< 1 Wakorintho 4 >

1 Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za Mungu.
Saaledes agte man os: som Kristi Tjenere og Husholdere over Guds Hemmeligheder!
2 Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu.
I øvrigt kræves her af Husholdere, at man maa findes tro.
3 Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu.
Men mig er det saare lidet at bedømmes af eder eller af en menneskelig Ret; ja, jeg bedømmer end ikke mig selv.
4 Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana ndiye anihukumuye.
Thi vel ved jeg intet med mig selv, dog er jeg ikke dermed retfærdiggjort; men den, som bedømmer mig, er Herren.
5 Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
Derfor dømmer ikke noget før Tiden, førend Herren kommer, som baade skal bringe for Lyset det, som er skjult i Mørket, og aabenbare Hjerternes Raad; og da skal enhver faa sin Ros fra Gud.
6 Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine.
Men dette, Brødre! har jeg anvendt paa mig selv og Apollos for eders Skyld, for at I paa os kunne lære dette „ikke ud over, hvad der staar skrevet”, for at ikke nogen af eder for eens Skyld skal opblæse sig mod en anden.
7 Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea?
Thi hvem giver dig Fortrin? og hvad har du, som du ikke har faaet givet? men naar du virkelig har faaet det, hvorfor roser du dig da, som om du ikke havde faaet det?
8 Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi!
I ere allerede mættede, I ere allerede blevne rige, I ere blevne Konger uden os, ja, gid I dog vare blevne Konger, for at ogsaa vi kunde være Konger med eder!
9 Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonyesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia.
Thi mig synes, at Gud har fremstillet os Apostle som de ringeste, ligesom dødsdømte; thi et Skuespil ere vi blevne for Verden, baade for Engle og Mennesker.
10 Kwa ajili ya Kristo sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Kristo. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa.
Vi ere Daarer for Kristi Skyld, men I ere kloge i Kristus; vi svage, men I stærke; I hædrede, men vi vanærede.
11 Mpaka saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao.
Indtil denne Time lide vi baade Hunger og Tørst og Nøgenhed og faa Næveslag og have intet blivende Sted
12 Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili,
og arbejde møjsommeligt med vore egne Hænder. Udskælder man os, velsigne vi; forfølger man os, finde vi os deri;
13 tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Mpaka sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu.
spotter man os, give vi gode Ord; som Verdens Fejeskarn ere vi blevne, et Udskud for alle indtil nu.
14 Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa.
Ikke for at beskæmme eder skriver jeg dette; men jeg paaminder eder som mine elskede Børn.
15 Hata kama mnao walimu 10,000 katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Kristo Yesu kwa kuwaletea Injili.
Thi om I end have ti Tusinde Opdragere i Kristus, have I dog ikke mange Fædre; thi jeg har i Kristus Jesus avlet eder ved Evangeliet.
16 Basi nawasihi igeni mfano wangu.
Jeg formaner eder altsaa, vorder mine Efterfølgere!
17 Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Kristo Yesu, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kanisa.
Derfor har jeg sendt Timotheus til eder, som er mit elskede og trofaste Barn i Herren, og han skal minde eder om mine Veje i Kristus, saaledes som jeg lærer alle Vegne i enhver Menighed.
18 Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu.
Men nogle ere blevne opblæste, i den Tanke, at jeg ikke kommer til eder;
19 Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao.
men jeg skal snart komme til eder, om Herren vil, og gøre mig bekendt, ikke med de opblæstes Ord, men med deres Kraft.
20 Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu.
Thi Guds Rige bestaar ikke i Ord, men i Kraft.
21 Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?
Hvad ville I? Skal jeg komme til eder med Ris eller med Kærlighed og Sagtmodigheds Aand?

< 1 Wakorintho 4 >