< 1 Yohana 3 >

1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
See how great a sincere love the Father has given us, that we should be called children of God! Because the world didn’t know Him, it doesn’t know us.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, now we are children of God, and it hasn’t yet appeared what we will be. We know that when He appears we will be like Him, because we will see Him just as He is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
Everyone who has this hope fixed on Him purifies himself, just as He is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Everyone who practices sin also practices lawlessness. Sin is lawlessness.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
You know that He appeared to take away sins. There is no sin in Him.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
No one who lives in Him sins. No one who sins has seen Him or knows Him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Little children, don’t let anybody deceive you. The one who practices righteousness is righteous, just as He is righteous.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
The one who practices sin is the Devil’s, because the Devil has sinned from the beginning. The Son of God appeared for this purpose, that He might destroy the works of the Devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
No one who is born of God practices sin, because God’s seed lives in him. He can’t continue to sin, because he is born of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
By this the children of God and the children of the Devil are obvious: anyone who doesn’t practice righteousness is not God’s, and neither is anyone who doesn’t sincerely love his brother or sister.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
For this is the message that you have heard from the beginning, that we should sincerely love one another.
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
Don’t be like Cain, who belonged to the evil one, and killed his brother. Why did he kill him? Because Cain’s deeds were evil, and his brother’s were righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Don’t be surprised, brothers and sisters, if the world hates you.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
We know that we have passed out of death into life, because we sincerely love our brothers and sisters. Whoever doesn’t sincerely love lives in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
Whoever hates his brother or sister is a murderer, and you know that no murderer has eternal life living in him. (aiōnios g166)
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
By this we know God’s sincere love, because He laid down His life for us. So we also ought to lay down our lives for our brothers and sisters.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
If someone has this world’s goods, and sees a brother in need, and closes up his heart of compassion from him, how does God’s sincere love live in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My little children, let’s not sincerely love just in words or in language, but in deed and in truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
This is how we will know that we belong to the truth, and how we will assure our hearts before Him
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
whenever our hearts condemn us; for God is greater than our hearts, and He knows all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our hearts don’t condemn us, we have confidence before God;
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
and we receive from Him whatever we ask, because we keep His commandments and do the things that please Him.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
This is His commandment, that we believe in the name of His Son, Jesus Christ, and that we sincerely love one another, just as He commanded us.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
Whoever keeps His commandments lives in Him, and He lives in that person. This is how we know that He lives in us: by the Spirit He has given us.

< 1 Yohana 3 >