< 1 Wakorintho 3 >

1 Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.
I also, brethren, was not able to speak to you as to spiritual men, but as those who are not spiritual, as to babes in Christ.
2 Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.
I fed you with milk, not with meat; for ye were not yet able to bear it. Nor indeed are ye able even now;
3 Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?
for ye are yet unspiritual. For while there is among you rivalry and strife, are ye not unspiritual, and walking after the manner of men?
4 Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?
For while one saith, I am of Paul, and another, I am of Apollos, are ye not [[like common]] men?
5 Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
Who then is Apollos, and who is Paul, but ministers through whom ye believed, and that as the Lord gave to each?
6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
I planted, Apollos watered; but God gave the growth.
7 Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
So then, neither he that planteth nor he that watereth is anything, but God that giveth the growth.
8 Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
And he that planteth and he that watereth are one; and each will receive his own reward, according to his own labor.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
For we are God's fellow-laborers; ye are God's field, ye are God's building.
10 Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.
According to the grace of God bestowed on me, I, as a skilful master-builder, have laid the foundation; and another buildeth thereon; but let every one take heed, how he buildeth thereon.
11 Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.
For other foundation can no one lay than that which is laid, which is Christ Jesus.
12 Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,
But if any one build upon this foundation with gold, silver, precious stones, wood, hay, stubble,
13 kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.
the work of every one will be made manifest; for the day will show it; because it is revealed in fire; and the fire itself will prove what every one's work is.
14 Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.
If the work which any one built thereon remaineth, he will receive reward;
15 Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.
if any one's work shall be burned up, he will lose the reward; but he will be saved himself, yet as one escaping through fire.
16 Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Know ye not, that ye are God's temple, and that the Spirit of God dwelleth in you?
17 Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.
If any one defaceth the temple of God, God will deface him; for the temple of God is holy, and such are ye.
18 Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn g165)
Let no one deceive himself; if any one thinketh himself wise among you in this world, let him become a fool, that he may become wise. (aiōn g165)
19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”
For the wisdom of this world is foolishness with God; for it is written: “He that taketh the wise in their craftiness;”
20 tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”
and again: “The Lord knoweth the thoughts of the wise, that they are vain.”
21 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,
So then let no one glory in men. For all things are yours;
22 ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu
whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things to come, —all are yours;
23 na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.
and ye are Christ's, and Christ is God's.

< 1 Wakorintho 3 >