< 1 Wakorintho 6 >
1 Kama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu?
你们如果与邻居起了纷争,为什么要向不义的法官提交诉状呢?你应该将这件事告知其他信徒。
2 Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo?
难道你们不知道吗?基督信徒将审判世界。如果世界都由你们来审判,怎么就不配审判如此琐碎小事?
3 Hamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya?
你们不知道吗?我们将要审判天使,更何况今世所发生的这种人间之事?
4 Kwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, chagueni kuwa waamuzi, watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kanisa.
如果你需要评判今世之事,怎能让教会并不尊重的人做出审判?
5 Nasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waaminio?
我说的这番话,就是要让你们羞愧。为什么?难道你们中间没有智慧之人,可以审判这样的纷争吗?
6 Badala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!
相反,信徒会跑到法庭状告其他信徒兄弟,向不信上帝之人提交诉状?
7 Huko kuwa na mashtaka miongoni mwenu ina maana kwamba tayari ni kushindwa kabisa. Kwa nini msikubali kutendewa mabaya? Kwa nini msikubali kunyangʼanywa?
你们状告彼此,已经是一个彻头彻尾的灾难。接受这不公正不好吗?为什么不甘心受到欺骗?
8 Badala yake, ninyi wenyewe mwadanganya na kutenda mabaya, tena mwawatendea ndugu zenu.
你们的行为反倒会造成不公正,造成欺骗,而且是针对你们在教会中的信徒同伴。
9 Je, hamjui kwamba wasio haki hawataurithi Ufalme wa Mungu? Msidanganyike: Waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wahanithi, wala walawiti,
你们难道不知道吗?不义之人将无法继承上帝之国,不要被蒙骗!那些淫乱、膜拜神像、奸淫、性变态、同性恋、
10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyangʼanyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.
偷窃、贪婪、酗酒、辱骂人或勒索之人,都不能继承上帝之国。
11 Baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Yesu Kristo na katika Roho wa Mungu wetu.
你们有些人曾经如此,但借由主耶稣基督之名,凭着上帝之灵,你们变得洁净、圣洁和正义。
12 “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini si vitu vyote vyenye faida. “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini sitatawaliwa na kitu chochote.
人们会说:“我有做事自由”,但任何事情都要适可而止。“我有做事的自由”,但绝不会受任何事的掌控!人们说
13 “Chakula ni cha tumbo, na tumbo ni la chakula”: lakini Mungu ataviangamiza vyote viwili. Mwili haukuumbwa kwa ajili ya zinaa bali kwa ajili ya Bwana na Bwana kwa ajili ya mwili.
食物是为了肠胃,肠胃是为了食物,但上帝却会废掉这两者。同样,身体的存在不是为了淫乱,而是为了主而存在。同样,主也是为了身体而存在。
14 Naye Mungu aliyemfufua Bwana kutoka kwa wafu atatufufua sisi pia kwa uweza wake.
上帝凭借其力量让主复活,也要用同样的力量让我们复活。
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo mwenyewe? Je, nichukue viungo vya mwili wa Kristo na kuviunganisha na mwili wa kahaba? La hasha!
你们难道不知道吗?你们的身体就是基督身体的一部分,我们怎么能使用基督的身体,与娼妓的身体苟合?当然不可以!
16 Hamjui kwamba aliyeungwa na kahaba anakuwa mwili mmoja naye? Kwa kuwa imenenwa, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
难道你不知道吗?与娼妓苟合,就是与她成为“一体。”记得经文所说:“两个人要成为一体。”
17 Lakini mtu aliyeungwa na Bwana anakuwa roho moja naye.
但与主结合,就代表与主的灵融为一体
18 Ikimbieni zinaa. Dhambi zingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe.
行淫乱之事。人类所犯罪行都在身体之外,唯有淫乱是对自己身体犯下的罪。
19 Je, hamjui ya kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe,
你们不知道吗?我们体内的圣灵,就住在身体这个圣灵之殿中,这圣灵是你从上帝那里领取的并不属于你自己。
20 kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
你并不属于自己,而是根据标价购买而来。所以要用你的身体为上帝带来荣耀!