< 1 Yohana 3 >
1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Behold what manner of love the Father hath bestowed upon us, that we should be called children of God l For this cause the world knoweth us not, because it knew him not.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, now are we children of God, and it hath not yet been manifested what we shall be. We know that, when it shall be manifested, we shall be like him; because we shall see him as he is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
And every one that hath this hope in Him purifieth himself, even as He is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Whoever committeth sin transgresseth thereby the law; for sin is a transgression of the law.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
And ye know that he was manifested to take away sins; and in him is no sin.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Whoever abideth in him sinneth not; whoever sinneth hath not seen him, nor known him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
My children, let no one deceive you; he that doeth righteousness is righteous, even as he is righteous.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
He that committeth sin is of the Devil; for the Devil sinneth from the beginning. For this purpose the Son of God was manifested, that he might destroy the works of the Devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Whoever hath been born of God doth not commit sin, because his seed abideth in him; and he cannot sin, because he hath been born of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
In this are manifest the children of God and the children of the Devil. Whoever doeth not righteousness is not of God, and he that loveth not his brother.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
For this is the message that ye have heard from the beginning, that we should love one another;
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
not as Cain was of the Evil One, and slew his brother. And wherefore did he slay him? Because his own works were evil, and his brother's righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Wonder not, brethren, if the world hateth you.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
We know that we have passed out of death into life, because we love the brethren; he that loveth not abideth in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Whoever hateth his brother is a murderer; and ye know that no murderer hath everlasting life abiding in him. (aiōnios )
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
Herein we know love, in that he laid down his life for us; and we ought to lay down our lives for the brethren.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
But whoever hath this world's goods, and seeth his brother having need, and shutteth up his compassion from him, how dwelleth the love of God in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My children, let us not love in word, nor in tongue, but in deed and in truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
And hereby we know that we are of the truth, and shall assure our hearts before him;
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
because if our heart condemn us, God is greater than our heart, and knoweth all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our heart condemn us not, we have confidence toward God;
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
and whatever we ask, we receive of him, because we keep his commandments, and do the things that are pleasing in his sight.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
And this is his commandment, that we should believe in the name of his Son Jesus Christ, and should love one another, as he gave commandment.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
And he that keepeth his commandments abideth in him, and he in him; and hereby we know that he abideth in us, by the Spirit, which he gave us.