< 1 Yohana 2 >

1 Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki.
My little children, these things write I unto you, that ye may not sin. And if any man sin, we have an Advocate with the Father, Jesus Christ the righteous:
2 Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
and he is the propitiation for our sins; and not for ours only, but also for the whole world.
3 Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
And hereby know we that we know him, if we keep his commandments.
4 Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
He that saith, I know him, and keepeth not his commandments, is a liar, and the truth is not in him:
5 Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
but whoso keepeth his word, in him verily hath the love of God been perfected. Hereby know we that we are in him:
6 Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
he that saith he abideth in him ought himself also to walk even as he walked.
7 Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
Beloved, no new commandment write I unto you, but an old commandment which ye had from the beginning: the old commandment is the word which ye heard.
8 Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.
Again, a new commandment write I unto you, which thing is true in him and in you; because the darkness is passing away, and the true light already shineth.
9 Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
He that saith he is in the light, and hateth his brother, is in the darkness even until now.
10 Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
He that loveth his brother abideth in the light, and there is none occasion of stumbling in him.
11 Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
But he that hateth his brother is in the darkness, and walketh in the darkness, and knoweth not whither he goeth, because the darkness hath blinded his eyes.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
I write unto you, [my] little children, because your sins are forgiven you for his name’s sake.
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
I write unto you, fathers, because ye know him which is from the beginning. I write unto you, young men, because ye have overcome the evil one. I have written unto you, little children, because ye know the Father.
14 Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
I have written unto you, fathers, because ye know him which is from the beginning. I have written unto you, young men, because ye are strong, and the word of God abideth in you, and ye have overcome the evil one.
15 Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Love not the world, neither the things that are in the world. If any man love the world, the love of the Father is not in him.
16 Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
For all that is in the world, the lust of the flesh, and the lust of the eyes, and the vainglory of life, is not of the Father, but is of the world.
17 Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn g165)
And the world passeth away, and the lust thereof: but he that doeth the will of God abideth for ever. (aiōn g165)
18 Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
Little children, it is the last hour: and as ye heard that antichrist cometh, even now have there arisen many antichrists; whereby we know that it is the last hour.
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
They went out from us, but they were not of us; for if they had been of us, they would have continued with us: but [they went out], that they might be made manifest how that they all are not of us.
20 Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
And ye have an anointing from the Holy One, and ye know all things.
21 Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli.
I have not written unto you because ye know not the truth, but because ye know it, and because no lie is of the truth.
22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana.
Who is the liar but he that denieth that Jesus is the Christ? This is the antichrist, [even] he that denieth the Father and the Son.
23 Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
Whosoever denieth the Son, the same hath not the Father: he that confesseth the Son hath the Father also.
24 Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
As for you, let that abide in you which ye heard from the beginning. If that which ye heard from the beginning abide in you, ye also shall abide in the Son, and in the Father.
25 Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios g166)
And this is the promise which he promised us, [even] the life eternal. (aiōnios g166)
26 Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
These things have I written unto you concerning them that would lead you astray.
27 Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
And as for you, the anointing which ye received of him abideth in you, and ye need not that any one teach you; but as his anointing teacheth you concerning all things, and is true, and is no lie, and even as it taught you, ye abide in him.
28 Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
And now, [my] little children, abide in him; that, if he shall be manifested, we may have boldness, and not be ashamed before him at his coming.
29 Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.
If ye know that he is righteous, ye know that every one also that doeth righteousness is begotten of him.

< 1 Yohana 2 >