< 1 Wakorintho 1 >
1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
Павел, покликаний апостол Ісуса Христа, волею Божою, та Состен брат,
2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
церкві Божій в Коринтї, осьвяченим в Ісусї Христї, покликаним сьвятим, з усїма, которі призивають імя Господа нашого Ісуса Христа, на всякому місці, у них і в нас:
3 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
благодать вам і впокій од Бога, Отця нашого, і Господа Ісуса Христа.
4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
Дякую Богу моєму всякого часу за вас про благодать Божу, дану вам в Христї Ісусї,
5 Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
тим, що у всьому ви збагатились ним у всякім слові і всякім знанню,
6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
яко ж сьвідченнє Христове утверджено в вас,
7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
так що ви не маєте недостатку нї в однім даруванню, дожидаючись одкриття Господа нашого Ісуса Христа,
8 Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
котрий і утвердить вас до кінця, щоб ви були невинуваті в день Господа нашого Ісуса Христа.
9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
Вірен бо Бог, через котрого покликані ви в общеннє Сина Його, Ісуса Хрнста, Господа нашого.
10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
Благаю ж вас, браттє, імям Господа нашого Ісуса Христа, щоб те саме говорили ви всі, і щоб не було між вами розділення, а щоб були з'єднані в одному розумінню і в одній мислі.
11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
Звіщено бо менї про вас, браттє моє, від Хлоїних, що між вами єсть незгодини.
12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
Кажу ж про те, що кожен з вас говорить: Я Павлів; а я Аполосів; а я КиФіїн; а я Христів.
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Хиба поділивсь Христос? хиба Павла розпято за вас? або в імя Павлове хрестились ви?
14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
Дякую Богові, що я нікого з вас не охрестив, тільки Криспа та Гая,
15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
щоб хто не сказав, що в імя моє я охрестив.
16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
Хрестив же я й СтеФанів дім; більш не знаю, чи кого другого хрестив.
17 Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
Не послав бо мене Христос хрестити, а благовістити, не в премудрости слова, щоб не опустїв хрест Христів.
18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
Слово бо про хрест погибаючим дурощі, нам же, що спасаємось, сила Божа.
19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
Писано бо: Погублю премудрість премудрих, і розум розумних відкину.
20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn )
Де мудрець? де письменник? де дослїджуватель віку сього? Чи не обернув Бог премудрість сьвіта сього в дурощі? (aiōn )
21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
Коли бо у премудрості Божій не пізнав сьвіт Бога премудростю, то зводив Бог дурощами проповіді спасти віруючих.
22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
Коли і Жиди ознак доповняють ся, і Греки премудростї шукають,
23 Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
ми проповідуємо Христа рознятого, Жидам поблазнь, Грекам же дурощі,
24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
самим же покликаним, і Жидам і Грекам, Божу силу й Божу премудрість:
25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
тим що немудре Боже мудріще від людей, а неміцне Боже кріпше людей.
26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
Спогляньте бо на покликаннє ваше, браттє, що небагато (між вами) премудрих по тїлу, небагато сильних, небагато благородних;
27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
ні, немудре сьвіїа вибрав Бог, щоб осоромити премудрих, і безсильне сьвіта вибрав Бог, щоб осоромити потужне,
28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
і незначне сьвіту і погорджене вибрав Бог, і те чого нема, щоб те, що є, в нїщо обернути,
29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
щоб не велсчалось нїяке тїло перед Ним.
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
З Него ж і ви в Христї Ісусї, що став ся нам премудростю від Бога, і праведностю, і освяченнєм, і викупленнєм,
31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
щоб, яко ж писано: Хто хвалить ся, в Господі хвалив ся.