< 1 Wakorintho 16 >
1 Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo.
Touchant la collecte qui se fait pour les Saints, faites comme j'en ai ordonné aux Eglises de Galatie.
2 Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango.
C'est que chaque premier jour de la semaine, chacun de vous mette à part chez soi, ce qu'il pourra assembler suivant la prospérité [que Dieu lui accordera], afin que lorsque je viendrai, les collectes ne soient point à faire.
3 Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu.
Puis quand je serai arrivé, j'enverrai ceux que vous approuverez par vos Lettres pour porter votre libéralité à Jérusalem.
4 Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.
Et s'il est à propos que j'y aille moi-même, ils viendront aussi avec moi.
5 Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia.
J'irai donc vers vous, ayant passé par la Macédoine; car je passerai par la Macédoine.
6 Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo.
Et peut-être que je séjournerai parmi vous, ou même que j'y passerai l'hiver; afin que vous me conduisiez partout où j’irai.
7 Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda.
Car je ne vous veux point voir maintenant en passant, mais j'espère que je demeurerai avec vous quelque temps, si le Seigneur le permet.
8 Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste,
Toutefois je demeurerai à Ephèse jusqu'à la Pentecôte.
9 kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.
Car une grande porte, [et de grande] efficace m'y est ouverte, mais il y a plusieurs adversaires.
10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo.
Que si Timothée vient, prenez garde qu'il soit en sûreté parmi vous; car il s'emploie à l'œuvre du Seigneur comme moi-même.
11 Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.
Que personne donc ne le méprise; mais conduisez-le en toute sûreté, afin qu'il vienne me trouver; car je l'attends avec les frères.
12 Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.
Quant à Apollos notre frère, je l'ai beaucoup prié d'aller vers vous avec les frères, mais il n'a nullement eu la volonté d'y aller maintenant: toutefois il y ira quand il en aura la commodité.
13 Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari.
Veillez, soyez fermes en la foi, portez-vous vaillamment, fortifiez-vous.
14 Fanyeni kila kitu katika upendo.
Que toutes vos affaires se fassent en charité.
15 Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi,
Or, mes frères, vous connaissez la famille de Stéphanas, [et vous savez] qu'elle est les prémices de l'Achaïe, et qu'ils se sont entièrement appliqués au service des Saints;
16 mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii.
Je vous prie de vous soumettre à eux, et à chacun de ceux qui s'emploient à l'œuvre [du Seigneur], et qui travaillent avec nous.
17 Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu.
Or je me réjouis de la venue de Stéphanas, de Fortunat, et d'Achaïque; parce qu'ils ont suppléé à ce que vous ne pouvez pas faire pour moi.
18 Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.
Car ils ont recréé mon esprit et le vôtre: ayez donc de la considération pour de telles personnes.
19 Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana.
Les Eglises d'Asie vous saluent. Aquilas et Priscille, avec l'Eglise qui [est] en leur maison, vous saluent affectueusement en [notre] Seigneur.
20 Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
Tous les frères vous saluent. Saluez-vous l'un l'autre par un saint baiser.
21 Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.
La salutation [est] de la propre main de moi Paul.
22 Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.
S'il y a quelqu'un qui n'aime point le Seigneur Jésus-Christ, qu'il soit anathème, Maranatha.
23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous!
24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.
Mon amour s'étend à vous tous en Jésus-Christ. Amen.