< 1 Wakorintho 5 >
1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
In short, it is reported, there is whoredom among you; and such whoredom as is not even named among the heathen, that a son should even take the wife of his father.
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
And ye are inflated, and have not rather sitten down in grief, that he who hath done this deed might be separated from you.
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
And I, while distant from you in body but present with you in spirit, have already, as if present, judged him who perpetrateth this deed;
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
that ye all assemble together, in the name of our Lord Jesus Messiah, and I with you in spirit, together with the energy of our Lord Jesus Messiah;
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
and that ye deliver him over to Satan, for the destruction of the flesh, that in spirit he may have life, in the day of our Lord Jesus Messiah.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
Your glorying is not praiseworthy. Know ye not, that a little leaven leaveneth the whole mass?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Purge out from you the old leaven, that ye may be a new mass, as ye are unleavened. For our passover is the Messiah, who was slain for us.
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
Therefore let us celebrate the festival, not with the old leaven, nor with the leaven of wickedness and bitterness, but with the leaven of purity and sanctity.
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you by letter, not to commingle with whoremongers.
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
But I say not, with the whoremongers who are in the world, nor speak I of the avaricious, or of the rapacious, or of the idol-worshippers, otherwise ye would be obliged to go out of the world.
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
But this is what I wrote to you, that ye commingle not, if any one is called a brother, and is a whoremonger, or avaricious, or an idol-worshipper, or a railer, or a drunkard, or rapacious, with him who is such, not even to eat bread.
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
For what business have I to judge them who are without? But those within the body, judge ye,
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
and those without, God judgeth; and remove ye the wickedness from among you.