< 1 Wakorintho 4 >

1 Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za Mungu.
所以,要把自己看作基督的仆人,为“上帝的奥秘”负责。
2 Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu.
不仅如此,承担这一职责之人,还必须值得信赖。
3 Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu.
无论你或其他人评判我,我都完全不介意。事实上,我甚至也不会评判自己。
4 Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana ndiye anihukumuye.
我不记得自己做过错事,但这并不代表我在道德上称得上良善正直,只有主才能评判我。
5 Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
所以,在恰当时机到来之前——即主降临之前,不要做出任何评判。他将照亮那被隐藏的、最黑暗的秘密,袒露人心里的动机。届时,上帝会给每个人应得的称赞。
6 Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine.
那么,兄弟姐妹们,我用我自己和亚波罗给你们做例子,让你们了解,不要超越经文所记内容,不要自高自大,不要偏爱任何人。
7 Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea?
是什么让你如此特别?你拥有了什么,才让上帝不肯给予你?既然是来自上帝的给予,为什么要傲慢地否认这一点?
8 Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi!
你以为拥有了所需的一切。你以为自己如此富有。你以为自己是王,不再需要我们。我倒真的希望你就是国王,这样我们就可以与你共同为王!
9 Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonyesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia.
在我看来,上帝将我们这些使徒排在队列的最后,作为一种展示,尽管我们也会向其他人一样死去,但那只是我们在整个宇宙面前、在天使和人类面前,演了一场戏。
10 Kwa ajili ya Kristo sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Kristo. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa.
我们是基督的愚人,但与上帝同在的你却如此智慧。我们软弱,你们强壮!你们受人尊敬,我们被瞧不起!
11 Mpaka saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao.
即使是现在,我们仍然饥渴难耐、衣不蔽体、遭受殴打、无处安身。
12 Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili,
我们艰难辛苦地劳作。被人咒骂,我们会为其祝福;遭人迫害,我们会忍受;
13 tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Mpaka sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu.
被人毁谤,我们报以善意。直到现在,人们视我们为泥土、这世上最肮脏的垃圾。
14 Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa.
我写这番话并非让你们羞愧,而是把你们当作我最爱的孩子一样给出警告。
15 Hata kama mnao walimu 10,000 katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Kristo Yesu kwa kuwaletea Injili.
纵然你们有成千上万的基督徒教师,但却没有多少人可以称其为父。因为基督耶稣的缘故,当我与你们分享福音,便可成为你们的父亲。
16 Basi nawasihi igeni mfano wangu.
所以我请求你们,一定要效法我。
17 Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Kristo Yesu, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kanisa.
也正是因为这个原因,我派提摩太去拜访你们。他与主同在,是我最值得信赖、最喜爱的儿子。他将提醒你们我如何追随基督,就像我在各会堂中所作的教导。
18 Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu.
有人以为我不会到他们那里去,于是就变得骄傲自负。
19 Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao.
但只要是主的意愿,我很快就会去往那里。然后了解那些傲慢自负的人都说了什么,知晓他们的能力如何。
20 Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu.
因为上帝之国并不关注言语,而要看能力。
21 Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?
那么你期待什么?让我带着棍子去殴打你,还是带着爱和温柔的灵出现?

< 1 Wakorintho 4 >