< 1 Yohana 3 >

1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
See what great love the Father has lavished upon us, that we should be called children of God! The reason the world does not know you is that it did not know him.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, now we are children of God, and what we will be has not yet been revealed. But we know that when he appears, we will be like him, because we will see him as he is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
Everyone who places this hope in him purifies himself, just as he is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Everyone who practices sin also practices lawlessness; sin is lawlessness.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
But you know that he appeared in order to take away our sins, and in him there is no sin.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
No one who abides in him continues in sin; no one who continues in sin has either seen him or known him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Little children, let no one deceive you. Whoever practices righteousness is righteous, just as he is righteous.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
Whoever practices sin is of the devil, for the devil has been sinning from the beginning. The reason the Son of God appeared was to destroy the works of the devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
No one who has been born of God continues in sin, because God's seed abides in him; he cannot continue in sin, because he has been born of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
By this the children of God and the children of the devil are revealed: Anyone who does not practice righteousness is not of God, nor is anyone who does not love his brother.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
For this is the message you have heard from the beginning, that we should love one another.
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
We should not be like Cain, who was of the evil one and murdered his brother. And why did he murder him? Because his own deeds were evil, but the deeds of his brother were righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Do not be surprised, my brothers, if the world hates you.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
We know that we have passed from death to life because we love our brothers. Whoever does not love his brother abides in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
Anyone who hates his brother is a murderer, and you know that no murderer has eternal life abiding in him. (aiōnios g166)
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
By this we know love, that he laid down his life for us. And we ought to lay down our lives for our brothers.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
If anyone has the world's goods and sees his brother in need but closes his heart against him, how does the love of God abide in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My little children, let us not love in word or speech, but in deed and truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
By this we know that we are of the truth and can reassure our hearts before him:
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
If our hearts condemn us, God is greater than our hearts and knows all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our hearts do not condemn us, we have confidence before God
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
and receive from him whatever we ask, because we keep his commandments and do what is pleasing in his sight.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
And this is his commandment, that we believe in the name of his Son Jesus Christ and love one another, just as he commanded.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
Whoever keeps his commandments abides in God, and God abides in him. And we know that he abides in us because of the Spirit he has given us.

< 1 Yohana 3 >