< 1 Yohana 1 >

1 Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
That which was from the beginning, that which we have heard, that which we have seen with our eyes, that which we beheld, and our hands handled, concerning the Word of Life—
2 Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios g166)
and the Life appeared, and we have seen, and testify, and declare to you the continuous Life, which was with the Father, and was revealed to us— (aiōnios g166)
3 Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo.
we declare to you that which we have seen and heard, that you also may have fellowship with us, and our fellowship [is] with the Father, and with His Son Jesus Christ;
4 Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
and these things we write to you, that your joy may be full.
5 Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
And this is the message that we have heard from Him, and announce to you, that God is light, and darkness is not in Him at all;
6 Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
if we may say, “We have fellowship with Him,” and may walk in the darkness—we lie, and do not [speak] the truth;
7 Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
and if we may walk in the light, as He is in the light—we have fellowship with one another, and the blood of His Son Jesus Christ cleanses us from every sin;
8 Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
if we may say, “We have no sin,” we lead ourselves astray, and the truth is not in us;
9 Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote.
if we may confess our sins, He is steadfast and righteous that He may forgive us the sins, and may cleanse us from every unrighteousness;
10 Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.
if we may say, “We have not sinned,” we make Him a liar, and His word is not in us.

< 1 Yohana 1 >