< 1 Wakorintho 16 >

1 Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo.
Concerning now the collection which [is] for the saints as I have directed the churches of Galatia, so also you yourselves do perform.
2 Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango.
Every first (Sabbath *N(k)O*) each of you aside of his own should put treasuring up (which one *NK(o)*) (maybe *N(k)O*) he shall be successful, so that not when I may come then collections there may be.
3 Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu.
When then I may have arrived, whomever (maybe *NK(o)*) you shall approve, with letters these I will send to carry the bounty of you to Jerusalem;
4 Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.
If then suitable it shall be for me also me also to go, with me myself they will go.
5 Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia.
I will come however to you when Macedonia I may have gone through; Macedonia for I am going through,
6 Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo.
With you then possibly (I will continue *NK(o)*) or even I will winter, so that you yourselves me may equip wherever if I shall go.
7 Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda.
Not I want for you now in passing to see; I hope (for *N(k)O*) a time certain to remain with you, if the Lord (shall permit. *N(k)O*)
8 Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste,
(I will remain *NK(o)*) however in Ephesus until Pentecost;
9 kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.
A door for to me has opened great and productive and are opposing many.
10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo.
If now may come Timothy, do see that without fear he shall be with you; the for work of [the] Lord he is doing as also I myself. also I myself.
11 Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.
Not anyone therefore him may despise; do equip however him in peace, so that he may come to me; I am expecting for him with the brothers.
12 Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.
Concerning now Apollos the brother, greatly I exhorted him that he may go to you with the brothers; and at all not was [his] will that now he may come, he will come however when he may have opportunity.
13 Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari.
do watch, do stand firm in the faith, do act like men, do be strong.
14 Fanyeni kila kitu katika upendo.
All things of you in love should be done.
15 Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi,
I exhort now you, brothers; you know the house of Stephanas that it is firstfruit of Achaia and to service to the saints they have devoted themselves;
16 mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii.
that also you yourselves may be subject to such as these and to everyone who is joining in the work and laboring.
17 Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu.
I rejoice however at the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus, because (your *N(k)O*) deficiency these filled up;
18 Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.
They refreshed for my spirit and yours. do recognize therefore such as these.
19 Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana.
Greet you the churches of Asia. (he greets *N(K)O*) you in [the] Lord heartily Aquila and (Prisca *N(k)O*) with the at house of them church.
20 Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
Greet you the brothers all. do greet one another with a kiss holy.
21 Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.
The greeting by my own hand of Paul;
22 Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.
If anyone not loves the Lord (Jesus Christ *K*) he should be accursed. (Marana tha! *N(k)O*)
23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
The grace of the Lord Jesus (Christ *K*) [be] with you.
24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.
The love of Mine [be] with all you in Christ Jesus. (Amen *KO*) (to Corinthians first it was written from Philippi through of Stephanas and Fortunatus and Achaicus and Timothy. *K*)

< 1 Wakorintho 16 >