< 1 Wakorintho 2 >

1 Ndugu zangu nilipokuja kwenu, sikuja na maneno ya ushawishi wala hekima ya hali ya juu nilipowahubiria siri ya Mungu.
Ka püie aw, nami veia law lü, ngthupkia Pamhnama ngthungtak ka ning ja mtheh üng, ngthu mpyawng mahnak ja ksingnak am sumei veng.
2 Kwa kuwa niliamua kutokujua kitu chochote wakati nikiwa nanyi isipokuwa Yesu Kristo aliyesulubiwa.
Jesuh Khritaw kutlamktung üng taiha ngthua thea nami veia ka, ka ksing vai am ve.
3 Mimi nilikuja kwenu nikiwa dhaifu na mwenye hofu na kwa kutetemeka sana.
Nangmia vei ka law üng ktha ngcek lü cäi lü ngkhyet veng.
4 Kuhubiri kwangu na ujumbe wangu haukuwa kwa hekima na maneno ya ushawishi bali kwa madhihirisho ya nguvu za Roho
Ka pyen ja ka mtheimthangnak cun nghngicima khyaihnaka ngthu üng pyena am kya lü, Pamhnama Ngmüimkhya ja johit üng ni akya ve.
5 ili imani yenu isiwe imejengwa katika hekima ya wanadamu bali katika nguvu za Mungu.
Nami jumnak cun Pamhnama johita kya lü nghngicima ksingnaka am kya.
6 Lakini miongoni mwa watu waliokomaa twanena hekima, wala si hekima ya ulimwengu huu au ya watawala wa dunia hii wanaobatilika. (aiōn g165)
Jumeinak üng dämduh pängki veia pumngyam mah akba kami ngthukhyüki. Ahina pumngyam cun khawmdek upkiea asäng üng khyük be theikia khawmdek pumngyam am ni. (aiōn g165)
7 Sisi tunanena hekima ya Mungu ambayo ni siri, tena iliyofichika, ambayo Mungu aliikusudia kabla ya ulimwengu kuwepo, kwa ajili ya utukufu wetu. (aiōn g165)
Khawmdek am a ngtün law ham üngka naw mi hlüngtainak vaia axü päng, acun cun khyang üngka naw ngthupkia Pamhnam pumngyam ni kami sang ta. (aiōn g165)
8 Hakuna hata mtawala mmoja wa nyakati hizi aliyeelewa jambo hili. Kwa maana kama wangelielewa, wasingemsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn g165)
Acun cun hina khawmdek upkie naw am ksing u, ami ksing vai sü ta hlüngtainaka Bawipa kutlamktung üng am ami taih vai sü. (aiōn g165)
9 Lakini ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna jicho limepata kuona, wala sikio limepata kusikia, wala hayakuingia moyoni wowote, yale Mungu amewaandalia wale wampendao”:
“Mik üng am hmuh, hnga üng am ngjak, nghngicima mlung üng am lutki, Pamhnam naw ani mhläkphyanakiea phäha a pitpyang ni” tia Cangcim naw pyenki.
10 Lakini mambo haya Mungu ametufunulia kwa Roho wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani sana ya Mungu.
Mimi cun, acuna ngthu Pamhnama Ngmüimkhya naw jah ksingsaki ni. Ngmüimkhya naw avan naküt cun suihjap lü, Pamhnama ngthupkia nümnak pi ksing theiki.
11 Kwa maana ni nani anayejua mawazo ya mtu isipokuwa roho iliyo ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu ajuaye mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
Mi Ngmüimkhya naw ni, mi mäta mawng a ksing. Acuna mäiha Pamhnama Ngmüimkhya naw ni Pamhnama mawng a ksing ta.
12 Basi hatukupokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, ili tuweze kuelewa kile kipawa ambacho Mungu ametupatia bure.
Acunakyase, khawmdeka ngmüimkhya am mi yaki. Pamhnama a jah pete mi jah ksingnak thei vaia Pamhnama veia ka, Pamhnama Ngmüimkhya mi yahki.
13 Haya ndiyo tusemayo, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya wanadamu bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua kweli za kiroho kwa maneno ya kiroho.
Cuna kyalü Ngmüimkhya takie, Ngmüimkhya üng sängki kami jah mtheha kba kami khyübe hin khyanga themnak naw a jah mthei am pyen lü Ngmüimkhya a jah mthei khyübe ni kami pyen.
14 Mtu ambaye hana Roho hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa upambanuzi wa rohoni.
Pamhnama Ngmüimkhya üngkhyüh lawki letsawnge cun Ngmüimkhya am taki naw am doei thei. Ngmüimkhya am taki naw acubange cun akcanga am jah ksing lü i ja pi am jah ngai, isetikyaküng amimi cun Ngmüimkhya lam üng jah msuimsäpa kya se ni.
15 Mtu wa kiroho hubainisha mambo yote, lakini yeye mwenyewe habainishwi na mtu yeyote.
Ngmüimkhya khyang cun naw avana ngthumkhyah theiki, acunsepi, ani cun u naw ngthu am mkhya thei.
16 “Kwa maana ni nani aliyefahamu mawazo ya Bwana ili apate kumfundisha?” Lakini sisi tunayo mawazo ya Kristo.
U naw, Bawipaa mlung ksingki ni? U naw a dawnak vai mtheh thei khai ni? Mimi cun Khritawa mlung mi taki.

< 1 Wakorintho 2 >