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
In this the children of God and children of the devil are revealed: Whoever does not do what is righteous is not from God, neither is the one who does not love his brother.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
For this is the message that you have heard from the beginning: We should love one another.
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
We should not be like Cain, who was from the evil one and murdered his brother. Why did he kill him? Because his works were evil and his brother's righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Do not be amazed, my brothers, if the world hates you.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
We know that we have passed out of death into life, because we love the brothers. Anyone who does not love remains in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Anyone who hates his brother is a murderer. You know that no murderer has eternal life residing in him. (aiōnios )
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
By this we know love, because Christ laid down his life for us. We also ought to lay down our lives for the brothers.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
But whoever has the world's goods, sees his brother in need, and shuts up his heart of compassion from him, how does the love of God remain in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My dear children, let us not love in word nor in tongue, but in actions and truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
It is by this we know that we are from the truth, and we assure our hearts before him.
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
For if our hearts condemn us, God is greater than our hearts, and he knows all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our hearts do not condemn us, we have confidence toward God.
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
Whatever we ask we will receive from him, because we keep his commandments and do the things that are pleasing before him.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
This is his commandment: that we should believe in the name of his Son Jesus Christ and love one another, just as he gave us this commandment.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
The one who keeps God's commandments remains in him, and God remains in him. By this we know that he remains in us, by the Spirit whom he gave to us.