< 1 Yohana 2 >

1 Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki.
My children, these things I write to you, that ye may not sin. And if any one have sinned, we have an advocate with the Father, Jesus Christ the righteous.
2 Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
And he is a propitiation for our sins; and not for ours only, but also for the whole world.
3 Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
And hereby we know that we know him, if we keep his commandments.
4 Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
He that saith, I know him, and keepeth not his commandments, is a liar, and the truth is not in him.
5 Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
But whoever keepeth his word, truly in him is the love of God perfected. Hereby we know that we are in him.
6 Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
He that saith he abideth in him ought himself also so to walk, even as he walked.
7 Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
Beloved, I write no new commandment to you, but an old commandment, which ye have had from the beginning. The old commandment is the word which ye have heard.
8 Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.
Again, a new commandment I write to you, which thing is true in him, and in you; because the darkness is passing away, and the true light now shineth.
9 Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
He that saith he is in the light, and hateth his brother, is in the darkness until now.
10 Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
He that loveth his brother abideth in the light, and there is no occasion of stumbling in him;
11 Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
but he that hateth his brother is in the darkness, and walketh in the darkness, and knoweth not whither he goeth, because the darkness hath blinded his eyes.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
I write to you, my children, because your sins have been forgiven you for his name's sake.
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
I write to you, fathers, because ye know him that was from the beginning. I write to you, young men, because ye have overcome the Evil One. I have written to you, my children, because ye know the Father.
14 Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
I have written to you, fathers, because ye know him that was from the beginning. I have written to you, young men, because ye are strong, and the word of God abideth in you, and ye have overcome the Evil One.
15 Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Love not the world, nor the things in the world. If any one loveth the world, the love of the Father is not in him;
16 Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
because all that is in the world, the lust of the flesh, and the lust of the eyes, and the pride of life, is not of the Father, but is of the world.
17 Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn g165)
And the world is passing away, and the lust thereof; but he that doeth the will of God abideth for ever. (aiōn g165)
18 Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
My children, the last time is come; and as ye have heard that Antichrist is coming, even now there are many antichrists; whereby we know that the last time is come.
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
They went out from us, but they were not of us; for if they had been of us, they would have remained with us; but they went out, that they might be made manifest that they are not all of us.
20 Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
And ye have an anointing from the Holy One, and know all things.
21 Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli.
I have not written to you because ye know not the truth, but because ye know it, and that no lie is of the truth.
22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana.
Who is the liar, but he that denieth that Jesus is the Christ? This is the antichrist, who denieth the Father and the Son.
23 Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
Whoever denieth the Son, the same hath not the Father; he that acknowledgeth the Son hath also the Father.
24 Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
As for you, let that which ye have heard from the beginning abide in you. If that which ye have heard from the beginning shall abide in you, ye also will abide in the Son, and in the Father.
25 Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios g166)
And this is the promise which he himself promised us, even the life everlasting. (aiōnios g166)
26 Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
These things I have written to you concerning those who seduce you.
27 Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
And the anointing which ye yourselves received from him abideth in you, and ye have no need that any one teach you; but as his anointing teacheth you concerning all things, and is truth, and is not a lie, even as it hath taught you, ye shall abide in him.
28 Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
And now, my children, abide in him; that when he shall appear, we may have confidence, and not be ashamed before him at his coming.
29 Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.
If ye know that he is righteous, ye know that every one also that doeth righteousness hath been born of him.

< 1 Yohana 2 >