< 1 Wakorintho 3 >

1 Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.
Nhune, vakuulu na vanuna vango, nanilyajovile numue heene vana Mhepo, loi ndavule avaana m'biili. Ghwene avaana avadebe ava Kilisite.
2 Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.
Nilyavanywisisie utusiva ni nyama, ulwakuva namukiling'anisie kulia inyama. Nambe lino namuling'anisie.
3 Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?
Ulwakuva umue namulim'bili. Ulwakuva ikilule namatupa ghavonike mulyumwue. Vuuli, namukukala kuling'ana nu m'bili, vuuli, namughenda ndavule vulevule vwa kimuunhu.
4 Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?
Ulwakuva umuunhu jumo iiti, “Nikum'bingilila u Paulo” Ujunge iiti “Nikum'bingilila u Apolo,” namukukala ndavule avaanhu?
5 Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
U Apolo ghwe veeni? nu Paulo ghwe veeni? Avavombili vajuula juno mumwitike, kwa ghweni juno u Mutwa akam'pelile imbombo.
6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
Une nilyavyalile, U Apolo akaponia amalenga looli u Nguluve akakusia.
7 Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
Pa uluo, nakwekuuti juno akavyalile nambe juno alyaponisie amalenga alinikimonga. Looli ghwe Nguluve juno ikusia.
8 Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
Lino juno avalile najuno ikwusilila amalenga vooni valing'ine, najula juno ikwupilagha uluhombo lwa mwene kuling'ana nhi mbombo jamwene.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
Ulwakuva usue tulivavomba mbombo va Nguluve, umwue muli bustani ja Nguluve, lijengo lya Nguluve.
10 Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.
Kuhumilanila nulusungu lwa Nguluve luno nikapelilue heene n'jengaji um'baha, nilyavikile ulwalo, nujunge ijenga pakyanya pa lwene. Looli umuunhu ilolelelaghe ndavule ijenga.
11 Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.
Ulwakuva nakwaele ujunge juno kwandebijenga ulwalo ulunge kukila luno lujengilue, luno ghwe Yesu Kilisite.
12 Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,
1Lino, ndavule un'jinu ghwinu ijenga pakyanya ni sahabu, ni ndalama, namavue gha lutogo, amapiki amasoli, nambe amatundu,
13 kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.
imbombo ja mwene jilya fwikulilue, kulumuli lwa pamwisi jifwikuluagha. Ulwakuva jilifwikulivua nu mwoto. Umwoto ghuli ghelagha uvunono vwa mbombo jino umuunhu ghweni akajivombile.
14 Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.
Ndavule kyoni kino umuunhu ajangile kisighalila umwene ilikwupilagha uluvonolo.
15 Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.
Looli imbombo ja muunhu jingalanguke nu mwooto, naikwambulila kiinu. Looli umwene jujuo ipokuagha, ndavule kusena ku mwotoo
16 Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Namukagula kuuti umue mulinyumba nyimik ja kufunnyila ja Nguluve nakuuti Mhepo ghwa Nguluve ikukala mun'kate mulyumue?
17 Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.
Nave umuunhu angananganie inyumba inyumba ija kufunyila ija Nguluve, u Nguluve ikumunangania umuunhu ujuo. Ulwakuva inyumba inyimike jakufunyila ija Nguluve nyimike, pauluo najumue.
18 Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn g165)
Umuunhu alisyangile mwene, nave jumonga n'kaate mulyumue isaagha kuuti alinuluhala kumasiki agha, avisaghe hweene “N'jasu” apuo peiva nuluhala. (aiōn g165)
19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”
Ulwakuva uluhala lwa mu iisi iji vuyasu pavulongolo pa Nguluve, ulwakuva jilembilue, “Vikolua avanyaluhala nuvuvesi vuvanave”
20 tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”
Kange u Nguluve akagwile amasaghe gha vanyaluhala palivuvule.”
21 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,
Apuo umuunhu nalighiniagha avaanhu! Ulwakuva ifiinu fyoni fiinhu.
22 ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu
Nave ghwe Paulo, nambe u Apolo, nambe u Kefa, nambe iisi, nambe amikalile, nambe vufue, nambe ifinu fino pwefile, nambe fino filyava. Fyooni fiinhu,
23 na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.
Umue mulivakilite va Nguluve.

< 1 Wakorintho 3 >