< 1 Wakorintho 3 >

1 Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.
And so, brothers, I was not able to speak to you as if to those who are spiritual, but rather as if to those who are carnal. For you are like infants in Christ.
2 Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.
I gave you milk to drink, not solid food. For you were not yet able. And indeed, even now, you are not able; for you are still carnal.
3 Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?
And since there is still envy and contention among you, are you not carnal, and are you not walking according to man?
4 Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?
For if one says, “Certainly, I am of Paul,” while another says, “I am of Apollo,” are you not men? But what is Apollo, and what is Paul?
5 Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
We are only the ministers of him in whom you have believed, just as the Lord has granted to each of you.
6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
I planted, Apollo watered, but God provided the growth.
7 Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
And so, neither he who plants, nor he who waters, is anything, but only God, who provides the growth.
8 Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
Now he who plants, and he who waters, are one. But each shall receive his proper reward, according to his labors.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
For we are God’s assistants. You are God’s cultivation; you are God’s construction.
10 Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.
According to the grace of God, which has been given to me, I have laid the foundation like a wise architect. But another builds upon it. So then, let each one be careful how he builds upon it.
11 Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.
For no one is able to lay any other foundation, in place of that which has been laid, which is Christ Jesus.
12 Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,
But if anyone builds upon this foundation, whether gold, silver, precious stones, wood, hay, or stubble,
13 kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.
each one’s work shall be made manifest. For the day of the Lord shall declare it, because it will be revealed by fire. And this fire will test each one’s work, as to what kind it is.
14 Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.
If anyone’s work, which he has built upon it, remains, then he will receive a reward.
15 Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.
If anyone’s work is burned up, he will suffer its loss, but he himself will still be saved, but only as through fire.
16 Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Do you not know that you are the Temple of God, and that the Spirit of God lives within you?
17 Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.
But if anyone violates the Temple of God, God will destroy him. For the Temple of God is holy, and you are that Temple.
18 Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn g165)
Let no one deceive himself. If anyone among you seems to be wise in this age, let him become foolish, so that he may be truly wise. (aiōn g165)
19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”
For the wisdom of this world is foolishness with God. And so it has been written: “I will catch the wise in their own astuteness.”
20 tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”
And again: “The Lord knows the thoughts of the wise, that they are vain.”
21 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,
And so, let no one glory in men.
22 ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu
For all is yours: whether Paul, or Apollo, or Cephas, or the world, or life, or death, or the present, or the future. Yes, all is yours.
23 na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.
But you are Christ’s, and Christ is God’s.

< 1 Wakorintho 3 >