< 1 Yohana 3 >
1 Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Behold, how great love the Father has bestowed on us, that we should be called the children of God! For this reason, the world knows us not, because it knew him not.
2 Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Beloved, now are we the children of God, and it does not yet appear what we shall be: but we know that, when he shall appear, we shall be like him; for we shall see him as he is.
3 Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
And every one that has this hope in Him purifies himself, even as He is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi.
Every one that works sin, works also transgression of law: and sin is transgression of law.
5 Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi.
And you know that he was manifested, that he might take away our sins; and in him there is no sin.
6 Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Whoever abides in him, sins not. Whoever sins, has neither seen him nor known him.
7 Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki.
Little children, let no one deceive you: he that works righteousness is righteous, even as he is righteous.
8 Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi.
He that works sin is of the devil, for the devil sins from the beginning: for this purpose was the son of God manifested, that he might destroy the works of the devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Whoever has been begotten of God does not work sin; because his seed remains in him: and he can not sin, because he has been begotten of God.
10 Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
By this the children of God are manifest, and the children of the devil. Whoever does not work righteousness is not of God; neither is he that loves not his brother.
11 Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi.
For this is the message that you have heard from the beginning, that we should love one another.
12 Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
Not as Cain, who was of the wicked one, and slew his brother: and for what reason did he slay him? because his own works were evil, and his brother’s, righteous.
13 Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia.
Wonder not, my brethren, if the world hates you.
14 Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini.
We know that we have passed from death to life, because we love the brethren: he that loves not his brother, abides in death.
15 Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Whoever hates his brother, is a murderer: and you know that no murderer has eternal life abiding in him. (aiōnios )
16 Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu.
By this we know the love of Christ, because he laid down his life for us: and we ought to lay down our lives for the brethren.
17 Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo?
Whoever has this world’s goods, and sees his brother have need, and shuts his heart against him, how dwells the love of God in him?
18 Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli.
My little children, let us not love in word, nor in tongue, but in deed, and in truth.
19 Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu
And by this we know that we are of the truth; and we shall have our hearts at rest before him:
20 kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
for if our heart condemn us, we know that God is greater than our heart, and knows all things.
21 Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu,
Beloved, if our heart condemn us not, we have confidence toward God,
22 lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza.
and whatever we ask, we receive from him, because we keep his commandments, and do the things that are pleasing in his sight.
23 Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru.
And this is his commandment: That we should believe on the name of his Son Jesus Christ, and love one another, as he gave us commandment.
24 Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
And he that keeps his commandments abides in him, and he in him. And by this we know that he abides in us, by the Spirit which he has given us.