< 1 Wakorintho 5 >

1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
We heard a report that there is sexual immorality among you, a kind of immorality that is not even permitted among the Gentiles. The report is that one of you is sleeping with his father's wife.
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
You are so arrogant! Should you not mourn instead? The one who did this must be removed from among you.
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
For even though I am absent in body, I am present in spirit. I have already passed judgment on the one who did this, just as though I were there.
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
When you are assembled in the name of our Lord Jesus and I am with you in spirit, and the power of our Lord Jesus is present,
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
hand this man over to Satan for the destruction of the flesh, so that his spirit may be saved on the day of the Lord.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
Your boasting is not good. Do you not know that a little yeast leavens the whole loaf?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Cleanse yourselves of the old yeast so that you may be new dough, so that you may be unleavened bread. For Christ, our Passover lamb, has been sacrificed.
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
So let us then celebrate the festival, not with the old yeast, the yeast of bad behavior and wickedness. Instead, let us celebrate with the unleavened bread of sincerity and truth.
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you in my letter not to associate with sexually immoral people.
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
In no way did I mean the immoral people of this world, or the greedy, or swindlers, or idolaters, since to stay away from them you would need to go out of the world.
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
But now I am writing to you not to associate with anyone who is called a brother but who is living in sexual immorality, or who is greedy, or is an idolater, or is verbally abusive, or is a drunkard, or a swindler. Do not even eat a meal with such a person.
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
For how am I involved with judging those who are outside the church? Instead, are you not to judge those who are inside the church?
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
But God judges those who are on the outside. “Remove the evil person from among you.”

< 1 Wakorintho 5 >