< 1 Wakorintho 6 >

1 Kama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu?
Doth any one of you, who hath a matter against another, dare to go to law before the unrighteous, and not before the holy?
2 Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo?
Or do ye not know, that the holy will judge the world? And if the world is to be judged by you, are ye unworthy to judge in causes of the least importance?
3 Hamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya?
Know ye not, that we shall pass judgment upon angels? How much more, concerning affairs of this life?
4 Kwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, chagueni kuwa waamuzi, watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kanisa.
If then ye have any causes relating to this life, set them to judge who are of no repute in the church.
5 Nasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waaminio?
I speak to your shame. Is it so, that there is not a wise man among you, not one that will be able to judge between his brethren?
6 Badala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!
Nay, brother goeth to law with brother, and that before unbelievers.
7 Huko kuwa na mashtaka miongoni mwenu ina maana kwamba tayari ni kushindwa kabisa. Kwa nini msikubali kutendewa mabaya? Kwa nini msikubali kunyangʼanywa?
Now therefore it is altogether an evil among you, that ye have suits against each other. Why do ye not rather submit to wrong? Why do ye not rather allow yourselves to be defrauded?
8 Badala yake, ninyi wenyewe mwadanganya na kutenda mabaya, tena mwawatendea ndugu zenu.
But ye yourselves wrong, and defraud, and that too your brethren.
9 Je, hamjui kwamba wasio haki hawataurithi Ufalme wa Mungu? Msidanganyike: Waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wahanithi, wala walawiti,
Know ye not, that wrongdoers shall not inherit the kingdom of God? Be not deceived; neither fornicators, nor idolaters, nor adulterers, nor the effeminate, nor abusers of themselves with mankind,
10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyangʼanyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.
nor thieves, nor the covetous, nor drunkards, nor revilers, nor extortioners, shall inherit the kingdom of God.
11 Baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Yesu Kristo na katika Roho wa Mungu wetu.
And such were some of you; but ye were washed, but ye were made holy, but ye were accepted as righteous in the name of the Lord Jesus, and in the Spirit of our God.
12 “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini si vitu vyote vyenye faida. “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini sitatawaliwa na kitu chochote.
All things are lawful for me, but all things are not profitable; all things are lawful for me, but I will not be brought under the power of anything.
13 “Chakula ni cha tumbo, na tumbo ni la chakula”: lakini Mungu ataviangamiza vyote viwili. Mwili haukuumbwa kwa ajili ya zinaa bali kwa ajili ya Bwana na Bwana kwa ajili ya mwili.
Meats are for the stomach, and the stomach for meats; but God will make an end of both it and them. But the body is not for fornication, but for the Lord, and the Lord for the body;
14 Naye Mungu aliyemfufua Bwana kutoka kwa wafu atatufufua sisi pia kwa uweza wake.
and God both raised up the Lord, and will also raise up us by his power.
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo mwenyewe? Je, nichukue viungo vya mwili wa Kristo na kuviunganisha na mwili wa kahaba? La hasha!
Know ye not, that your bodies are members of Christ? Shall I then take the members of Christ, and make them members of a harlot? God forbid!
16 Hamjui kwamba aliyeungwa na kahaba anakuwa mwili mmoja naye? Kwa kuwa imenenwa, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
Know ye not, that he who is connected with a harlot is one body with her? “For the two,” saith he, “shall become one flesh;”
17 Lakini mtu aliyeungwa na Bwana anakuwa roho moja naye.
but he that is connected with the Lord is one spirit with him.
18 Ikimbieni zinaa. Dhambi zingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe.
Flee fornication. Every other sin which a man may commit, is apart from the body; but he that committeth fornication, sinneth against his own body.
19 Je, hamjui ya kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe,
Know ye not, that your bodies are temples of the Holy Spirit which is in you, which ye have from God, and that ye are not your own?
20 kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
For ye were bought with a price. Therefore glorify God in your body.

< 1 Wakorintho 6 >