< 1 Yohana 2 >

1 Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki.
My children, these things I write to you, that ye sin not. But if any one should sin, we have an Advocate with the Father, Jesus the Messiah, the righteous.
2 Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
For he is himself the propitiation for our sins; and not for ours only, but also for all the world.
3 Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
And by this we shall be sensible that we know him, if we keep his commandments.
4 Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
For he that saith, I know him, and doth not keep his commandments, is a liar, and the truth is not in him.
5 Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
But he that keepeth his word, in him is the love of God truly completed: for by this we know that we are in him.
6 Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
He that saith, I am in him, is bound to walk according to his walkings.
7 Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
My beloved, I write no new commandment to you, but the old commandment which ye had from the beginning; and the old commandment is the word, which ye have heard.
8 Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.
Again, a new commandment I write to you, which is true in him and in you; because the darkness hath passed away, and the true light beginneth to appear.
9 Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
Whoever therefore shall say that he is in the light, and hateth his brother, is in darkness until now.
10 Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
He that loveth his brother, abideth in the light, and in him is no stumbling.
11 Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
But he that hateth his brother, is in darkness, and walketh in darkness; and he knoweth not whither he goeth, because the darkness hath blinded his eyes.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
I write to you, ye children, because your sins are forgiven you for his name's sake.
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
I write to you, ye fathers, because ye have known him who existed from the beginning. I write to you, ye young men, because ye have vanquished the evil one.
14 Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
I have written to you, ye little ones, because ye have known the Father. I have written to you, ye fathers, because ye have known him who was from the beginning, I have written to you, ye young men, because ye are strong, and the word of God dwelleth in you, and ye have vanquished the evil one.
15 Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Love not the world, nor any thing in it; for whoever loveth the world, hath not the love of the Father in him.
16 Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
For all that is in the world, is, the lust of the body, and the lust of the eyes, and the pride of the world; which are not from the Father, but from the world itself.
17 Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn g165)
And the world is passing away, both it and the lust thereof; but he that doeth the pleasure of God, abideth for ever. (aiōn g165)
18 Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
My children, it is the latter time; and as ye have heard that a false Messiah was to arise, so there are now many false Messiahs; and from this we know that it is the latter time.
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
From us they went out, but they were not of us; for if they had been of us, they would have continued with us: but they went out from us, that so it might be known, that they were not of us.
20 Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
But ye have an unction from the Holy One; and ye discriminate every person.
21 Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli.
I have not written to you, because ye know not the truth, but because ye know it, and because no falsehood is of the truth.
22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana.
Who is false, but he that denieth that Jesus is the Messiah? And that person is a false Messiah. He that denieth the Father, denieth also the Son.
23 Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
And he that denieth the Son, also believeth not the Father. He that confesseth the Son, confesseth also the Father.
24 Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
And what ye heard from the first, let that remain with you. For if that, which ye heard from the first, remaineth with you, ye also will remain in the Father and in the Son.
25 Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios g166)
And this is the promise, which he hath promised us, even life eternal. (aiōnios g166)
26 Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
And these things I have written to you, on account of those who seduce you.
27 Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
And ye also, if the unction which ye have received from him remaineth in you, need not that any one should teach you; but as that unction is from God, it teacheth you all things; and it is true, and no falsehood is in it. And as it hath taught you, remain ye in him.
28 Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
And now, my children, remain ye in him; that so, when he shall be manifested, we may not be ashamed before him, but may have an open countenance at his coming.
29 Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.
If ye know that he is righteous, ye also know, that whoever doeth righteousness, is from him.

< 1 Yohana 2 >