< 1 Wakorintho 6 >

1 Kama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu?
Dare any one of you, having a matter against another, prosecute his suit before the unjust, and not before the saints?
2 Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo?
Do ye not then know that the saints shall judge the world? and if the world is judged by you, are ye unworthy of [the] smallest judgments?
3 Hamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya?
Do ye not know that we shall judge angels? and not then matters of this life?
4 Kwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, chagueni kuwa waamuzi, watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kanisa.
If then ye have judgments as to things of this life, set those [to judge] who are little esteemed in the assembly.
5 Nasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waaminio?
I speak to you [to put you] to shame. Thus there is not a wise person among you, not even one, who shall be able to decide between his brethren!
6 Badala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!
But brother prosecutes his suit with brother, and that before unbelievers.
7 Huko kuwa na mashtaka miongoni mwenu ina maana kwamba tayari ni kushindwa kabisa. Kwa nini msikubali kutendewa mabaya? Kwa nini msikubali kunyangʼanywa?
Already indeed then it is altogether a fault in you that ye have suits between yourselves. Why do ye not rather suffer wrong? why are ye not rather defrauded?
8 Badala yake, ninyi wenyewe mwadanganya na kutenda mabaya, tena mwawatendea ndugu zenu.
But ye do wrong, and defraud, and this [your] brethren.
9 Je, hamjui kwamba wasio haki hawataurithi Ufalme wa Mungu? Msidanganyike: Waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wahanithi, wala walawiti,
Do ye not know that unrighteous [persons] shall not inherit [the] kingdom of God? Do not err: neither fornicators, nor idolaters, nor adulterers, nor those who make women of themselves, nor who abuse themselves with men,
10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyangʼanyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.
nor thieves, nor covetous, nor drunkards, nor abusive persons, nor [the] rapacious, shall inherit [the] kingdom of God.
11 Baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Yesu Kristo na katika Roho wa Mungu wetu.
And these things were some of you; but ye have been washed, but ye have been sanctified, but ye have been justified in the name of the Lord Jesus, and by the Spirit of our God.
12 “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini si vitu vyote vyenye faida. “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini sitatawaliwa na kitu chochote.
All things are lawful to me, but all things do not profit; all things are lawful to me, but I will not be brought under the power of any.
13 “Chakula ni cha tumbo, na tumbo ni la chakula”: lakini Mungu ataviangamiza vyote viwili. Mwili haukuumbwa kwa ajili ya zinaa bali kwa ajili ya Bwana na Bwana kwa ajili ya mwili.
Meats for the belly, and the belly for meats; but God will bring to nothing both it and them: but the body [is] not for fornication, but for the Lord, and the Lord for the body.
14 Naye Mungu aliyemfufua Bwana kutoka kwa wafu atatufufua sisi pia kwa uweza wake.
And God has both raised up the Lord, and will raise us up from among [the dead] by his power.
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo mwenyewe? Je, nichukue viungo vya mwili wa Kristo na kuviunganisha na mwili wa kahaba? La hasha!
Do ye not know that your bodies are members of Christ? Shall I then, taking the members of the Christ, make [them] members of a harlot? Far be the thought.
16 Hamjui kwamba aliyeungwa na kahaba anakuwa mwili mmoja naye? Kwa kuwa imenenwa, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
Do ye not know that he [that is] joined to the harlot is one body? for the two, he says, shall be one flesh.
17 Lakini mtu aliyeungwa na Bwana anakuwa roho moja naye.
But he that [is] joined to the Lord is one Spirit.
18 Ikimbieni zinaa. Dhambi zingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe.
Flee fornication. Every sin which a man may practise is without the body, but he that commits fornication sins against his own body.
19 Je, hamjui ya kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe,
Do ye not know that your body is [the] temple of the Holy Spirit which [is] in you, which ye have of God; and ye are not your own?
20 kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
for ye have been bought with a price: glorify now then God in your body.

< 1 Wakorintho 6 >