< 1 Yohana 2 >
1 Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki.
Ami laga bacha khan, moi tumikhan ke etu likhi ase tumikhan paap nokorile nimite. Kintu jodi kunba paap kore, amikhan laga Baba Isor logote kotha kori diya ekjon ase, Jisu Khrista, kun dharmik ase.
2 Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
Tai amikhan laga paap maph kori diya ekjon ase, aru khali amikhan ekla nimite nohoi, kintu pura duniya nimite.
3 Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
Etu pora amikhan Taike jani loise, jodi amikhan Tai laga adesh khan mani kene thake koile.
4 Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
Kun manu koi, “Moi Isor ke jane,” kintu kotha mani kene nathake, tai misa kowa manu ase, aru tai logote hosa nai.
5 Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
Kintu kun manu Isor laga kotha mane, tai logot te Isor laga morom to sob phale bhal bonai dise. Etu pora amikhan jane amikhan Tai logote ase:
6 Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
kun manu tai Isor logote ase koi, Khrista jineka beraise, etu nisena tai bhi bera bole lage.
7 Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
Morom laga bhai khan, moi tumikhan ke notun niyom likha nohoi, hoilebi kuntu purana niyom tumikhan logote shuru pora ase, etu he koi ase. Etu purana niyom he tumikhan huni thaka laga kotha ase.
8 Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.
Hoilebi moi tumikhan nimite notun niyom likhi di ase, juntu niyom Khrista aru tumikhan usorte hosa ase, kelemane andhera to jai ase, aru hosa laga puhor to juli ase.
9 Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
Kun manu ujala te ase eneka koi, aru nijor laga bhai bhoini khan ke ghin kore, tai etiya bhi andhera te ase.
10 Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
Kun manu tai laga bhai ke morom kore tai ujala te ase aru tai kitia bhi biya rasta te nagiribo.
11 Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
Kintu kun manu tai laga bhai ke ghin kore tai andhera te ase aru andhera te berai ase. Tai kote jai ase tai nijor bhi najane, kelemane andhera pora tai laga suku andha kori dise.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
Moi tumikhan ke likhi ase, morom laga bacha khan, kelemane Khrista laga naam pora tumikhan laga paap maph paise.
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
Moi apuni khan ke likhi ase, baba khan, kelemane apuni khan jane utu ekjon kun ase, jun shuru pora ase. Moi tumikhan nimite likhi ase, jawan manu khan, kelemane tumikhan biya ekjon logote jiti loise.
14 Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Moi tumikhan ke likhi dise, chutu bacha khan, kelemane tumikhan Baba Isor ke jane. Moi etu apuni khan ke likhise, baba khan, kelemane apuni khan jane etu ekjon ke kun shuru pora ase. Moi tumikhan ke likhise, jawan manu khan, kelemane tumikhan takot ase, aru Isor laga kotha tumikhan logote ase, aru tumikhan biya uporte jiti loise.
15 Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Etu duniya ke morom nokoribi aru etu duniya te thaka jinis khan ke morom nokoribi. Jodi kunba manu etu duniya ke morom kore, titia tai logote Baba Isor laga morom nai.
16 Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
Kelemane ki to etu duniya te ase- mangso laga itcha, aru suku laga itcha, aru jibon laga phutani- etu Baba pora nohoi kintu etu duniya laga ase.
17 Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn )
Etu duniya aru tai laga itcha khan khotom hoi ase. Kintu kun manu Isor laga itcha pora thake tai hodai thakibo. (aiōn )
18 Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
Chutu bacha khan, etu hekh laga homoi ase. Tumikhan Khrista bhirodhi ahi ase koi kene hunise, aru etiya to bisi Khrista bhirodhi jon ahi jaise. Etu pora amikhan jane hekh homoi to ahise.
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
Khrista ke bhirodh kora khan to amikhan pora ulaikene jaise, kintu taikhan to amikhan pora nohoi. Jodi taikhan to amikhan pora ase koile amikhan logote thaki bole asele. Kintu jitia taikhan ulaikene jaise, etu pora jani loise taikhan kun bhi amikhan pora nohoi.
20 Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
Kintu tumikhan Pobitro Ekjon pora asirbad paise, aru tumikhan sob hosa jani ase.
21 Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli.
Moi tumikhan hosa najane koi kene etu likha nai, kintu tumikhan jani ase aru hosa te eku misa nai.
22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana.
Kun misa kowa jon ase, tai ekjon, jun pora Jisu he Khrista ase koi kene mana kore? Etu manu Khrista bhirodhi ase, kelemane tai Baba aru Putro ke mana kori ase.
23 Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
Kun manu Jisu ke mana kore tai laga Baba nai. Kun manu Jisu ke loi, tai logote Baba ase.
24 Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
Aru tumikhan to, shuru pora ki kotha hunise etu tumikhan logote thaki bole dibi. Jodi tumikhan shuru pora ki hunise etu monte rakhe koile, tumikhan hodai Putro aru Baba logote thakibo.
25 Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios )
Etu kosom Khrista pora amikhan ke dise- anonto jibon. (aiōnios )
26 Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
Moi etu kotha tumikhan nimite likhi ase, utu manu karone bhi kun pora tumikhan ke biya rasta te loijabo.
27 Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
Aru tumikhan to, ki asirbad tumikhan Khrista pora paise etu tumikhan logote he ase, aru dusra pora tumikhan ke sikhai dibole dorkar nai. Kintu Tai laga asirbad pora ki sikhai dise etu hosa ase aru misa nohoi, aru tumikhan ke sikhai diya nisena, Tai logote thakibi.
28 Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
Etiya, bacha khan, Tai logote thakibi, jitia Tai wapas ahibo, moi khan mon dangor koribo aru Tai aha homoi te sorom nakhabo.
29 Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.
Jodi tumi jane Tai dharmik ase koi kene, titia hoile tumikhan etu bhi jani thakibo kun manu thik kaam kore tai Isor pora jonom hoise.