< 1 Wakorintho 5 >

1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
Whoredom is actually heard of among you, and such whoredom as is not even named among the nations—as that one has the wife of the father!
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
And you are having been puffed up, and did not rather mourn, that he may be removed out of the midst of you who did this work,
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
for I indeed, as being absent as to the body, and present as to the spirit, have already judged, as being present, him who so worked this thing:
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
in the Name of our Lord Jesus Christ—you being gathered together, also my spirit—with the power of our Lord Jesus Christ,
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
to deliver up such a one to Satan for the destruction of the flesh, that the spirit may be saved in the Day of the Lord Jesus.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
Your glorying [is] not good; have you not known that a little leaven leavens the whole lump?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Cleanse out, therefore, the old leaven, that you may be a new lump, according as you are unleavened, for our Passover was sacrificed for us also—Christ,
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
so that we may keep the celebration, not with old leaven, nor with the leaven of evil and wickedness, but with unleavened [bread] of sincerity and truth.
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you in the letter, not to keep company with whoremongers—
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
and certainly not with the whoremongers of this world, or with the covetous, or extortioners, or idolaters, seeing you ought then to go forth out of the world—
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
and now, I wrote to you not to keep company with [him], if anyone, being named a brother, may be a whoremonger, or covetous, or an idolater, or a railer, or a drunkard, or an extortioner—do not even eat together with such a one;
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
for what have I also to judge those outside? Do you not judge those within?
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
And judge those without God; and put away the evil from among yourselves.

< 1 Wakorintho 5 >