< 1 Wakorintho 5 >
1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
Celo se sliši, da je kurbarstvo med vami, in to tako kurbarstvo, kakoršno se tudi med pogani ne imenuje, da ima nekdo ženo svojega očeta.
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
In vi ste napihneni in niste rajši žalovali, da bi se odpravil iz sredi vas tisti, kteri je tako delo storil?
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
Ker jaz kakor nenazoči s telesom ali nazoči z duhom odsodil sem uže kakor nazoči, da se tisti, kteri je tako napravil,
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
V imenu Gospoda našega Jezusa Kristusa, kedar se zberete vi in moj duh, z močjo: Gospoda našega Jezusa Kristusa,
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
Izročí satanu na pogubo mesa, da se duh zveliča na dan Gospoda Jezusa.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
Ni dobra hvala vaša. Jeli ne veste, da malo kvasa vse testo skisa?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Izčistite torej stari kvas, da boste novo testo, kakor ste presni; kajti tudi naša pasha se je za nas zaklala, Kristus.
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
Za to praznujmo ne v starem kvasu hudobe in napačnosti, nego v presnini čistote in resnice.
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
Pisal sem vam v listu, da se ne mešate s kurbarji.
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
In ne sploh s kurbarji tega sveta, ali lakomci, ali roparji, ali malikovalci; kajti drugače bi vam bilo iz tega sveta iti.
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
Sedaj sem vam pa pisal, da se ne mešate, če je ta, kteri se brat imenuje, kurbar, ali lakomec, ali malikovalec, ali psovač, ali pijanec, ali ropar. S takim tudi da ne jeste.
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
Kajti kaj je meni mari, da tudi sodim tiste, kteri so zunej? Ne sodite li vi tistih, kteri so notri?
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
Kteri so pa zunej, tiste sodi Bog. Odpravite hudobnika izmed sebe.