< 1 Wakorintho 3 >
1 Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.
And I, brethren, could not speak to you as to spiritual, but as to carnal, [even] as to babes in Christ.
2 Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.
I have fed you with milk, and not with meat: for hitherto ye were not able [to bear it], neither yet now are ye able.
3 Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?
For ye are yet carnal: for whereas [there is] among you envying, and strife, and divisions, are ye not carnal, and walk as men?
4 Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?
For while one saith, I am of Paul; and another, I [am] of Apollos; are ye not carnal?
5 Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
Who then is Paul, and who [is] Apollos, but ministers by whom ye believed, even as the Lord gave to every man?
6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
I have planted, Apollos watered: but God hath given the increase.
7 Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
So then, neither is he that planteth any thing, neither he that watereth: but God that giveth the increase.
8 Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
Now he that planteth and he that watereth are one: and every man shall receive his own reward, according to his own labor.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
For we are laborers together with God: ye are God's husbandry, [ye are] God's building.
10 Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.
According to the grace of God which is given to me, as a wise master-builder, I have laid the foundation, and another buildeth upon it. But let every man take heed how he buildeth upon it.
11 Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.
For other foundation can no man lay than that which is laid, which is Jesus Christ.
12 Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,
Now if any man buildeth upon this foundation, gold, silver, precious stones, wood, hay, stubble;
13 kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.
Every man's work will be made manifest: for the day will declare it, because it will be revealed by fire; and the fire will try every man's work, of what sort it is.
14 Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.
If any man's work abideth which he hath built upon it, he shall receive a reward.
15 Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.
If any man's work shall be burned, he will suffer loss: but he himself shall be saved; yet so as by fire.
16 Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Know ye not that ye are the temple of God, and [that] the Spirit of God dwelleth in you?
17 Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.
If any man defileth the temple of God, him will God destroy: for the temple of God is holy, which [temple] ye are.
18 Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn )
Let no man deceive himself. If any man among you seemeth to be wise in this world, let him become a fool, that he may be wise. (aiōn )
19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”
For the wisdom of this world is foolishness with God. For it is written, He taketh the wise in their own craftiness.
20 tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”
And again, The Lord knoweth the thoughts of the wise, that they are vain.
21 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,
Therefore let no man glory in men: for all things are yours:
22 ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu
Whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things to come; all are yours;
23 na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.
And ye are Christ's; and Christ [is] God's.